Posts

Showing posts from November 19, 2017

BREAKING NEWS: MUGABE ANG’OLEWA UENYEKITI WA ZANU-PF

Image
Chama tawala nchini Zimbabwe, ZANU-PF, kimemtimua Rais Robert Mugabe, kwenye uenyekiti wa chama na kumteua aliyekuwa Makamu wa Rais kabla ya kufutwa kazi na Mugabe, Emerson Mnangagwa kuongoza chama hicho.Anatakiwa ajiuzulu mwenyewe urais au kung’olewa madarakani kwa lazima kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na Bunge la nchi hiyo. Vilevile chama tawala ZANU-PF kimemfutia uanachama mke wa Rais Mugabe, Grace Mugabe. Hatua hiyo inamnyang’anya moja kwa moja cheo cha uenyekiti wa Baraza la Wanawake la chama hicho. Kikao cha Kamati Kuu ya chama tawala nchini Zimbabwe, ZANU-PF kinaendelea muda huu huku lengo ni kumng’oa madarakani Rais Robert Mugabe aliyedumu kwa miaka 37. Washiriki wa karibu wa Rais Robert Mugabe katika chama alichokianzisha wamemtaka kiongozi huyo kuondoka madarakani kufuatia shinikizo kubwa la maandamano linaloendelea nchini humo sanjari na jeshi kuingilia kati. Katika kikao hicho kinachoendelea leo, Novemba 19, viongozi wa juu wa chama hich

Haya Ndio Madhara 6 Ya Kutoa Mimba

Image
Kutoa mimba ni nini? Hii ni hali ya mwanamke kwa hiari yake mwenyewe kuharibu mimba iliyoingia ndani ya kizazi chake. Kutokana kuongezeka kwa idadi ya mahusiano duniani na kutotumia njia za uzazi wa mpango kwa watu wengi walioko kwenye mahusiano, wasichana wengi kwa sasa wanatoa mimba. Utafiti nilioufanya mwenyewe nimegundua kwamba zaidi ya asilimia tisini ya wasichana wanaokua kwenye mahusiano na wanaume zaidi ya mwaka mmoja kabla ya ndoa hutoa mimba na asilimia tano tu ya wote ndio wanaamua kuzaa. Sio ajabu kusikia mtu ameolewa akiwa ametoa mimba nne mpaka tano. Sasa unajiuliza bado kuna mtu humo au mfu? Hata hivyo hao wanaozaa pia hujikuta wamebeba mimba zingine wakati watoto wao wakiwa wadogo na kulazimika kuzitoa. Najua watu wengi wanatoa mimba kukwepa aibu, kutokua tayari kisaikolojia na kadhalika lakini ni bora kutumia njia za uzazi wa mpango kama condomu kuzuia mimba na kama kondomu huiwezi basi tumia njia zingine kama sindano na vijiti kwasababu wengi w

BONGO MOVIE NIAJE, WALIMSUSA LULU AU?

Image
KUNA mambo katika maisha siyo kanuni, lakini utamaduni umeyafanya kuwa kama ndiyo utaratibu. Na haya yako mengi kutegemea na mila za kila jamii. Huwezi kushtakiwa kwa kutokufanya, lakini wanaojumuika na wewe watakesha wakikushangaa. Jirani yako akipatwa na matatizo, siyo lazima ujitoe na kumsaidia kwa wakati huo, lakini utamaduni wetu unakuona mtu wa ajabu kama ikikutokea hivyo, halafu wewe badala ya kujumuika naye kwa kumfariji, unaalika watu wa ngoma na kufurahi pamoja nao. Hali iko hivyo kwa wafanyakazi wa ofisi moja, wa tasnia moja na hata watu wanaotoka jamii moja.Kwa mfano, watu wa makabila tofauti kutoka mikoa mbalimbali, wanapokutana katika mkoa au wilaya moja huwa kama ndugu na mmoja wao anapopatwa na matatizo au kuwa na shughuli, wengi hutazamiwa kuwepo. Katika eneo kama hilo, ingawa huwezi kumpeleka mtu kortini, lakini inapotokea mmoja anashindwa kuhudhuria shughuli hiyo, huonekana kama msaliti kwa wenzake, kitu ambacho kistaarabu kinatia doa. Na kushir

MANCHESTER UNITED WAITANDIKA NEWCASTLE BAO 4,POGBA NA ZLATAN WAKIREJEA

Image
      MANCHESTER UNITED (4-1-4-1): De Gea 6; Valencia 6.5, Smalling 7, Lindelof 5.5, Young 7; Matic 6.5; Rashford 6, Mata 7.5 (Herrera 83), Pogba 8 (Fellaini 70 6), Martial 7 (Ibrahimovic 77 6); Lukaku 7 77) SUBS UNUSED: Romero, Rojo, Lingard, Herrera, Shaw GOALS: Martial, Smalling, Pogba, Lukaku BOOKED: Smalling NEWCASTLE (4-4-2): Elliot 6; Yedlin 6.5, Clark 6.5, Lejeune 6.5, Manquillo 6; Murphy 6, Shelvey 7, Hayden 6.5, Ritchie 6.5 (Aarons 66 6); Joselu 5.5 (Mitrovic 71 5.5), Gayle 6.5 (Diame 77 6) SUBS UNUSED: Diame, Perez, Mbemba, Darlow, Gamez GOAL: Gayle BOOKED: Hayden REFEREE: Craig Pawson

Amtosa Mumewe Ulaya, Achukuliwa na Kiserengeti cha Gambia

Image
Mama mwenye watoto tisa Heidi Hepworth (44) akiwa na mpenzi wake wa sasa Mamadou Jallow. MWANAUME mmoja mkazi wa Uingereza Andy Hepworth, amesimulia kwa huzuni jinsi mkewe Heidi Hepworth (44) alivyomtosa, akamwachia watoto tisa na hivi sasa anajirusha na kivulana cha kutoka Gambia, Afrika. Mwanamke huyo anaishi na kijana huyo anayejulikana kama Mamadou Jallow (30) baada ya kufahamiana kupitia Mtandao wa Facebook ambapo aliamua kumfuata hukohuko Gambia na mpaka sasa anaishi naye huko. Jinsi alivyokolewa na mapenzi hayo mapya, sasa Heidi anadai talaka na kusema kuwa amempata ampendaye zaidi. …Enzi ya ndoa yao na mume wake Andy. “Ni jambo la ajabu, alianza tabia ambazo sikuzifahamu. Alianza kwenda gym, akakodisha vitanda maalum vya kuotea jua kwenye fukwe, akaanza kujichora tattoo na kuvaa nguo za ajabu,” anasema Hepworth na kuongeza: “Amekuwa mtu wa ovyo. Mwanzoni alikuwa mama mwenye upendo na anayejua majukumu yake. Hivi sasa ni kama shetani ameukamata m

Alietajwa kufariki ajali ya ndege kumbe yupo hai

Image
Mfanyakazi wa hoteli za kitalii za andBeyond Serengeti, Moses Muhina aliyetajwa kuwa ni miongoni mwa abiria waliofariki dunia katika ajali ya ndege ya Shirika la Coastal Aviation, imebainika alibadili ndege muda mfupi kabla ya safari ili kuwahi kazini. Muhina ambaye ni mwongozaji watalii katika hoteli hiyo, alikuwa aondoke na ndege ya Coastal Aviation saa nne asubuhi lakini viongozi wa hoteli walimbadilishia ndege, hivyo aliondoka na Air Exel iliyofika salama Serengeti. Akizungumza na gazeti hili, meneja uendeshaji wa Hoteli ya andBeyond Serengeti Under Canvas, Mussa Matala alisema Muhina ambaye anasomeka kwenye orodha ya ndege kama Maina alikuwa apande ndege hiyo lakini walimbadilishia. Alisema waliomba aondolewe kwenye orodha ya wasafiri wa ndege hiyo lakini kwa bahati mbaya hadi ndege ilipoondoka jina lake lilikuwapo. Wakati huohuo, raia watano wa kigeni ambao walifariki dunia katika ajali hiyo, akiwamo rubani Dewald Raubenheimer raia wa Afrika Kusini, ambay

Uwoya Roho Mkononi Rwanda! Anaswa na Mabaunsa

Image
Muigizaji Irene Uwoya Siku chache baada ya Hamad Ndikumana ‘Katauti’ kufariki dunia, imedaiwa kuwa, usalama wa mzazi mwenziye marehemu, muigizaji Irene Uwoya ambaye jana alikwea ‘pipa’ kwenda kuhani msiba nchini Rwanda ni mdogo. Uwoya ambaye alifunga ndoa na marehemu na kuishi naye kwa miaka kadhaa kabla ya kutengana, alianza kufanya mipango ya safari Jumatano iliyopita, saa chache mara baada ya kupokea taarifa za kifo hicho kilichotokea Jumanne usiku. CHANZO CHAFUNGUKA Kwa mujibu wa chanzo makini kutoka Rwanda, kuna kikundi cha watu ambacho kimekuwa na hasira na mrembo huyo kwa kile wanachofikiri kuwa kifo cha Ndikumana kimetokana na ‘stress’ zilizosababishwa na mrembo huyo. “Kwa kweli huku usalama wa Uwoya ni mdogo sana maana kama unavyojua kuna mashabiki ambao walikuwa wanamkubali Ndikumana ambaye alikuwa na mchango mkubwa sana katika soka la Rwanda,” kilidai chanzo hicho. WANAAMINI UWOYA NDIYO KIKWAZO Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, wanac