Posts

Showing posts from April 14, 2017
Image
7 Tips to Make a Guy Fall in Love With You Love is a complicated thing. The chemistry of attraction is hard to pin down but it doesn’t stop people from falling in love. With every passing minute people meet, get married, start families, and create life-long partnerships. The force behind it all is simple: who would want to give up on love? We won’t have this beautiful world as it is if it wasn’t for love. People spend years waiting and searching for something true and pure. Sometimes it happens faster than expected – sometimes everything feels hopeless. No matter what you do: never give up on yourself and on finding love. We are here to help! 1.Be confident.....

Waliovunjiwa Nyumba Mkwajuni na Mkunguni Dar Kulipwa

Image
BUNGE limeelezwa kuwa wananchi waliovunjiwa nyumba katika eneo la Mkwajuni wilayani Kinondoni ambao wana hati watalipwa fidia. Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia (CUF) aliyetaka kujua hatima ya watu waliovunjiwa nyumba katika eneo hilo. Naibu Waziri alisema, ni kweli watu walivunjiwa nyumba katika eneo la Mkwajuni na Mkunguni, hivyo wapeleke hati zao wizarani walipwe fidia. Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Salma Mwassa (CUF) aliyetaka kujua kuna umuhimu gani kusarisimisha nyumba alisema, kunapunguza migogoro ya ardhi. Mabula alisema urasimishaji wa ardhi maana yake ni kutambua miliki ya wananchi kwenye maeneo yaliyoendelezwa bila kupimwa kisheria. Matokeo ya urasimishaji ni kutoa hati miliki na kuweka miundombinu ya msingi kama vile barabara, maji, mifereji ya maji ya mvua na ikiwezekana majina ya mitaa. “Urasimashaji ni mpango

skari Polisi 8 Wauawa na Majambazi.....Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi

Image
Ra i s wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Askari Polisi 8 waliouawa kwa kushambuliwa na watu wenye silaha jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani. Askari Polisi hao walikuwa wakitoka kubadilishana doria na wameshambuliwa kwa kupigwa risasi wakiwa wanasafiri kwa gari katika barabara ya Dar es Salaam – Lindi. Mhe. Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP-Ernest Mangu, familia za askari wote waliouawa, Askari Polisi wote na Watanzania wote walioguswa na vifo hivyo. “Nimeshtushwa na nimesikitishwa sana na vifo vya askari wetu 8 ambao  wamepoteza maisha wakiwa wanalitumikia Taifa, naungana na familia za marehemu wote, Jeshi la Polisi na Watanzania wote katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na majonzi ya kuondokewa na vijana wetu shupavu. “Namuomba Mwenyezi Mungu atupe moyo wa subira, uvumilivu na ustahimil

OFISI YA MDHIBITI NA MKAGUZI WA MAHESABU YA SERIKALI YAWASILISHA RIPOTI YAKE KWA MWAKA WA FEDHA UNAOISHIA 2015/2016.

Image
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Prof Musa Assad akizungumza na waandishi wa Habari(hawapo Pichani) kuhusu Ripoti ya Ofisi yake kwa mwaka wa Fedha unaoisha 2015/2016 Leo Aprili 13,2017 Mjini Dodoma. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Prof Musa Assad na Mwenyeketi Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.Naghenjwa Kaboyoka wakiangalia moja ya kitabu cha Ripoti kutoka Ofisi yake wakati alipokutana na na waandishi wa Habari(hawapo Pichani) kuhusu Ripoti ya Ofisi yake kwa mwaka wa Fedha unaoisha 2015/2016 Leo Aprili 13,2017 Mjini Dodoma. Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO Dodoma.