Posts

Showing posts from June 6, 2013

HISTORIA MPYA YAANDIKWA HATIMAYE NGWEA AZIKWA NA MAELFU YA WATU KWENYE MAKABURI YA KIHONDA MKOANI MOROGORO....

Image
PICHA ZA MAZIKO YAKE                                                                          HII NDO NYUMBA YA MILELE YA NGWEAR.   Baada ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, Albert Mangweha aka Ngwair leo amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao. Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri.    Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita. Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.“Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa sana ni umati usioelezeka mungu akulaze mahali pema peponi,” ameandika Izzo B kwenye...

M 2 THE P AKILIA KWA UCHUNGU WAKATI WA KUMUAGA ALBERT NGWEA MOROGORO MCHANA HUU

Image
                                                          M2  THE P amefanikiwa  kutoa  salamu zake  za  mwisho  kwa  rafiki yake  kipenzi  ambaye  alikuwa  naye  huko  Afrika  kusini  tena  walikuwa  ndani  ya  chumba  kimoja  kabla ya  mauti  kumkuta Ngwea....!! Mwanzoni, M 2 THE P alikuwa  amefichwa  na  kudanganywa  kuwa  Ngwea  alikuwa  ametangulia  Tanzania. Baadaye  Maggie  alilazimika  kumweleza  ukweli...... ... TUPE MAONI YAKO 

UPDATES KUTOKA MOROGORO: WAKAZI WAANZA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MANGWEA

Image
  Mama Mzazi wa Mangweha, Denisia Mangweha akiwa nyumbani kwake kabla ya safari kuelekea Uwanja wa Jamhuri. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akiwasili nyumbani kwa Mama mzazi wa Mangweha.   PATA HABARI KAMILI>>>>>>>

BREAKING NEWS: M 2THE P AWASILI TANZANIA KWA AJILI YA KUMZIKA NGWAIR, SIKILIZA HAPA ALICHOKISEMA AKIWA BONGO

Image
Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya leo (June 6).Akizungumza na Times Fm asubuhi hii Mgaza Pende a.k.a M 2 The P amewashukuru watanzania kwa kumuombea japo hali yake bado haijawa nzuri sana lakini ameamua kurudi Tanzania kuja kumzika ndugu yake Mangwea.   PATA HABARI KAMILI>>>>>>>

PICHA ZAIDI MAANDALIZI YA KUAGWA ALBERT MANGWEA MKOANI MOROGORO

Image
Meza kuu hii ikiwa ni maandalia ya kuuwaga mwili wa msanii marehemu Albert Mangwea aliyefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo mkoani morogoro.Utaratibu huu umeandaliwa katika uwanja wa jamuhuri mkoani morogoro kwa lengo la kuwapa fursa wakazi wa mji huo kupata nafasi za kuuwaga mwili huo kabla ya maziko   PATA HABARI KAMILI>>>>>>>

MUME WA KHADIJA KOPA AFARIKI DUNIA

Image
                                      Khadija Omar Kopa akiwa na mumewe Jaffari Ally enzi za uhai wake.Mume wa Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki, Khadija Omar Kopa, aitwaye Jaffari Ally amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.    Marehemu alikuwa anasumbuliwa na matatizo katika mfumo wa upumuaji na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika hospitali ya wilaya Bagamoyo.   Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN. ...

M 2 THE P AKIWA SOUTH AFRICA NA WAKATI HUO HAJUI CHOCHOTE KUHUSU NGWEA ,,

Image
M2 the P alipotembelewa na huyu sister anayeitwa Magie aliyeenda kumjulia hali baada ya msanii huyo kutoka hospitali Msanii M2 the P aliyekutwa mahuhuti pamoja na Ngwair ambaye alifariki, anaendelea vizuri kiafya na ameshatoka hospitali. Mpaka sasa M To The P hajui kama Mangwea amefariki na anadhani mwenzake ametangulia kwenda Dar es Salaam. “Hapo Magie anamtania ikabidii amyeyushe eti ukirudi bongo mwambie Mangwea nina case nae yakuondoka bila SOMA ZAIDI >>>>>>>

PICHA NATUKIO YALIYOJIRI KWENYE SEND OFF YA FROLA MVUNGI ILIYOFANYIKA JANA

Image
Msanii H.Baba akiwa na bestman wake wakiwa kwenye sendoff ya mke wake mtarajiwa SOMA ZAIDI >>>>>>>

HAIKUWA KAZI RAHISI KUINGIA MOROGORO KUTOKANA NA UMATI WA WATU ULIOFURIKA NJIANIW

Image
Msafara wa kupokea mwili wa msanii  marehemu Albert Mangwea ukiwa unaingia morogoro hapa ni eneo la nane nane,Umati mkubwa umejitokeza katika mapokezi hayo jioni ya leo Wakazi wa Morogoro wakikimbilia gari lililobeba mwili wa marehemu huku wakiimba nyimbo zake      MAPOKEZI YA MWILI WA NGWEA ENEO LA MAZIMBU ROAD KIHONDA KUELEKEA NYUMBANI KWAO MANGWEAR

KUTOKANA NA HALI YA MSHITUKO WATU ZAIDI YA SITA WAZIMIA WAKATI WAKIAGA MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA.

Image
WATU sita wameanguka na kupoteza fahamu wakati wa kuuaga mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania katika viwanja vya Leaders Club, watu hao ni wanawake wanne na wanaume wawili na wanaendelea kupewa huduma ya kwanza kutoka kwa kik osi cha msalaba mwekundu waliopo katika viwanja hivi na kuwapa huduma ya kwanza. Mwandishi wa Habarimpya.com akiwa katika viwanja hivyo jijini Dar es Salaam anasema kwamba umati mkubwa umezidi kuongezeka katika viwanja hivyo huku vilio vikitawala. Wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya wakiongozwa na msanii maarufu Abdul Nassib (Diamond Platinumz) wamejitokeza kwa wingi katika tukio hilo kihistoria katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya. Akizungumza na Habarimpya.com katika viwanja hivyo msanii aliyewahi kutamba na kibao chake cha kwanza cha Zeze langu T.I.D ambaye kwa sasa anatamba na Bendi yake ya muziki ya Top Band amesema kwamba, "Kuna mipango mingi tulipanga na Mangwea lakini leo nasikitika sana k

MAELFU NA MAELFU YA WATU WAJITOKEZA MPENDWA WETU ALBERT NGWEA.....SALAMU ZA MWISHO ZIMEANZA KUTOLEWA

Image
Diamond Platnumz akipita mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Albert Mangwea kutoa heshima zake za mwisho. Rais wa Chama cha Wanamuziki Nchini Tanzania akitoa neno la Shukurani kwa wananchi walifanikisha shughuli nzima maelfu ya wananchi wakielekea kutoa heshima zao za mwisho Mwili wa marhemu Albert Mangwea ukiwa kwenye jeneza tayari kwa watu kutoa heshima za mwisho Umati wa watu wakiwa wamepanga mstari tayari kwa kwenda kuaga huku kikosi cha msalaba mwekundu na polisi kikiwa stand by. Baadhi ya wasanii wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga. hili ndo gari maalumu la kusafirisha mwili wa marehemu toka dar es saalam mpaka mkoani morogoro

BAADHI YA WASANII NA WATU MAARUFU WAKIWA WAMEPANGA MSTARI TAYARI KABISA KWA AJILI YA KUMUAGA MANGWAIR

Image
Mwili wa marhemu Albert Mangwea ukiwa kwenye jeneza tayari kwa watu kutoa heshima za mwisho Baadhi ya ma super star wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga.