Posts

Showing posts from May 14, 2017

FAHAMU UKWELI JUU YA VITA VYA KARANSEBES AMBAVYO ZAIDI YA WANAJESHI 10000 WALIUANA

Image
Unaweza kudhani ni hadithi ya kutunga lakini hii kweli ilitokea! Vita ya Karansebes, ni miongoni mwa matukio yaliyoushangaza sana ulimwengu baada ya wanajeshi wa jeshi moja la Austria, kushambuliana wenyewe kwa wenyewe na kusababisha wanajeshi zaidi ya 10,000 kupoteza maisha. Ilikuwaje? Usiku wa Septemba 17, 1788, wanajeshi zaidi ya 100,000 wa Jeshi la Austria lililokuwa linaundwa na makabila mbalimbali, walikuwa wameweka kambi katika Mji wa Karansebes (Romania ya sasa) wakijiandaa kuvamia Himaya ya Ottoman (Uturuki ya sasa). Ili kurahisisha uvamizi, wanajeshi waligawana katika makundi, wengine wakaenda upande mmoja na wengine upande mwingine. Wakati wakijiandaa kufanya shambulio, kukatokea kutoelewana kati yao, wakaanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kimakosa wakidhani wanawapiga wanajeshi wa Ottoman. CHANZO CHAKE KINASHANGAZA Inaelezwa kuwa kundi moja kati ya yale mawili, lilivuka Mto Timis na kuingia Mji wa Hussar uliokuwa ngome ya wanajeshi washiri

Tamasha la Dar Bodaboda Superstar Lafanyika

Image
Baadhi ya washiriki wakiwa katika michuano ya kuendesha bodaboda. Bodaboda iliyokuwa ikishindaniwa na waendesha Pikipiki. Baadhi ya wananchi wakifuatilia michuano hiyo. Mkurugenzi Mkazi wa International Republican Institute(IRI),Robina Namusisi akizungumza na Global TV Online. Burudani zikiendelea. MAKAMPUNI ya JP Decaux pamoja na International Republican Institute (IRI) zilizokuwa zimeandaa Tamasha la Waendesha Pikipiki leo limefanyika katika Viwanja vya Tanganyika Parkers Jijini Dar es Salaam. Kati ya washiriki wa tamasha hilo la bodaboda mmoja alijinyakulia pikipiki baada ya kuwashinda washiriki wengine kutokana na vigezo vya mashindano hayo kuvikidhi. Akizungumza na mtandao huu, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JP Decaux, Shaban Makugaya alisema kuwa lengo la tamasha hilo lilikuwa ni kuweka uamsho, msisitizo na kuendelea kutoa elimu ya usalama barabarani kwa madereva wa pikipiki na abiria kwa madhumuni la kuzingatia sheria za us

Fainali za U-17 Afrika, kuanza Leo Gabon

Image
FAINALI za 12 za Kombe la Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 zinatarajiwa kuanza leo mjini Franceville, Gabon hadi Mei 28, mwaka huu itakapofikia tamati. Mechi mbili za Kundi A zinatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Franceville kuanzia Saa 10:00 jioni kati ya wenyeji Gabon dhidi ya Guinea na baadaye Saa 1:00 usiku kati ya Cameroon na Ghana. Mechi za Kundi B zitaanza kesho, kwa michezo miwili pia kuchezwa Uwanja wa Port-Gentil, ya kwanza Saa 9:00 Alasiri kati ya mabingwa watetezi, Mali na Tanzania wanaoshiriki kwa mara ya kwanza kabisa michuano hiyo na wa pili utazikutanisha Angola na Niger kuanzian Saa 12:00 jioni. Awali michuano hiyo ilikuwa ifanyike Madagascar kuanzia Aprili 2 hadi 16, mwaka huu lakini Kamati Kuu ya CAF chini ya rais wake wa zamani, Mcameroon Issa Hayatou ikaipokonya uenyeji nchi hiyo Januari mwaka huu kwa madai Kamati ya Ukaguzi iligundua mapungufu makubwa. Ingawa hiyo ilih

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Image
Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyingi

Kauli ya Rais Mstaafu Mkapa Kuhusu Serikali Kubana Uhuru wa Habari

Image
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mzee Benjamin Mkapa amevikosoa vyombo vya habari barani Afrika na haswa kusini mwa Jangwa la Sahari kwa kile alichosema vingi vimejikita katika kuripoti habari za kisiasa na matukio ya nani kafanya nini au kawa nani, badala ya kuripoti habari za uchumi za kuwasaidia wananchi. Mzee Mkapa aliyasema hayo alipokuwa akifanya mahijiano na na Idhaa ya Kiswahili ya Deutsche Welle (DW) ya nchini Ujerumani ambapo alisema kwenye vyombo vya habari vya Afrika kuna upungufu mkubwa wa wa habari za uchumi na maendeleo zilizofanyiwa utafiti wa kina. “Tatizo moja kubwa la vyombo vya habari vya nchi za Afrika hasa hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara ni kwamba habari nyingi zinazopewa kipaumbele ni zile za kisiasa na zinazohusu nani ni nani na kafanya nini.” “Kuna upungufu mkubwa wa habari za kiuchumi na maendeleo zilizofanyiwa utafiti wa kina na zinazochochea maendeleo. Kuna habari kidogo sana za utetezi wa kimaendeleo na kujipanga ili tupige

Fahamu Aina 61 Za Ubanaji Wa Nywele

Image