Posts

Showing posts from October 5, 2017

Wolper Anapozomeana na Kivuli Chake

Image
Jacqueline Wolper Massawe, aliye pia na a.k.a nyingi zikiwemo za Gambe na Amber Rose wa Bongo. MIONGONI mwa waigizaji wa kike niliowahi kufanya naye kazi kwa kipindi kirefu na kwa ukaribu zaidi ni pamoja na mrembo Jacqueline  Wolper Massawe, aliye pia na a.k.a nyingi zikiwemo za Gambe na Amber Rose wa Bongo. Mkononi nimefumbata miaka saba sawa tangu nianze kazi ya uandishi wa habari, kwenye magazeti haya pendwa. Ninao uzoefu mkubwa kwa kuwafahamu watu wengi maarufu kwa maana ya maisha yao ndani na nje ya kazi zao, nawajua sana hususan wasanii wa filamu ambao nafanya nao kazi mara kwa mara. Hata wengi wao wananijua vyema , kwenye eneo la kazi kwamba huwa siruki sentensi kwenye kuanika ukweli. Hivi karibuni, Wolper alikaririwa na mmoja wa waandishi wenzangu akisema kitendo cha kumshika na kumbeba mtoto wa mwigizaji mwenzake, Faiza Ally kimemuondolea gundu ya kutopata mtoto hivyo na yeye kutarajia kupata wa kwake mwakani. Sawa, Wolper yuko sahihi lakini mbona m

FAIZA ALLY AJITOSA SAKATA LA DIAMOND PLATINUMZ NA ZARI THE BOSS LADY,AFUNGUKA LIVE

Image
Huku Tetesi na Stori kibao zikikamata headlines mitandaoni kuwa couple ya @diamondplatnumz Na mama watoto wake @zarithebosslady SASA IMEBAKI STORI, Faiza Ameandika ujumbe Huu :. By @faizaally_ – Diamond kijana mdogo sana anahitaji ku have funny na watoto wenzie na sisi wa dada watu wazima tuangalie watu wa kutoka nao… Go baba and have funny enjoy the world ndio useto down …. jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano , bado hujaiona dunia hata robo, we ni star , hela ipo there is lot to see…nasema with clean heart no hate kwa zari au kwa yoyote , nimezurula sana duniani kabla ya kuzaa na kutulia…jiachie life is today buana

Taarifa Muhimu ya TCU kwa Wanafunzi Waliokosa Vyuo

Image
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia Umma kuwa  awamu ya kwanza ya Udahili wa wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na masomo ya shahada za awali ulimalizika tarehe 30 Agosti 2017. Tume inawaarifu kuwa imekamilisha zoezi la uhakiki wa majina ya waombaji wote walioomba kujiunga na Vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo wa 2017/18. Hata hivyo kutokana na  waombaji wengi  kutochaguliwa  kutokana na sababu mbali mbali, Tume inatangaza kuwa itafungua maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe 4 hadi 10 Octoba 2017 ili kuruhusu makundi yafuatayo kuomba udahili: •  Waombaji watakaokuwa wamekosa nafasi kwenye awamu ya kwanza; •  Waombaji wa kidato cha Sita walioshindwa kuomba katika  awamu ya kwanza; •  Waombaji wenye vigezo vya Stashahada  walioshindwa kupata Namba ya Uhakiki wa Tuzo (AVN); •  Waombaji ambao wamemaliza mitihani ya “Cambridge”  mwaka 2017 na matokeo yao yameshatoka; na •  Waliokuwa wanafunzi wa vyuo vikuu watakao kuwa na uthibitsho toka vyuo vy

PENZI LA ZARI THE BOSS LADY NA DIAMOND PLATINUMZ LAYUMBA VIBAYA

Image
  Ule uhusiano maarufu zaidi Afrika Mashariki wa Diamond Platnumz na Zarina Hassan inaelekea upo katika hatua mbaya ya uhai wake kutokana na yanayoendelea katika mitandao ya kijamii. Katika kipindi cha miezi miwili uhusiano huo umepamba vichwa vya habari kabla na baada ya Diamond kukiri kuzaa na mwanamitindo Hamisa Mobetto. Hata hivyo, baada ya sekeseke hilo kupita ilionekana huenda hali imekuwa shwari hasa baada ya Diamond kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa Zari, Septemba 23 mwaka huu nchini Afrika Kusini. Inavyoonekana moto unafukuta ndani kwa ndani kwani tangu juzi wapendanao hao wamekuwa wakifuta picha zao za pamoja katika akaunti zao za Instagram. Pamoja na kufuta picha, Zari anaonekana kurusha vijembe katika mtandao wa Snapchat akisema hawezi kufanywa mjinga katika mitandao ya kijamii. Katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa Diamond, mashabiki walisubiri kwa hamu kuona atakachoandika Zari kama ilivyo kawaida yake lakini ilipita kimya. Wengi wametafsiri kuwa pamoja na

IGP Sirro Kuhusu Miili Iliyookotwa Coco Beach

Image
IGP Simon Sirro. MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amesema wameunda timu ya wataalamu kuchunguza miili iliyookotwa na sampuli kutoka miili hiyo zimechukuliwa. Amesema iwapo kuna watu ambao ndugu zao wamepotea ni vyema wakafika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa ajili ya vipimo na kufanyika upelelezi. “Bahari ni kubwa inapita katika nchi nyingi na inachukua kila kitu, haya mambo yanapotokea hata nchi nyingine yanatokea, kwa hiyo kimsingi tumeunda timu ya wataalamu ya kupeleleza kuhusu miili hii, wamechukua majimaji kutoka mwilini,” alisema. IGP Sirro alisema, “Kama kuna mtu ambaye ndugu yake amepotea afike makao makuu ya Polisi upande wa DCI tuweze kufanya uchunguzi kuona kama ni ndugu yake.” Alisema miili hiyo haijabainika kuwa ni ya watu wa Taifa gani. “Tatizo letu Watanzania ni kwamba moja kwa moja wanaanza kuhisi, sijui kwa nini tunakuwa tunaishi kwa hisia na hii hisia hisia si nzuri, tuseme kitu tukiwa na uhakik

ACT- WAMJIBU RAIS MAGUFULI ISHU YA KUTOONGEZA MISHAHARA

Image
Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu, akizungumza na  waandishi wa habari. CHAMA cha Act-Wazalendo kimesikitishwa  na kauli ya Rais Magufuli aliyoitoa jana kwenye ufunguzi wa mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) kuhusu mishahara ya wafanyakazi aliposema  alipoingia madarakani hakusema ataongeza mishahara kwa vile hakuchaguliwa kuongeza mishahara na kwamba ana jukumu la kuwahudumia wananchi. Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi ACT Wazalendo,  Ado Shaibu, alisema: “Swali la kujiuliza baada ya kauli hiyo ni, je, wafanyakazi wa Tanzania wanastahili kufanyiwa hivi na serikali wanayoihudumia? Jibu bila shaka ni hapana.  Serikali inatoa wapi ujeuri wa namna hii dhidi ya wafanyakazi nchini wakati kiuzalishaji na kimapato inawategemea wafanyakazi? “Licha ya mchango wao madhubuti katika ujenzi wa taifa kwenye sekta mbalimbali, kwa utumishi wao wa kutukuka, ukweli wa mambo ni kuwa wafan