Posts

Showing posts from September 21, 2017

Mzee Akilimali aliamsha dude Yanga

Image
Katibu wa Baraza la Wazee wa Klabu ya Yanga, Ibrahimu Akilimali amemtaka Makamu Mwenyekiti wa Klabu hiyo Clement Sanga kujiuzulu kwa madai kuwa yeye ndiye chanzo cha matatizo yote yanayotokea ndani ya Klabu hiyo. Mzee Akilimali amesema wamegundua mgomo uliotokea hapo jana kwa wachezaji kutohudhuria mazoezi ni njama iliyopangwa na Sanga wakidai kuwa wachezaji hawajalipwa mishahara yao suala ambalo sio sawa. "Mimi naona tu kwamba Sanga sasa imefikia hapa, ili tufanye vizuri nawasihi Watanzania wote hususani wana Yanga na wapenzi wa Yanga bwana Sanga sasa hivi atamke kujiuzulu, chonde chonde Bwana Sanga iache Yanga watu tuketi pamoja na wewe mwenyewe tuchague viongozi Yanga tusonge mbele" amesema Mzee Akilimali Mzee Akilimali amesema siku moja kabla ya mazoezi alionekana Makamu Mwenyekiti wa Klabu hiyo Sanga akiwa na Nahodha wa Timu hiyo Nadir Haroub 'Canavaro' pamoja na Mshambuliaji wa Kimataifa Thaban Kamusoko ambapo baada ya kutoka hap

Irene Uwoya: Napenda mwanaume mwenye sura ya kiume

Image
MWIGIZAJI maarufu wa kike wa filamu za Bongo anayeitingisha Bongo Movie ambae pia aliwahi kuolewa na mcheza soka kutoka Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Katauti’, mlimbwende Irene Uwoya, amesema kuwa mpenzi wake wa sasa ana ngeu nyingi mwilini mwake kutokana na kuchanwa visu. Uwoya amesema watu kama hao ndiyo anaowataka yeye, kwa sababu inaonyesha uanaume halisi, na si wanaume kuwa laini kama mtoto wa kike. Alipoulizwa juu ya hilo alifunguka: “Sijasema napenda wanaume wenye sura mbaya. Nimesema napenda mwanaume mwenye sura ya kiume, mwanaume uwe na ngeu. Mimi bwana’angu ana ngeu za kuchanwa visu, viwembe na nahisi hata bunduki zimemkosakosa,” alisema Irene Uwoya Mwigizaji huyo kwa sasa hajaweka wazi mahusiano yake tangu alipoachana na aliyekuwa mpenzi wake, msanii wa Bongo Fleva, Msami Baby, na amesema hataweka tena mahusiano yake wazi. NA : SAMSON JEREMIAH/GPL