Posts

Showing posts from February 9, 2016

Kwani ni lazima uolewe???

Image
HAKIKA sifa na utukufu zimuendee yeye Jalali ambaye ametupa nafasi ya kuweza kukutana tena siku ya leo hii.Moja ya kitu kinachonishangaza kwa wanawake wengi ni kuwa na ndoto zaidi ya kuolewa kuliko kufikia ndoto zao halisi kwa maana ya maono ambayo wamekuwa wakiyawaza kwa muda mrefu. Tabia hii ya wanawake wengi ya kutaka au kukimbilia kuolewa si jambo baya, kama ikitokea ukapata bahati hiyo ya kuolewa lakini kama haitatokea sio ishu sana bali kumbuka kuwa kuna maisha nje ya kuolewa nayo si mengine ni maisha ya kufikia ndoto zako. Kama haujaolewa Ni kweli Mungu alituumba na kutuweka duniani ili tuujaze ulimwengu lakini hata hilo la upande wa pili nalo ni la kushukuru pindi linapokukuta, linauma ila kupunguza maumivu yake ni kulikuba li na kujifunza vitu vingine vingi ili uweze kuendelea na maisha mengine. Hulka ya wanawake kuolewa imekuwa ni sehemu ya wengi wao, utamsikia binti wa miaka 16 amemaliza darasa la saba anataka kuolewa eti kisa amefeli mtihani wa mwisho,

Mafuta ya Wizi ya Diesel Yakamatwa Bandari ya Dar

Image
Jeshi la Polisi kitengo cha majini limekamata tani zipatazo 20 za mafuta ya dizeli yaliyokuwa katika Jahazi lililokuwa kando ya bandari ya Dar es Salaam likijiandaa kwa safari ya kwenda Zanzibar. Mkuu wa Kitengo hicho cha Polisi cha Wanamaji, Bw. Mboje John Kanga amesema watu watano wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo na uchunguzi zaidi unaendelea.

ALIKIBA NA WILDAID WATOA WIMBO KUPINGA UJANGILI WA TEMBO.

Image
 Video ya wimbo huo imerekodiwa jijini Los Angeles Marekani ambapo Alikiba alikuwa mgeni rasmi kweye hafla maalum iliyoandaliwa na shirika la uhifadhi wanyamapori la kimataifa la WildAid. Chini ya kauli mbiu “Ujangili Unatuumiza Sote”, Alikiba amefanya kazi na WildAid kuongeza uelewa wa Watanzania kuhusu tatizo la ujangili wa tembo ambao wamechinjwa kwa maelfu miaka ya hivi karibuni kwa ajili ya meno yao. Hatimaye Alikiba ametoa wimbo wake “Lupela” uliokuwa ukisubiriwa na mashabiki wake Afrika Mashariki kwa wiki kadhaa sasa. Wimbo huo ni sehemu ya kampeni ya “Ujangili Unatuumiza Sote” iliyozinduliwa mwaka jana na WildAid na African Wildlife Foundation mashirikia yanayofanya kazi pamoja barani Afrika na Asia kupunguza mahitaji ya bidhaa zitokanazo na wanyamapori na kuongeza uelewa wa janga la ujangili linaloikabili Afrika. Katika uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Slipway jijini Dar es salaam, wageni mbalimbali na waandishi wa habari walipata

ASILIMIA 10 YA WATANZANIA WANAMILIKI UCHUMI WA NCHI’

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua  Mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji  Wananchi Kiuchumi kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua  Mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji  Wananchi Kiuchumi kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kaipata maelezo kutoka kwa Bi Fatuma Kango kuhusu Msimbomilia  au Barcode baada ya kufungua Mkutano wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es slaam Februari 9, 216. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafisi nchini, Reginald Mengi baada ya kufungua mkutano wa  Wadau wa Uwezeshaji Wananchi  Kiuchumi kwenye

Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda Apata Ajali Mbaya ya Gari

Image
Mtu mmoja amefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa akiwemo mke wa waziri mkuu mstaafu Mizengo Pinda Mama Tunu Pinda baada ya gari walilokuwa wakisafiria kumgonga mwendesha pikipiki wakati akikatisha barabara katika eneo la Mkundi barabara ya Morogoro Dodoma manispaa ya Morogoro. Ajali hiyo imetokea majira ya saa nane mchana katika eneo la Mkundi ikihusisha gari lenye namba za usajili STK 9242 gari la mke wa waziri mstaafu Mizengo Pinda likitokea Dodoma kwenda jijini Dar-es-Salaam  na pikipiki Majeruhi wengine wa ajali hiyo ni dereva wa gari hilo Bw Anjelo Mwisa, mlinzi wa mke wa waziri mkuu mstaafu Gaudensi Tembo na kijana wa familia ya Mama Tunu Pinda Bwana Gilbert Sampa. Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa mkoa wa Morogoro Dr Rita Liamuya amesema hali ya mke wa waziri mkuu mstaafu na majeruhi wengine zinaendelea vizuri na kueleza kuwa  majeruhi hao wanatarajia kuhamishiwa jijini Dar-es-Salaam kwa matibabu zaidi TOA MAONI YAKO

Breaking News.....Watuhumiwa 9 walio tungua HELKOPTA wamekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wakiwa na bunduki 27

Image
Watuhumiwa 9 wamekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wakiwa na bunduki 32 pamoja na meno matatu ya Tembo. .. Watuhumiwa walihusika kumuua Rubani wa Helicopter ya Mwiba. ... Mmoja alikamatwa akafanikisha wengine 8