Posts

Showing posts from January 5, 2017

CLINTON KUSHUHUDIA DONALD TRUMP AKIAPISHWA MAREKANI

Image
Hillary Clinton na mumewe Bill wamethibitisha kwamba watahudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mpya wa Marekani Donald Trump mjini Washington DC. George W Bush na mkewe Laura pia wametangaza kwamba wanapanga kuhudhuria sherehe hiyo mnamo tarehe 20 Januari. Wamesema wanataka "kushuhudia kukabidhiwa madaraka kwa rasi mwingine kwa njia ya amani." Tajiri huyo kutoka Manhattan, New York ataapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani katika makao makuu ya serikali Capitol Hill. Bw Trump alimshinda Bi Clinton katika uchaguzi mkuu uliofanyika Novemba mwaka jana na amemkosoa Bw Bush kutokana na vita vya Iraq na mashambulio ya 9/11. Kabla ya tangazo hilo la Jumanne, Jimmy Carter alikuwa ndiye rais wa zamani pekee aliyekuwa amesema angehudhuria sherehe hiyo. Rais mwingine mstaafu George HW Bush, 92, amesema hataweza kuhudhuria kutokana na umri wake. Bi Clinton amekuwa haonekani sana hadharani tangu aliposhindwa na Bw Trump uchaguzini Novemba. Wakati wa kampeni, Bw

Mwanamke wa kwanza kugombea urais Tanzania afariki dunia

Image
Mwanamke wa kwanza kugombea urais nchini Tanzania, Dkt. Anna Senkoro amefariki dunia leo ambapo Hospitali ya Taifa Muhimbili imethibitisha kutokea kwa kifo hicho. Dkt. Senkoro ndiye mwanamke wa kwanza kugombea urais nchini Tanzania ambapo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 alipeperusha bendera ya chama za PPT- Maendeleo. Katika uchaguzi huo mgombea wa CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliibuka mshindi. Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, PPT- Maendeleo kilimtangaza Dkt. Anna Senkoro kuwa mgombea wake lakini alikihama chama hicho na kijiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo alitimkia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) siku chache kabla ya kampeni kuanza. Mbali na masulaa ya kisiasa, Anna Senkoro alikuwa ni Daktari na pia mama wa watoto watatu

ANASWA AKIFUKUA KABURI LA ALBINO

Image
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kufukua kaburi la marehemu ambaye likuwa ni mlemavu wa ngozi (Albino) aliyefariki mwaka 2010 kwa lengo la kuchukua viungo vyake.Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa na Kamanda a Polisi Mkoani Mbeya DCP Dhahiri Kidavashari inasema kuwa mnamo tarehe 03.01.2017 majira ya saa 01:00 usiku katika Kijiji cha Mumba kilichopo Kata ya Ilembo, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JONAS JOHN mkazi wa Chapakazi alikamatwa na askari Polisi akiwa na wenzake wawili wakifukua kaburi la marehemu SISTER OSISARA aliyekuwa mlemavu wa ngozi (ALBINO) Inadaiwa kuwa marehemu alifariki dunia mwaka 2010 kwa ugonjwa wa homa na kuzikwa katika makaburi ya Kijiji cha Mumba. Mtuhumiwa alikutwa na majembe na makoleo ambayo walikuwa wakiyatumia kufukuria kaburi hilo. Baada ya mahojiano mtuhumwa huyo aliwataja washirika wenzake wawili ambao walikimbia baada ya kuwaona askari. Jeshi hilo linaendelea na msako mkali wa kuwatafuta watuhu