Posts

Showing posts from October 9, 2017

Wivu wa Mapenzi Wasababisha Mauaji ya Kinyama ya Watu wawili

Image
Watu wawili wamefariki dunia na mwingine mmoja kujijeruhi baada ya kutokea ugomvi unaohusishwa na wivu wa mapenzi mjni Bunda. Tukio hilo lilitokea jana saa tano asubuhi katika Mtaa wa Bunda Stoo baada ya mtu mmoja kuwavamia watu wawili kisha kuwachoma visu kabla ya kujichoma mwenyewe. Akizungumza mjini hapa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed alisema jana kuwa waliouawa ni Daudi Phares (29) mkazi wa Bunda na msichana aliyetambulika kwa jina moja la Monica (22) mkazi wa Magu mkoani Mwanza. Kamanda huyo alimtaja aliyejijeruhi baada ya kujichoma kisu maeneo mbalimbali mwilini mwake kuwa ni Selemani Jeremia (33) ambaye ni mkazi wa Magu. Alisema kuwa siku ya tukio Selemani alisafiri kutoka Magu mkoani Mwanza hadi Bunda ambapo alifika nyumbani kwa Daudi na kumkuta akiwa na Monica. Baada ya kufika nyumbani hapo Selemani alianza kumchoma visu Dauidi katika sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwamo kifuani upande wa kushoto na kusababisha ki

MKUU WA WILAYA YA MBULU AAGIZA KITUO CHA POLISI KUJENGWA HARAKA.

Image
Mkuu Wa wilaya ya mbulu  chelestino s mofuga leo 09/10/2017 amekutana na wajumbe wa WDC  wa kata ya Eshkesh , kujadili maendeleo ya kituo cha polisi cha yaeda chini ambacho kinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba 2017.  Mkuu huyo amemuagiza mkuu wa kituo cha polisi kuwachukua maelezo na  kuahidi kusimamia kikamilifu  michango ya wananchi ili kujenga kituo hicho.  Mkuu wa wilaya aliunda tume kuchunguza matukio ya ujangili wa nyara za serikali, wizi wa mifugo na mauaji ya binadamu mnamo mwezi wa nne 2017, na moja ya mapendekezo ya uthibiti wa matukio ya uhalifu ni kujenga kituo cha polisi. Wajumbe hao wamebainika kusuasua kusimamia michango licha ya wananchi kuunga mkono ujenzi huo. Mkuu wa wilaya ametoa siku 30 kukamilisha michango ya ujenI wa kituo cha polisi.

Waziri wa afya afariki baada ya kukimbia

Image
Slim Chaker aliteuliwa waziri wa afya mwezi uliopita Waziri wa afya nchini Tunisia amefariki kutokana na mshutuko wa moyo baada ya kushiriki katika mbio za kuchangisha fedha za kusaidia kupambana na ugonjwa wa saratani. Slim Chaker, 56, aliugua baada ya kukimbia mita 500, kufariki kwenye hospitali ya kijeshi, kwa mujibu wa wizara ya afya. Waziri mkuu Youssef Chahed alisema kuwa amempoteza ndugu ambaye alikuwa akitoa huduma ya kibinadamu. Wanawake waislamu nchini Tunisia waruhusiwa kuolewa na wanaume wasio waislamu Mbio hizo ziliandaliwa kwenye mji wa pwani wa Nabeul siku ya Jumapili kuchangisha fedha za kujenga zahanati ya watoto ya kutibu ugonjwa wa saratani. Bwana Chaker aliteuliwa kuwa waziri wa afya mwezi uliopita wakati wa mabadiliko makubwa ya baraza la mawaziri.

Hallelujah ya Diamond yaweka rekodi Kimataifa Yatikisa Uingereza

Image
                Diamond Platnumz haishi kutuamsha na habari kubwa zinazohusiana na nyimbo zake kila kukicha. Baada ya kuachia wimbo wake mpya ‘Hallelujah’ ambao amewashirikisha Morgan Heritage kuweka rekodi kubwa ya kufikisha views milioni moja ndani ya masaa 15, wimbo huo umeonekana kufanya vizuri katika kituo cha BBC Radio 1Xtra ya nchini Uingereza. Hallelujah’ umeshika namba moja katika Top 5 ya kipindi cha Afro Boss cha radio hiyo kwa kuzishinda ngoma nyingine kama ‘Inde’ ya Heavy K, ‘Maradona’ ya Niniola, ‘My Baby’ ya Magnom na ‘Nhema’ ya EXQ . Wimbo huo unaendelea kufanya vizuri nchini humo ikiwemo na kwenye kituo kingine cha Capital Xtra.

BREAKING NEWS: AJALI MBAYA ,GARI YA ABIRIA AINA YA HIECE LATUMBUKIA ZIWANI

Image
              Gari ndogo la abiria (hiace) likiwa na abiria limetumbukia ziwani wakati likijaribu kuingia kwenye kivuko cha Kigongo Ferry jijini Mwanza, watu watatu tu mpaka sasa wameokolewa Chanzo: Radio Free Afrika

SHAMSA FORD AZIDI KUMSHUKIA ILALA MJINGA,AMPA MAKAVU LIVE

Image
          UKITAKA kujua kichaa cha ‘Queen’ wa Bongo Muvi, Shamsa Ford, basi jaribu kuichokonoa ndoa yake, na hicho ndicho anachokifanya mtu mmoja aliyemfahamu kwa jina la Ilala Mjinga, ambaye kazi yake ni moja tu, kusambaza taarifa za uongo mitandaoni kuhusiana na ndoa yake na mumewe, Chid Mapenzi. Kwa mujibu wa Shamsa ambaye siku chache nyuma alisema kuwa anamuona jini-mkatakamba anainyapianyapia ndoa yake, hatimaye mambo yakamfika shingoni na kuamua kushusha waraka kwenye ukurasa wake wa Instagram, akiwataka wale wote ambao wanadhani atakuja kuachana na mumewe, basi wajue kwamba hiyo ni ndoto sawa na kusubiri embe dodo kwenye mti wa korosho! NA ISRI MOHAMED/GPL Post Views: 22

Waziri Mkuchika awachimba biti watumishi

Image
Waziri, George Mkuchika amefunguka na kuweka wazi mipango yake katika kutumikia nafasi yake na kusema yeye ataanza kuhakikisha watumishi wa Umma wanatumia muda wao kufanya kazi na hataki kusikia watumishi wameondoka makazini kwenda kunywa chai. Waziri Mkuchika ambaye leo Oktoba 10, 2017 ameapishwa na Rais Magufuli kuwa Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora amesema kuwa katika kipindi chake atahakikisha wafanyakazi wanalipwa mshahara kulingana na kazi zao kweli, na wanatumia muda wa kazi kufanya kazi za serikali. "Kwanza katika kipindi changu nikiwa Waziri kwa watumishi wa Umma, nataka wananchi wanapofika maofisini wawakute maofisini, mara nyingi wengi wanaripoto ofisini baada ya muda wanaondoka wanasema wanaenda kunywa chai, yaani wananchi wanatoka vijijini wanamsuburi mtumishi aje eti ameenda kunywa chai jambo hili kuanzia leo nitasimamia kuhakikisha watumishi wa umma wanashinda kazini kwao ili kila mtumishi wa Umma alipwe ms

Mawaziri Wapya wa JPM Waanika Mikakati Yao, Sasa ni Mchakamchaka

Image
Mawaziri na Manaibu Waziri wakiapa, Ikulu Dar. MAWAZIRI na manaibu walioapishwa na Rais John Magufuli, wametoa ahadi ya jinsi watakavyotekeleza majukumu yao. Mawaziri na manaibu walioapishwa leo Jumatatu wametoa ahadi muda mfupi baada ya kula kiapo Ikulu jijini Dar es Salaam. Waziri Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika amesema atahakikisha watumishi wanakuwepo ofisini kuwahudumia wananchi. Amesema baadhi ya watumishi wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenda kunywa chai, hivyo atahakikisha wanabaki ofisini kutoa huduma. Kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, Mkuchika amesema, “Nitatoa elimu na nitatumia muda wangu mwingi na ndugu zangu wa Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa). Nitaongea na Waziri wa Elimu somo la rushwa lifundishwe kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.” “Ni wizara yenye changamoto nyingi, ng’ombe wanapigwa mnada, hawana maeneo ya malisho, viwanda vya mifugo na mchango wa maziwa ni tatizo, niko katika tafakari, nin

Diamond Platinumz awagaragaza Davido na Wizkid Afrimma 2017

Image
                Msanii wa muziki Bongo, Diamond ameibuka mshindi baada ya kunyakuwa tuzo ya Afrimma katika kipengele cha Best Artist of The Year. Tuzo hizo ambazo zimetolewa usiku wa kuamkia leo Taxes nchini Marekani, Diamond amewashinda wasanii kadhaa wakubwa wa Afrika kama Davido na Wizkid ambao walikuwa wakiwania tuzo hiyo katika kipengele kimoja kama inayonekana hapa chini;  Artist of The Year Flavour (Nigeria) Diamond Platnumz ( Tanzania) Fally Ipupa- Congo Wizkid (Nigeria) Cassper Nyovest (South Africa) Davido – (Nigeria) Eddy Kenzo – Uganda Tekno – Nigeria Mr Eazi – Nigeria C4 Pedro – Angola