Posts

Showing posts from March 15, 2016

Mama Diamond Atoa Siri ya Zari

Image
Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ametoboa siri ya mkaza mwanaye, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kushindwa kuishi Bongo na badala yake kukimbilia nchini Afrika Kusini ‘Sauz’. Sandra au Mama D aliyasema hayo katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda juu ya uhusiano wake na Zari kufuatia tetesi kuwa hawaivi ndipo akaweka mambo sawa. Mama D alisema kuwa yeye na Zari wapo vizuri lakini kinachomfanya mkwewe huyo kushindwa kuishi naye Bongo ni kutokana na biashara zake kudoda nchini Afrika Kusini. “Unajua anapokuwa huku (Bongo), biashara zake huwa zinayumba sana, wakati mwingine akipiga simu akiulizia biashara zinakwendaje anaambiwa hali ni mbaya au hazijaingiza chochote hapo ndipo huwa anachanganyikiwa. “Kwa mfano hivi karibuni alipiga simu akaambiwa hakuna fedha kabisa na biashara haziendi. Kilichofuata ni kujiandaa na kumchukua Tiffah (Latifah Nasibu) kisha akaondoka zake. “Hicho ndicho kinacho

Siri Imefichuka...CUF Watoa Sababu za Maalim Seif Sharif Hamad Kuishi Serena Hoteli Pamoja na Gharama Iliyotumika Hadi sasa

Image
SIRI imefichuka kuhusu hatua ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (SUK), Maalim Seif Sharif Hamad, kuishi hotelini jijini Dar es Salaam. Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), amekuwa akiishi katika Hoteli ya Serena jijini Dar tangu aliporuhusiwa kutoka Hospitali ya Hindu Mandal Machi 8, mwaka huu alipokuwa amelazwa kwa matibabu. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mmoja wa ofisa wa ngazi za juu wa CUF, alishangazwa na hatua ya baadhi ya watu kuhoji kiongozi huyo kuendelea kuishi hotelini hapo. Alisema hatua ya kiongozi huyo kuishi hotelini ni matokeo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kushindwa kutekeleza ahadi ya kumpa nyumba pindi anapokuwa Dar es Salaam katika shughuli zake. Alisema kutokana na hali hiyo imekuwa ni utaratibu kwa kiongozi huyo kufikia katika hoteli hiyo na gharama za kuishi hotelini hapo hulipwa na SMZ kwa mujibu wa sheria. “Tangu mwaka 2010 Maalim aliah

Rais Magufuli Awaapisha Wakuu wa Mikoa

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hafla hiyo fupi ya kuwaapisha Wakuu hao wa Mikoa imefanyika leo Ikulu,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga  kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Zelote Steven Zelote kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Mh. Anne Kilango Malecela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Paul Christian Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel E

ZIARA YA WAZIRI MKUU WILAYANI ISSENYI 2

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majajaliwa  akifurahia zawadi ya picha aliyozawadiwa na wananchi wa Kata ya Kakunyu wilayani Missenyi akiwa katika ziara ya mkoa wa Kagera  Machi 14, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Afisa Mifugo  wa Kata ya Kakunyu wilayani Missenyi, Eric Kagoro  akitoa maelezo mbele ya Waziri Mkuu na wananchi kuhusu tuhuma kuwa analinda wafugaji toka nchi jirani wanaolisha mifugo yao kwenye ardhi ya Tanzania kinyemela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)