Posts

Showing posts from May 17, 2017

Takukuru wanasa mali za mhasibu wao, Ana magorofa 7, Nyumba 9, Viwanja 37, Magari 5

Image
Miongoni mwa mali zinazomweka mhasibu huyo katika kundi la matajiri katika nchi hii inayotambuliwa kimataifa kama mojawapo ya mataifa maskini, ni pamoja na viwanja 37, maghorofa saba, nyumba za kawaida tisa, magari matano na pikipiki. Maghorofa, nyumba za kawaida na viwanja vya mhasibu huyo ambaye alishafukuzwa kazi tangu mwaka jana viko kwa mtawanyiko katika maeneo mbalimbali nchini yakiwamo ya ghali karibu na bahari, Kigamboni na Mbweni jijini Dar es Salaam na pia Bagamoyo mkoani Pwani. Kwingineko kuliko na mali hizo ni Kinondoni (Dar), Musoma, Nyegezi na Kiseke jijini Mwanza. Hata hivyo, chanzo cha uhakika kimeiambia Nipashe kuwa hivi sasa mali hizo ziko chini ya himaya ya Takukuru, baada ya kuzinasa kufuatia idhini ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyotokana na ombi la taasisi hiyo. Mei 9, mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilitoa amri ya zuio la mali za Gugai ambaye anakabiliwa na tuhuma za kujilimbikizia mali kinyume cha Sheria ya Kuzuia n

Q-Chillah, Ray C, TID, Matonya, Marlaw na Besta Turudisheni Muziki Wetu

Image
Stori: BRIGHTON MASALU | RISASI JUMATANO | RISASI VIBES “ NINACHO-KIPATA, nagawana na wenzangu maskini zaidi yangu, wenye dhiki kama mimi, waliopoteza wazazi wao kwa ugonjwa wa Ukimwi… wale wenzangu na mimi wasiojiweza kitandani, yaani wa leo wa kesho, dua nawaombea… moyo wangu wa mbigili… kila mtu wamchoma….” “Hebu tathmini kisha nipe jibu…,hivi kwa nini hutaki kunijibu, mitihani yote nimeshinda…nadhani ni wakati penzi letu sisi liwe wazi, roho yangu inauma…maumivu sasa basi…Sasa basi, niko thabiti, nielewe pesa siyo mapenzi, kwa utenzi huu nielewe baby, nakuhitaji mpenzi, wewe ndiyo faraja yangu…” TID “Umenikataa bila sababu, umeninyanyasa bila aibu… nimepata mwingine tabibu sasa wanifuatafuata nini? Kama ni pendo langu nilikupa lote, nilikujali kwa kila kitu na kukupa mahaba yote, sikudhani ungenidharau na kuniletea wengine…sikudhani ungenigeuka na kuanza kuninyanyasa, pesa na magari yako yalikufanya uwe kiburi, uliniacha ukaenda zako na kusahau utu

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 17.05.2017

Image
 

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI LEO TAREHE 17/05/2017

Image

Malima aachiwa kwa dhamana ya mil 5

Image
Tuesday, May 16, 2017 Aliyekuwa Naibu Waziri Wizara ya Fedha, Mhe Adam Malima ameachiwa leo kwa dhamana ya shilingi milion 5 katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la shambulio. Malima ambaye aliwahi kuwa mbunge wa Mkuranga amedaiwa kumzuia Ofisa huyo kufanya kazi yake ya kumkamata Ramadhani Kigwande kwa kosa la kumshambulia Mwita Joseph. Wakati akisoma mashtaka yaliyokuwa yakimkabili Mhe Malima, Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono alidai kuwa Mei 15,2017 katika eneo la Masaki kwa makusudi Malima alimzuia Ofisa wa polisi H.7818 PC ABDU kufanya kazi yake halali. Wakili Kombakono aliendelea kudai kuwa mshtakiwa huyo akiwa na nia ya kumzuia Mwita Joseph ambaye ni Ofisa oparesheni wa kampuni ya Priscane Business Enterprises  wakati alipokuwa akimkamata kwa kupaki vibaya gari namba T 587 DDL alimshambulia(Mwita) na kumsababishia maumivu. Kwa upande wa mshtakiwa wa kwanza, Ramadhani Mohammed Kigwande (Dereva wa Malima) naye anakabili

Mwanaye Madega Aua, Naye Auawa Ajalini

Image
Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa TFF, Iman Omary Madega. MWANDISHI WETU | CHAMPIONI |HABARI MWENYEKITI wa zamani wa Yanga, Imani Madega amepata msiba mkubwa baada ya mwanaye, Omary Madega kupata ajali iliyosababisha kifo na baadaye kuuawa kwenye ajali nyingine. Omary anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 32, aliuawa wakati akiwakimbia madereva wa bodaboda katika eneo la Chalinze mkoani Pwani akiwa anatumia gari la baba yake mdogo, Madega ambaye kitaalamu ni mwanasheria. Akizungumza na Championi Jumatano , Madega aliyeonyesha masikitiko makubwa alisema gari lililosababisha ajali ni Mitsubishi Pajero, mali yake. “Nina msiba mkubwa sana ndugu yangu. Nilisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Chalinze ambako nilipitiliza kwenye project yangu. Nikiwa huko gari lilisumbua.  “Nikamuita Omary ambaye ni mtoto wa kaka yangu aje alishughulikie. Alipofika pale alikuwa na fundi, akamchukua na mtu ambaye amekuwa akisimamia nyumba yangu ninapokuwa Dar es Salaam pamoja na msimamizi wa

Faida Za Pilipili Kichaa Kiafya Na Kitiba

Image
Tuesday, May 16, 2017 Afya Pilipili kichaa inaweza kustawi sehemu mbalimbali na inahitaji siku 100 za ukuwaji. Hustawi zaidi kwenye mazingira ya joto na unyevunyevu.Mmea huu hukua kufikia urefu wa futi mbili hadi nne. Ina wingi wa vitamini A pia ina vitamini B, vitamini E, vitamini C, Riboflavin, Potassium, Manganese. - Jamii nyingi hususa Marekani na bara la Asia wana historia ya kutumia pilipili kichaa kama tiba. Ni dawa yenye nguvu sana na matumizi mengi, hutumika sana kwa kusafisha damu na  kutoa sumu mwilini, pia hutumika kusisimua mzunguko wa damu na kuweka sawa uwiano wa tindikali(acid)mwilini. Pilipili kichaa imetumika kwa maradhi tofauti tofauti ikiwemo moyo, gauts, kupooza homa, kikohozi, tonsilatis, kichefuchefu  hemorhoids  kwa miaka mingi huko Asia na mashariki ya mbali. MAAJABU YA PILIPILI KICHAA; 1.Kutibu kidonda-Hii inaweza kuwa ni ajabu kwa walio wengi lakini ni tiba liyothibitishwa na imekuwa

Kauli ya Kamanda Sirro Kuhusu Askari Aliyefyatua Risasi Angani

Image
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro, leo amezungumza na waandishi wa habari akieleza juu ya mzozo uliotokea baina ya aliyewahi kuwa waziri katika serikali ya awamu ya nne, Adam Malima na Polisi katika eneo la Masaki lililopelekea askari huyo kufyatua risasi kadhaa hewani. Kamishna Sirro alieleza kuwa Mheshimiwa Adam Malima alikuwa ameegesha gari lake eneo ambalo haliruhusiwi kwa ajili ya maegesho ndipo alipokuja mfanyakazi wa kampuni ambayo ni wakala wa ukusanyaji wa madeni, kukamata teksi bubu pamoja na magari yaliyoegeshwa vibaya akiamuru gari la Malima lipelekwe “yard” ya kampuni hiyo. Lakini dereva wa Malima likataa na akaamua kuondoa gari katika eneo lilipokuwa limeegeshwa, ndipo askari wa Polisi alipoingilia tukio lile. “Yule dereva bado alikataa kupeleka gari yard, matokeo yake akaliondoa lile gari na askari wetu alipoona analiondoa lile gari akalirukia na kuingia kwa nguvu kisha akamlazimisha dereva kulirudisha gari lilip

MREMBOJOKATE MWEGELO AWAASA MASTAA WA BONGO KUSAIDIA JAMII ZAO

Image
Mjasiriamali na Mwanamitindo maarufu nchini Tanzania, Jokate Mwegelo, amewaasa watu maarufu nchini Tanzania kujitolea kusaidia kutatua changamoto mbalimbali kwenye jamii ili kupunguza mzigo kwa serikali. Jokate amesema hayo wikiendi iliyopita kwenye mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita wa shule ya Sekondari ya Jangwani . Mrembo huyo ambaye ni Kaimu Katibu Hamasa wa Chipukizi wa (UVCCM), amesema kuwa Tanzania ina watu wengi maarufu na wenye uwezo, lakini wachache tu ndiyo wamekuwa wakijitolea kusaidia sekta mbalimbali husasani Elimu na Afya kwani hali ilivyosasa, ni vigumu kwa serikali kutatua matatizo yote . Jokate alisema Shule ya Jangwani ni Kongwe lakini mpaka sasa inakabiliwa na matatizo mbalimbali wakati kuna wahitimu wengi ambao kwa sasa wana nyadhifa na wanashindwa japo kujitoa kutatua matatizo ya Shule hiyo. “ Mimi sijasoma Jangwani, lakini niliguswa na matatizo ya viwanja vya michezo na kuamua kujenga uwanja wa mpira wa kikapu na mpira wa pete (n

RAIS DKT. MAGUFULI ATEMBELEA SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA TAIFA - TBC

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe wakati alipowasili Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kuangalia uendeshaji wake na kuongea na watumishi leo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt Ayoub Rioba. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akioneshwa sehemu mbalimbali za studio za Redio na Televisheni za Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) alipotembelea leo kuangalia uendeshaji wake na kuongea na watumishi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika moja ya studio za Televisheni za Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) na mtangazaji Bi. Asha Haji alipotembelea leo kuangalia uendeshaji wake na kuongea na watumishi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na watumishi Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) alipotembelea leo kuangalia uendeshaji w