Posts

Showing posts from May 15, 2017

ADAM MALIMA ATISHIWA BUNDUKI NA POLISI

Image
TAHARUKI imeibuka mchana huu maeneo ya  Masaki karibu na Double Tree Hotel baada ya askari polisi mmoja kufyatua risasi hewani kutokana na kile kilichoonekana kuwepo kwa mzozo kati ya polisi na mbunge wa zamani wa Mkuranga, Pwani, Adam Kighoma Ali Malim. Taarifa zimeeleza kuwa chanzo cha tukio hilo yalikuwa ni majibizano kati ya Majembe Auction Mart waliokuwa wameambatana na polisi walipojaribu kukamata gari lililokuwa limeegeshwa barabarani. Inasemekana gari lilikuwa la mwanaye Kighoma Malima aliyekuwa eneo hilo kwa shughuli zake binafsi ambapo ofisa wa Majembe alivamia gari hilo na alipodaiwa kuonyesha vitambulisho aligoma kutoa ndipo wananchi walipolizingira gari wakitaka kumpiga wakizania ni jambazi. Polisi aliingilia kati na katika majibizano ya maneno na Malima, ndipo askari mmoja akafyatua risasi kadhaa hewani hali iliyozua taharuki kubwa eneo hilo. Mtandao wa Global Publishers umefanya jitihada za kumtafuta Malima kwa njia ya simu lakini simu zake

Mwigulu Nchemba: Bado Hatuna Sheria ya Kuthibiti Shisha

Image
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba bungeni leo amesema serikali bado haina sheria ya kuthibiti matumizi ya kilevi aina ya shisha ila lipo agizo la Waziri Mkuu la kupiga marufuku biashara hiyo na kutaka agizo hilo lifuatwe na kila mtu. Mwigulu Nchemba amesema hayo wakati akijibu swali bungeni kuhusu matumizi ya kilevi hicho cha shisha ambacho bado katika baadhi ya maeneo kimeendelea kutumika na kuleta athari kwa watumiaji. “Ni kweli serikali baada ya kuona matumizi ya kilevi cha Shisha yanaleta athari kwa binadamu, serikali imeanza kuweka sheria za kuthibiti matumizi ya shisha, usambazaji wa shisha na uagizaji wa kilevi hicho, lakini wakati tunasubiri sheria hizo tunatambua kuwa lipo agizo la Waziri Mkuu la kupiga marufuku matumizi ya kilevi cha shisha ambalo utekelezaji wake ulianza mikoani kama Dar es Salaam, Mbeya, Iringa na mikoa mingine imeendelea kuitikia. Kwa hiyo maelekezo ya Mh. Waziri Mkuu yanafanyiwa kazi bila kupunguza hata

Mwanafunzi Kukishitaki Chuo Kikuu cha UDSM

Image
Mwanafunzi aliyefukuzwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Alphonce Lusako, amewasilisha maombi Mahakama Kuu chini ya hati ya dharura, aruhusiwe kukishtaki chuo hicho kwa kumkatisha masomo. Mwanafunzi huyo aliyekuwa akisoma shahada ya kwanza ya sheria alifukuzwa baada ya kufutiwa usajili Januari 26, pamoja na mambo mengine akidaiwa kusajiliwa kwa makosa kwasababu aliwahi kufukuzwa chuoni hapo. Lusako anayewakilishwa na Wakili Jebra Kambole anaiomba Mahakama impe kibali cha kuishtaki UDSM na itoe amri ya kuzuia uamuzi wa kumfutia usajili. Maombi hayo yamepangwa kusikilizwa Mei 23 na Jaji Pellagia Khaday. Lusako alijiunga na UDSM kwa mara ya kwanza mwaka 2009 akiwa amedahiliwa kusoma Shahada ya Biashara katika Uhasibu. Hii ni mara ya pili kwa Lusako kufukuzwa chuoni hapo, mara ya kwanza ni Desemba 13, 2011, pamoja na wenzake kadhaa, akiwa mwaka wa tatu walifukuzwa na kufutwa katika mfumo wa elimu nchini wakidaiwa kuratibu mgomo wa wanafunzi UDSM. Hata hivyo

RAIS DKT. MAGUFULI AIFUTA MAMLAKA YA USTAWISHAJI MAKAO MAKUU CDA, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini Amri ya Rais (Presidential Order) kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA, tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasilikiza viongozi mbalimbali waliokuwa wakichangia mara baada ya kusaini Amri ya Rais (Presidential Order) kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA,tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kusaini Amri ya Rais (Presidential Order) kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA, tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. m. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Ardhi William Lukuvi, Waziri wa Katiba na Sh

MBUNGE LEMA ADAI UPINZANI TANZANIA NI KAZI SANA

Image
  Mbunge Godbless Lema amedai kuwa mpinzani wa siasa za bongo ni kazi ngumu sana, Mh Lema amesema hayo baada ya baaadhi ya watu kumdhihaki alipotoa shukrani zake kwa Mbunge Lazaro Nyalandu kufuatia kuwasaidia majeruhi wa ajali ya basi la Lucky Vicent. Jana baada ya Mbunge Godbless Lema kumshukuru Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM) Lazaro Nyalandu kuna kundi la watu liliibuka na kuanza kutoa maneno ya dhihaka kwa Lema huku wengine wakipongeza na kusema ni jambo la kheri kwa mbunge huyo kutambua kazi iliyofanywa na Nyalandu, lakini baada ya mijadala hiyo kuzidi kuwa mikuba aliibuka Mh. Lema na kutoa kauli hii kumjibu mtu mmoja ambaye alikuwa akimdhihaki.  "Kuwa mpinzani wa siasa Tanzania ni kazi ngumu sana, ila hatukati tamaa kwa sababu upendo wetu ni mkuu kuliko dhihaka. Mungu akubariki"   aliandika Godbless Lema 

CCM yawasimamisha viongozi wengine Arusha

Image
Monday, May 15, 2017 Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Arusha  kimewasimamisha viongozi wa kata mbili kutokana na tuhuma mbalimbali ikiwepo kushindwa kuratibu vyema chaguzi ndani ya chama hicho. Wiki iliyopita Katibu  wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole aliwasimamisha viongozi zaidi ya 30 wa kata tano, baada ya kubainika wameshindwa kusimamia majukumu yao. Chama hicho kimeendelea na hatua hiyo, ambapo leo (Jumatatu) viongozi wa kata ya Ngarenaro na Kaloleli wamesimamishwa ikiwa ni sehemu ya mkakati wa chama hicho, kujiimarisha katika jiji la Arusha, baada ya kupoteza mvuto ambao ulisababisha kushindwa katika uchaguzi uliopita. Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, wilaya ya Arusha ,Gasper Kishimbua amesema  CCM imechukuwa uamuzi huo, ili kuendelea kujiimarisha chama hicho. Kishimbua amewataja waliosimamishwa kuwa ni Mwenyekiti wa Kata ya Kaloleni, Amin Ngawala na Katibu wake, Regina Kessy. Katika Kata ya Ngarenaro, waliosimamishwa ni Mwenyekiti, Ally Mw

BREAKING: “Hans Pope amefuta uamuzi wa kujiuzulu uongozi Simba” – Haji Manara

Image
Baada ya kuripotiwa taarifa za kujiuzulu kwa Hans Pope Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, leo Jumatatu May 15, 2017 ripoti mpya kutoka kwa Afisa Habari wa club hiyo Haji Manara kutoka kwenye Instagram yake ameandika kuwa kiongozi huyo amefuta uamuzi wake. Kupitia Instagram Haji Manara ameandika >>>  Rasmi Hanspope arejea kundini, afuta uamuzi wake wa kujiuzulu, na ndio maana fans wetu nawaomba mtulie, hakuna kitakachoharibika, ni upepo mbaya ulipita na sasa umetulia, Karibu tena kamanda Pope<<< – Manara

Gigy Amchefua Wema Ukumbini

Image
Stori: Waandishi Wetu | IJUMAA WIKIENDA | D AR ES SALAAM Muuza nyago kwenye video za nyimbo za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ anadaiwa kumtia hasira na kumchefua staa wa sinema za za Kibongo, Wema Isaac Sepetu baada ya kukutana ukumbini kwenye bethidei ya meneja wa wasanii wa muziki. Ubuyu wa motomoto ulidai kuwa, baada ya kukutana, Gigy alidaiwa kucheza muziki kihasarahasara na mmoja wa ‘mazilipendwa’ wa Wema, jambo ambalo mlimbwende huyo hakupendezwa nalo. Ishu hiyo ilichukua nafasi kwenye Ukumbi wa Hyatt Regency The Kilimanjaro Hotel uliopo Posta jijini Dar ambapo mastaa kibao walikuwa wageni waalikwa kwenye shughuli hiyo iliyotawaliwa na mavazi ya kizamani. Wema Sepetu Kwa mujibu wa shushushu wa Wikienda aliyekuwa ndani ya shughuli hiyo, awali Wema alionekana mwenye bashasha tele akiwa na wapambe wake, lakini Gigy alipoanza makeke yake ndipo bibie huyo akapoa kama maji ya mtungi. “Mwanzoni Wema hakuwa na tatizo kabisa na Gigy, lakini baa

KIMENUKA MSIMBAZI, MO AIDAI SIMBA BILIONI ZAKE.

Image
Siku moja baada ya Simba kutiliana saini mkataba wa udhamini na kampuni ya SportPesa, mdau wa klabu hiyo Mohammed Dewji ‘MO’ anataka kulipwa kiasi cha shilingi bilioni 1.4 za Tanzania kutokana na viongozi wa Simba kukiuka makubaliano Mei 12, 2017, uongozi wa Simba ukiongozwa na Rais wa timu Bw. Evans Aveva, ulisaini mkataba wa miaka mitano na kampuni ya SportPesa wenye thamani ya Sh. 4.9 bilioni. MO anataka kulipwa pesa zote za mishahara alizokuwa akiwalipa wachezaji wa Simba tangu mwaka jana baada ya kubaini kuwa Simba imeingia mkataba na kampuni ya SportPesa bila kumshirikisha. MO kawaandikia Simba ‘demand note’ kwa kua wamekiuka makubaliano yao kwamba, atoe pesa kama makubaliaono ya kuingia kwenye mfumo wa hisa na ikitokea kampuni inataka kuidhamini Simba inabidi wakae meza moja viongozi na MO ili hiyo kampuni itambue mwelekeo wa Simba, lakini viongozi wa klabu hiyo wakasaini kimyakimya. Simba ilishaanza mchakato wa marekebisho ya katiba yao ili kuruhu

BREAKING: KATIBU CCM AUAWA USIKU WA KUAMKIA LEO

Image
Kibiti.   Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Bungu wilayani hapa, Alife Mtulia ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema mauaji hayo yamefanyika usiku wa kuamkia leo (Jumapili)  katika Kijiji cha Nyambunda. Amesema Mtulia aliuawa na watu hao alipokuwa anakwenda kuoga. Kamanda amesema mwili wa marehemu umepelekwa kituo cha afya cha Kibiti kwa uchunguzi. Mauaji ya askari Polisi, viongozi wa Serikali za Mitaa na raia yamekuwa yakifanyika mara kwa mara katika wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani. Jumanne wiki hii akiwasilisha bungeni bajeti ya wizara yake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba aliliambia Bunge kuwa Serikali itaanzisha mkoa mpya wa kipolisi katika wilaya za Kibiti, Rufiji, Mkuranga na Mafia. Utaitwa mkoa wa kipolisi Rufiji. Credit : Muungwana

Wanachuo Wengi kukosa tena mikopo

Image
BUNGE limeishauri serikali kuongeza bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) baada ya kubaini wanafunzi wengi watakosa fedha hizo mwakani kutokana na bajeti ndogo iliyotengwa. Ushauri huo ulitolewa bungeni mjini hapa juzi na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii ilipokuwa ikiwasilisha taarifa yake kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi na makadirio ya wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha. Akiwasilisha taarifa hiyo, mjumbe wa kamati hiyo, Hussein Bashe, alisema wamebaini wanafunzi wengi watakosa mikopo mwaka ujao wa fedha licha ya kuwa na ufaulu mzuri. Alisema mwaka huu wa fedha wanafunzi 48,502 walijaza fomu kwa ukamilifu lakini 25,555 tu ndiyo walipata mikopo na hivyo kuacha wengine 22,947 wakiwa hawana mikopo kutokana na bajeti iliyotengwa ya Sh. bilioni 427.5 kutotosheleza mahitaji. Bashe ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), alisema mwaka ujao wa fedha HESLB

MCHUNGAJI ALIWA NA MAMBA WATATU AKIJARIBU KUTEMBEA JUU YA MAJI KAMA YESU NCHINI ZIMBABWE

Image
Mchungaji wa kijiji kimoja huko zimbabwe Pastor Jonathan Mthethwa ametafunwa vizuri na mamba watatu alipokuwa akijitutumua kutembea juu ya maji Kama yesu katika mto MPUMALANGA au kwa jina maarufu MTO MAMBA kutokana na wingi wa mamba katika mto huo. Alikuwa anafanya majaribio ya imani(DEMO) aliyowafundisha waumini wake kanisani.... Shemasi aliyehojiwa anashangaa kwa nini aliliwa maana kabla alifunga na kuomba wiki nzima... Mashuhuda wanasema alitembea ndani ya maji kama mita 30, alipotaka kuanza kupanda ili aanze kutembea juu ya uso wa maji ndipo yalitokea mamamba makubwa matatu na kumtafuta na kumkatata vipande huku mwili wote ukiishia kwenye matumbo ya watafunaji hao... Waumini Muwe makini na Wachungaji wenu, Leo kaenda yeye kesho anaweza kuibuka mwingine TZ akawaambia kanisa zima litembee juu ya mto ruvu ile sehemu yenye mamba na viboko wengi kama mazoezi ya Imani. Au kama mafunzo ya vitendo baada ya kufundishwa Theory/Nadharia za kiimani kanisani.. Imani