Posts

Showing posts from November 9, 2016

Jaji Mutungi Avifutia Usajili Vyama Vitatu vya Siasa Nchini

Image
DAR ES SALAAM: Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi leo amevifutia usajili wa kudumu vyama vitatu vya siasa kwa makosa mbalimbali.  Vyama hivyo vilivyofutwa ni pamoja na Chama cha Haki na Ustawi wa Jamii (CHAUSTA) kinachoongozwa na  James Mapalala, Chama cha The African Progressive Party of Tanzania (APPT Maendeleo)  kinachoongozwa na Peter Kuga Mziray na Chama cha Jahazi Asilia kilichokuwa kinaongozwa na Kassim Bakari Ally. Akiongea na wanahabari leo, Jaji Mutungi amesema amevifuta vyama hivyo kwa kutumia kifungu cha 19 cha sheria ya vyama vya siasa namba 5 ya mwaka 1992.    Jaji Mtungi ameongeza kuwa, mchakato wa kufuta usajili wa vyama hivyo unatokana na zoezi la uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa mengine ya sheria ya vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu lililofanyika kuanzia Juni 26  hadi Julai 2016. Katika zoezi hilo la uhakiki ilibainika kuwa vyama tajwa hapo juu vimepoteza sifa za usajili wa kudumu kwa kuki

Rais Magufuli, Nkurunzinza Wampongeza Donald Trump kwa Kushinda Urais wa Marekani

Image
  Leo November 9, 2016 Marekani imeweka historia nyingine baada Donald Trump wa Chama cha Republican kutangazwa mshindi wa kiti cha Urais, na tayari ameanza kupokea pongezi kutoka kwa viongozi wa nchi mbalimbali ikiwemo Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli na Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ni miongoni mwa viongozi waliompongeza Donald Trump kupitia Twitter.   Rais Magufuli ametoa pongezi zake kwa Rais Donald Trump kupitia ukurasa wake Twitter Congratulation President-Elect and people of America for a democratic election,I assure and people of Tanzania for a continued friendship. — Dr John Magufuli (@MagufuliJP) November 9, 2016 Nkurunziza ampongeza Trump Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema ushindi wa Trump ni ushindi wa Wamarekani wote. Mr. @realDonaldTrump , on behalf of the people of Burundi, we warmly congratulate you. Your Victory is the Victory of all Americans. — Pierre Nkurunziza (@pnkurunziza) November 9, 2016 Tupia

Trump Ashinda Urais wa Marekani, Clinton Akubali Matokeo

Image
MAREKANI: Mgombea Urais wa Chama cha Republican, Donald Trump ameshinda kiti hicho. Trumpa ambaye mpaka sasa ana kura 288 huku Hillary Clinton akiwa na kura 218 za wajumbe kati ya kura zote 538. Kwa mujibu wa Katiba ya Marekani, Mshindi wa urais alitakiwa kushinda angalau kura 270 kati ya hizo 538 lakini Bw. Trump amevuka na kufikisha kura 279 mpaka sasa. Clinton akubali kushindwa CNN na NBC wameripoti kwamba mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton amempigia simu Donald Trump na kukubali kushindwa. Shangwe kambi ya Trump Shangwe, nderemo na vifijo zimetanda miongoni mwa wafuasi wa Donald Trump. Trump: Asanteni sana Trump amepanda jukwaani Manhattan, New York. Amewashukuru wafuasi wake na kusema amepigiwa simu na Hillary Clinton “kuwapongeza”. Akizungumza na wafuasi wake baada ya kutangazwa mshindi, Trump amewataka raia wote wa Marekani, waliomchagua na ambao hawakumchagua kuungana na kuanza kuijenga nchi yao kwani muda wa kampeni na siasa za kugawan

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA MWENYEKITI WA BODI YA TANAPA JENERALI GEORGE WAITARA NA MKUU WA JKT BRIGEDIA JENERALI MICHAEL ISAMUHYO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANAPA  ambaye pia Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara alipokutana naye kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Oktoba 8, 2016. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Michael Isamuhyo alipokutana naye kwa mazungumzo   Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Oktoba 8, 2016. Picha na IKULU

BREAKIN NEWZZ!!:- MSIBA MWNGINE MZITO WA TAIFA HUU HAPA WAZIRI WA ZAMANI AFARIKI DUNIA MUDA MCHACHE ULIOPITA GHAFLA!!

Image
Aliyewahi kuwa Waziri mwandamizi katika wizara mbalimbali, ikiwemo Wizara ya Elimu, Ndg.Joseph Mungai, amefariki dunia jioni ya leo, katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alipokua akipatiwa matibabu. Mungu ampumzishe kwa amani.! Posted by BONGO YETU at Tuesday, November 08, 2016 Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook Share to Pinterest