Posts

Showing posts from September 8, 2016

Hatimaye Mtatiro ‘Amchana’ Prof. Lipumba, Amuita ni Jemedari Aliyekimbia Vita

Image
Dar es Salaam: Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro amesema aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba amekiacha chama kwenye wakati mgumu baada ya kujiuzulu wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Agosti, mwaka jana, Profesa Lipumba alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kukabidhi barua kwa uongozi baada ya kushauriana kwa kipindi kirefu na viongozi na wazee wa chama hicho, akisema nafsi yake inamsuta kwa kuwa walikiuka malengo ya Ukawa. Hata hivyo, hivi karibuni Profesa Lipumba aliandika barua ya kutengua uamuzi wa kujiuzulu na uchaguzi ulipoitishwa ili kujaza nafasi hiyo hakuchukua fomu ya kugombea. Akizungumza katika mahojiano maalumu, Mtatiro amesema Profesa Lipumba amekitelekeza chama kikiwa katikati ya uwanja wa mapambano. Mtatiro aliyeteuliwa hivi karibuni na Baraza Kuu la CUF kuongoza kamati ya uongozi wa chama hicho baada ya kuvunjika kwa mkutano mkuu ulioitishwa kuziba nafasi ya mwenyekiti, amesema walijaribu kila mbin

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 08.09.2016

Image
Posted by  PHARS MSIRIKALE at Thursday, September 08, 2016

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI TAREHE 08/09/2016

Image

Wazee Wahofia Chadema Kuhujumiwa

Image
BARAZA la Wazee la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) limesema lina hofu ya kuhujumiwa chama chao kupitia kwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini kwa kuundiwa njama za kukifuta chama hicho kwenye orodha ya vyama vya siasa. Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Baraza la Wazee Taifa wa Chadema, Roderick Lutembeka, amesema pamoja na juhudi kubwa wanazozifanya kutatua mgogoro wa kisiasa, wamepata taarifa za kuwepo kwa njama hizo zinazopikwa dhidi ya Chadema kupitia baraza la vyama vya siasa. “Ni vyema msajili wa vyama vya siasa akawa wazi kwa Watanzania kwani Baraza la Vyama vya Siasa lililo chini yake limekuwa likiaandaa na kuahirisha vikao vya kukutana na vyama vyote vya siasa pasipo kututaarifu. “Mfano Agosti 29-30, ilikuwa baraza likae lakini likaahirisha hadi Septemba 3-4 napo pia wakaahirisha tena bila sisi kupewa taarifa yoyote,” alisema Lutembeka. Katibu Mkuu Baraza la Wazee la Chadema, Roderick Lutembeka akizu