Posts

Showing posts from April 5, 2017

VIDEO: Halima Mdee alivyotumia neno "fala" "mpumbavu" Bungeni

Image
 T azama Video:

Chadema, CUF vyatinga Mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi EALA

Image
Twaha Taslim aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki pia Mwanasheria wa CUF  VUGUVUGU la Uchaguzi wa wabunge wa Afrika Mashariki wazidi kulitikisa bunge. tayati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema na Chama Cha Wananchi CUF vimepanga kutinga mahakamani kupinga matokeo hayo. Jana Mweyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe alitoa kauli ya kupinga matokea hayo mahakamani kutokana na kudai kuwa uchaguzi huo ulikwenda kinyume na taratibu za uchaguzi. Leo akizungumza na Muungwana Blog kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Ahmed Katani, amesema kuwa uchaguzi huo umeendeshwa kinyume cha taratibu na kanuni za uchaguzi huo. Amesema kuwa jana majira ya saa 8 na dakika 37 kabla ya uchaguzi huo alipokea  barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi Dk, Thomas Kashililah. Kwa mujibu wa barua hiyo ya Msimamiza wa uchaguzi ambayo alikiri kuwa kwa wagombea wa CUF kuna matatizo na kwamba hatuweza kushiriki kuchaguzi. Katani amesema aliandik

Mbowe amtuhumu Rais Magufuli, kwa jambo hili.

Image
MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe amtuhumu Rais John Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusika kwa alichodai kuwa ni kukeukwa kwa taratibu za uchaguzi. Mbowe ameongea hayo jana usiku mara baada ya kutoka kwenye ukumbi wa bunge  ambapo amedai kuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Rais Magufuli kuhusika kwenye mchakato wa kuyakataa majin ya wagombea wa Chadema. Mbowe amesema  kuwa, wao hawatakubaliana na hilo kwa sababu Spika wa Bunge amekiuka kanuni za bunge, na uchaguzi wote ulikuwa wa kasoro. Wagombea waliopendekezwa na Chadema  Wenje Na Masha kupigiwa kura za hapana katika  kuwania kuiwakilisha Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki Majina ya wagombea na matokeo KUNDI A: WANAWAKE 1. Ndg. Happiness Elias LUGIKO - KE - CCM - KURA 196 2. Ndg. Fancy Haji NKUHI - KE - CCM - KURA 197 3. Ndg. Happiness Ngoti MGALULA - KE - CCM - KURA 125 4. Ndg. Zainabu Ras

Jinsi Facebook ilivyohusika mkasa wa binti aliyejitosa baharini

Image
KISA cha binti mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa kutokana na miaka yake) kujitupa baharini akiwa katika boti ya Kilimanjaro V akitoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar juzi, kinaanzia kwenye mawasiliano yake na mvulana mmoja, kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, imefahamika. Msichana huyo alikuwa akiwasiliana na mvulana huyo ambaye walifahamiana kupitia Facebook, kwa kutumia simu ya mkononi. Nipashe ilifika Kikwajuni, nyumbani kwa msichana huyo ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu (shule inahifadhiwa) na kuikuta familia yake ikiwa na majonzi, huku wakiwa hawaamini kilichotokea na binti huyo akiwa bado hai. Akizungumza kwa huzuni, mama mdogo wa msichana huyo, Asha Saleh Mandhi, alisema palitokea mzozo baina yake na binti huyo baada ya kumkuta na simu ya mkononi wakati wazazi wake hawajamnunulia. Alisema Jumatano iliyopita majira ya jioni akiwa nyumbani hapo na baada ya kupata taarifa kuwa mtoto wake wa kumlea anamiliki simu, alimwita na

Washindi wa Bunge la Afrika Mashariki

Image
Wabunge watakaoiwakilisha Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki wamepatikana.