Posts

Showing posts from April 15, 2016

Kajala amtolea chozi kigogo wa Wema!

Image
Kajala Masanja Na Imelda Mtema Siku chache baada ya gazeti dada na hili, Risasi Jumamosi kuandika juu ya aliyekuwa kigogo wa msanii Wema Sepetu, Clement Kiondo ‘CK’ kunaswa akiuza mishikaki, tukio hilo limemliza shosti wa Wema, Kajala Masanja. Kumwaga chozi kwa Kajala kumetokana na maelezo yake kwamba, baada ya kuiona habari hiyo hakuweza kuamini kama kweli ni CK yule aliyewahi kumtolea shilingi milioni 13 kama faini ili asiende jela kutokana msala aliokuwa nao. Wema Sepetu Akizunbumza na Ijumaa kwa majonzi, Kajala alisema: “Kiukweli nililia sana, nilishindwa kuamini kama kweli CK amefikia hali hiyo,” alisema Kajala ambaye pia aliwahi kudaiwa kutoka kimapenzi na jamaa huyo. Akasema stori hiyo isingekuwa imeambatana na picha asingeamini lakini alipoona zile picha zinazomuonesha CK akiwa jikoni akimhudumia mtu, alishindwa kujizuia na kujikuta akibubujikwa na machozi. Tukio la kunaswa kwa CK akiuza mishikaki lilinaswa na mapaparazi wetu juzikati kwenye baa m

TTCL Yajivunia Modemu Mpya za Intaneti ya 4G

Image
Afisa Mauzo Mkuu wa TTCL Shop Mwananyamala, Dar, Bi. Leyla Pongwe (katikati) akielezea namna ambavyo huduma ya 4G  LTE na router mpya ya TTCL inavyofanya kazi, kushoto ni Afisa Masoko, Bi. Mboka Kategela kutoka Kituo cha Huduma kwa Wateja cha Mwananyamala na kulia ni Afisa Mauzo, Bw. Chacha Ghati Mosenye walipofanya mahojiano na Global TV Online leo. Afisa Masoko Kutoka TTCL Extelecom, Samora Avenue -Dar, Bw. Joel J. Goyayi akielezea namna ambavyo modem zao zinavyofanya kazi. Wakisikiliza swali kutoka kwa mwandishi wa habari wa Global Publishers, Andrew Carlos (hayupo pichani) kuhusu uboreshwaji wa vifurushi vya intaneti vya TTCL. Bi. Mboka Kategela (kushoto) akishika modemu ya Mi-Fi wakati Bi. Leyla Pongwe akishika vocha ya TTCL ya Tsh. 5000/=. Wakitambulisha bidhaa hizo kwa wanahabri wa Global Publishers. Wakiwa kwenye picha ya pamoja. Wakisikiliza swali kutoka kwa mmoja wa wanahabari. Maofisa Masoko kutoka TTCl wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafan

HAWA NDIO MASTAA WA BONGO WALIOSHINDWA KUTIMIZA AHADI ZAO

Image
Mastaa wengi wa Bongo wamekuwa wakiahidi vitu vingi kwa mashabiki wao lakini vitu hivyo vinakuwa vinapotea hewani bila ya kutekelezeka. ‘Ahadi ni deni’, watu wengi wanakuwa wanasahau maneno ambayo mwanzo waliyasema wenyewe na bila hata ya kurudisha tena mrejesho kwa mashabiki wao juu ya kauli zao za mwanzo walizozisema. Baadhi ya mastaa wameshaanza kupoteza uaminifu kwa mashabiki wao kutokana na kuahidi kuja na vitu vingi lakini muda umezidi kwenda na mambo yanazidi kubadilika huku kauli zao zikiwa hazitekelezwi. Hawa ni baadhi ya mastaa walioshindwa kutekeleza ahadi zao kwa mashabiki wao. Wema Sepetu Ni mwaka mmoja takribani Madam atoe ahadi ya kuachia movie aliyofanya na staa wa movie kutoka Ghana, Van Vicker. Ni kweli kuna kipindi Sepetunga hakuwepo nchini kwa muda kidogo na alidai kuwa anaenda kushoot movie yake na staa huyo wa Ghana. Aliwahi kusema alifanya connection na Van Vicker kupitia Instagram. Movie hiyo hadi leo haijatoka. Naamini

Rais Salva Kiir Mayardit wa Sudani Kusini Awasili Tanzania

Image
Rais wa Sudani Kusini, Mhe. Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye kofia nyeusi) akishuka katika ndege ya Shirika la Kenya mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam. Rais wa Sudani Kusini, Mhe. Jenerali, Salva Kiir Mayardit akiongozana na rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Rais wa Sudani Kusini, Mhe. Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam. Rais wa Sudani Kusini, Mhe. Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Richard Sezi

Kilango atoa ya moyoni

Image
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela. ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela, ameibukia kanisani na kutoa ya moyoni, ikiwa siku tano baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wake. Kilango, ambaye Jumatatu wiki hii uteuzi wake ulitenguliwa baada ya Machi 20, mwaka huu, kudai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna mtumishi hewa wa serikali hata mmoja. Hata hivyo, Ikulu ilifanya uchunguzi na kubaini kuwa katika taarifa za awali kuna watumishi hewa 45, huku kazi ya uhakiki ikiendelea katika wilaya za Ushetu na Shinyanga. Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wote, alipokuwa akiwaapisha kuwa wafanya uchunguzi kuhusu uwapo wa watumishi hewa katika mikoa yao na kutoa taarifa. Kutokana na kutoa taarifa hizo zisizo za kweli, Jumatatu wiki hii, Rais Magufuli alitangaza kutengua uteuzi wake, akiwa amekaa kwenye nafasi hiyo kwa siku 27. Kilango amekuwa mkuu wa mkoa wa 19 tangu kuanzishwa kwa mkoa huo. Mbali na Kilango, Rais M

TAZAMA PICHA ZA HARUSI YA MR.BLUE ILIYOFUNGWA JANA

Image
Hatimaye Mr blue kaachana na ukapera kaamua kumuoa mama watoto wake Wyder!!! Hongera sana Mr Blue kwa hatua uliyofikia!!! Mr blue simbaaa akiwa na mke wake halali kabisaaa Wyder !!! Hakika Blue nayeye ameingia katika list ya wasanii mifano ya kuigwa katika maswala ya ndoa.. tupia neno la kumtakia kheri katika maisha ya ndoa...!!!bado baba Tiffah 

MWAKILISHI MPYA WA UNHCR NCHINI AJITAMBULISHA KWA WAZIRI KITWANGA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati), akimkaribisha ofisini kwake Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati alipokuwa anawasili ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha kwa Waziri huyo mara baada ya kuteuliwa na Shirika lake kuja kuiongoza UNHCR nchini. Hata hivyo, viongozi hao katika mazungumzo yao walijadiliana masuala mbalimbali jinsi wa kuwahudumia wakimbizi waliopo nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia), akimfafanulia jambo Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati Mwakilishi huyo alipomtembelea Waziri Kitwanga ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha baada ya kuteuliwa na UNHCR kuja kuwa kiongozi wa Shirika hilo nchini. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akimfafanulia jambo Mwakilishi