Posts

Showing posts from November 11, 2016

Rais JPM Awaongoza Mamia Kuagwa Mwili wa Samuel Sitta Karimjee Dar

Image
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli akiongoza waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Spika wa Bunge Mstaafu, Samuel John Sitta. …Akiwapa mkono wa pole wafiwa wa marehemu Sitta baada ya kutoa heshima za mwisho mbele ya jeneza. Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete akipita mbele ya jeneza kutoa heshima zake za mwisho. Makamu wa Rais Mstaafu, Dk. Gharib Bilal akipita mbele ya jeneza kuuaga mwili wa aliyekuwa Spika wa Bunge Mstaafu, Samwel Sitta. Viongozi mbalimbali wakiwa msibani hapo. Mbunge wa Muleba Kusini, Prof. Anna Tibaijuka (katikati) akiwa na waombolezaji wengine katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. …Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi naye akipita mbele kuuaga mwili wa marehemu Sitta. Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye akipita mbele ya jeneza kuuaga mwili wa marehemu. Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba naye akipita mbele ya jeneza kutoa heshima za mwisho.

Obama: ‘Ninamuunga Mkono’ Donald Trump, Nitashirikiana Naye

Image
MAREKANI: Rais mteule wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa ni ”heshima” kubwa kukutana na rais Barrack Obama katika mazungumzo ya mpito yaliofanyika katika ikulu ya White House. Rais Obama amesema kuwa ametiwa moyo kuhusu mazungumzo yao ya maswala mbalimbali yaliochukua zaidi ya saa moja. Trump ametilia shaka uraia wa rais Obama na kuapa kuharibu ufanisi wake wakati wa utawala wake. Bw Trump kwenye kampeni alimweleza Bw Obama kama rais mbaya zaidi kuwahi kuongoza Marekani. Wakati wa kampeni bwana Obama alisema kuwa bwana Trump ‘hafai’ kuongoza Marekani. Pia alisema Mwanarepublican huyo hana sifa na uwezo wa kuwa kiongozi wa Marekani. Mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York, ambaye sasa ni rais mteule, kwa muda mrefu alitilia shaka uhalali wa habari kwamba Obama alizaliwa Hawaii, na alikejeliwa hadharani na Rais Obama. Wawili hao walishauriana kwa zaidi ya saa moja afisi ya rais katika ikulu ya White House mnamo Alhamisi na walipojitokeza kwa wanahaba

Tanzia: Mbunge Hafidh Ali Tahir Afariki Dunia

Image
DODOMA: Mbunge wa Jimbo la Dimani lililopo visiwani Zanzibar, Mhe. Hafidh Ali Tahir (CCM) amefariki dunia saa 9 alfajiri ya leo katika Hospitali ya General iliyopo mkoani Dodoma alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu alizaliwa Oktoba 30, 1953 na aliwahi kuwa Mkuu wa Sauti ya Tanzania Zanzibar (1970-1978) na amekuwa mbunge tangu 2005 hadi mauti yanamkuta. Marehemu pia alikuwa mwanamichezo, mwamuzi wa FIFA na mpenzi wa Klabu ya Yanga kindakindaki na ni jana tu alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Tawi la wabunge Wana-Yanga mjini Dodoma chini ya Uenyekiti wa Venance Mwamoto. Taarifa zaidi kuhusu msiba huu zitatolewa hapo baadae. Mhe. Spika anaungana na Wabunge wote katika kuomboleza msiba huu.