Posts

Showing posts from April 25, 2018

RAIS ZUMA KUOA MKE WA 7, NI BINTI WA MIAKA 24 ALIYEZAA NAYE

Image
ALIYEKUWA Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ameushangaza umma baada ya kuwepo na taarifa za kutarajia kuoa mke wa saba, binti mdogo mwenye umri wa miaka 24. Taarifa hizo zimethibitishwa na binti huyo anayetarajiwa kuolewa na Zuma, Nonkanyiso Conco, kupitia chombo cha habari cha Times Live nchini humo. “Ndio tunaoana, hayo ndiyo naweza kusema kwa sasa, nahitaji kutoa taarifa kabla sijafanya interview (mahojiano) yoyote”, amesikika binti huyo akiuambia mtandao wa Times Live. Conco inti huyo tayari ana mtoto mchanga aliyezaa na Jacob Zuma siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Zuma, April 12, na tayari mahali imeshatolewa. Zuma ambaye ana miaka 76 mpaka sasa ameshaoa mara sita, na hii itakuwa ni mara ya saba kufunga ndoa, Tukio hilo limeonekana kuwakera baadhi ya wananchi wa Afrika Kusini na kutoa maoni yao kwenye mitandao ya kijamii, wakisema binti huyo ni mdogo sana kwa Zuma, kwani wana tofauti ya miaka 52.

Siri Wema Kuutosa Msiba wa Masogange Yafichuka!

Image
Wema Sepetu BAADA ya kuwa gumzo msibani wakati wa kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa video queen kwenye nyimbo mbalimbali za Bongo Fleva, Agness Gerald ‘Masogange’ kutokana na kutoonekana, siri imefichuka ya msanii wa filamu, Wema Sepetu kuutosa msiba huo. Awali habari zilidai kwamba Wema alishindwa kuhudhuria kwenye msiba huo kutokana na kwamba yeye na marehemu Masogange walikuwa na bifu kali na hawakuwahi kupatana. “Unajua Wema na Masogange walikuwa hawaivi, sasa inawezekana ndiyo maana hajaonekana msibani. Au ana sababu nyingine? Mimi kwa kweli nimeshangaa kutomuona,” alisikika akisema mmoja wa waombolezaji aliyekuwa amefika katika Viwanja vya Leaders jijini Dar kuuaga mwili wa Masogange. SIRI YAFICHUKA Kutokana na gumzo la Wema kuutosa msiba huo, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta kwa njia ya simu yake ya mkononi lakini iliita bila kupokelewa. Baada ya kutopokelewa, gazeti hili liliamua kumtafuta meneja wake, Neema Ndepanya ambaye alitoa siri ya Wema kutohudhuria m

Makaburi ya Vigae si Salama

Image
TAARIFA za watafiti zimeeleza kuwa matumizi ya maru maru (tiles, marble, terrazzo) katika kujengengea makaburi siyo salama kwa ardhi, kwani yana kemikali kali ambayo inaathiri udongo. Hayo yamebainishwa na mtaalamu wa Sayansi ya Mazingira na Kilimo, Prof. Julius Zake kutoka Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda , katika ripoti yake ya udongo wa Uganda huku akieelza njia sahihi ya kutumia mbolea na kueleza kwamba ujenzi wa makaburi kwa tiles unaongeza hatari kubwa ya udongo kushindwa kuzalisha. “Zamani watu walikuwa wanatumia nguo maalum (backcloth ) kuzikia wapendwa wao, sasa hivi watu wanakufa sana na wanazikwa kila mahali kwa wingi,tiles haziwezi kuharibika zinaingiliana na mizizi inayorutubisha udongo na kusaidia uzalishaji, hivyo udongo unaathirika na kemikali”, amesema mwanasayansi huyo. Mtaalamu huyo amesema ardhi sasa hivi imekuwa na acid nyingi na kusabaisha kushindwa kuwa na rutuba, ya kuweza kustawisha mazao na kutunza mazingira. CRE

Dodoma yapiga marufuku nyama ya nguruwe

Image
WAKATI leo mkoa wa Dodoma ukiwa mwenyeji wa maadhimisho ya sikuku ya Muungano halmashauri ya manispaa ya Dodoma imepiga marufuku biashara ya nyama ya nguruwe pamoja na mazao yake kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa homa ya nguruwe. Kwamijibu wa taarifa iliyotolewa na Daktari wa mifugo manispaa ya Dodoma Dk, Innocent Kimweri jana alisema kuwa kwa mamalaka aliyopewa na kifungu namba 17 cha sheria ya magonjwa ya mifugo namba 17 ya mwaka 2003 anatangaza kuwa hivi sasa manispaa ya Dodoma inamlipuko wa homa ya nguruwe. Alisema kutokana na hali hiyo kuanzia sasa anaweka zuio la biashara ya nguruwe pamoja na mazao yake hadi hapo itakapo tangazwa vinginevyo. “Hakuna mnyama yeyote wa jamii ya Nguruwe, ngiri nguruwe pori au nguruwe wa kufungwa atakaye ruhusiwa kuingia au kutoka nje ya wilaya ya Dodoma pasipo ruhusa ya maandishi kutoka kwa daktari wa mifugo wa wilaya ya Dodoma mjini”alisema Dk, Kimweri Vilevile alisema kuwa hakuna bidhaa inayotokana na nguruwe ikiwemo m