Posts

Showing posts from September 13, 2017

Lusekelo: Tusimtumie Lissu kupata umaarufu

Image
 Mchungaji Lusekelo ameandika ujumbe huo kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii na kusema kuwa mbona watu hao hawakuonekana kulaani mauaji ya Kibiti au kuitisha maombezi baada ya watu Kibiti kuuawa. "Tusitumie tatizo la ndugu yetu Tundu lissu kujipatia umaarufu wa kisiasa au wakidini, mtu yeyote ambaye anatumia tukio hili kujipatia umaarufu wa kisiasa au wakidini namfananisha na wale wahuni ambao basi likianguka anaenda kuchukua simu kwanza, ni jambo ovu sana wewe unakuwa ni sehemu ya watu walio mpiga risasi Tundu lissu. Mwenzako anaumwa wewe unatumia ugonjwa wake kujipatia umaarufu wa kidini au wakisiasa ni jambo baya sana, mbona sikusikia wakilaani mauaji ya kibiti au kuitisha maombezi watu wakibiti walipo uwawa, mbona hawaja laani utekaji na mauaji ya watoto Arusha hata wa Marekani (umoja wa ulaya) sikusikia wanalaani mauaji ya kibiti" aliandika Mzee wa Upako Aidha Mchungaji huyo amesema kuwa yeye anaamini watu hao wanatumia matatizo ya Tundu Lissu

Man U, PSG, Barcelona na Chelsea Zaua Ligi ya Mabingwa Ulaya

Image
Mchezo ukiendelea wa Ligi ya Mabingwa Ulaya  Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Manchester na Basel. MANCHESTER United imerejea kwa nguvu katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Basel, kama ilivyo kwa wababe wa Hispania, Barcelona waliopata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Juventus. Msimu wa 2017/18 wa michuano hiyo hatua ya makundi ulifunguliwa usiku wa kuamkia leo ambapo kulikuwa na mechi nyingi kwenye viwanja tofauti huu vigogo wengi wakiibuka na ushindi. Fellaini akishangilia baada ya kutupia bao la kwanza kwa Man Utd. MANCHESTER UNITED 3- 0 BASEL Ikicheza kwenye uwanja wake wa Old Traff ord, United ilipata ushindi huo muhimu katika Kundi A, mpira ukiwekwa wavuni na Marouane Fellaini dakika ya 35 na Romelu Lukaku dakika ya 53, mabao yote yakifungwa kwa kichwa huku Marcus Rashford akitokea benchi na kuifungia timu yake bao la tatu. Katika mchezo huo, kiungo wa United, Paul Pogba aliyekuwa nahodha wa kikosi chake aliumia da