Posts

Showing posts from October 24, 2013

MUUZA CHIPS AMTEKA MTOTO TANDALE DAR NA KUTOKOMEA NAE KUSIKOJULIKANA

Image
MTOTO wa kike mwenye umri wa miaka mitatu, Maryment Ibrahim ambaye anaishi Tandale jijini Dar es Salaam, hivi karibuni alipatwa na masahibu makubwa baada ya kutekwa nyara na kutoroshwa hadi Gairo mkoani Morogoro huku mtekaji akidaiwa kutaka apewe shilingi milioni 6 ili amuachie. Mama mzazi wa mtoto aliyetekwa akiwa na mwanaye. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Oktoba 16 mwaka huu baada ya kijana mmoja, anayefanya biashara ya kuuza chipsi anayejulikana kwa jina la Issa Ramadhani, kudaiwa kumchukua mtoto huyo aliyekuwa akicheza nyumbani kwao na kutoweka naye kabla ya wazazi wake kubaini na kwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’. Awali, ilidaiwa Ramadhan alikuwa na tabia ya kuwachukua watoto wadogo wa mtaani hapo na kuondoka nao na kuwarudisha baadaye, kitu kilichowafanya wazazi wa mtoto huyo kutokuwa na wasiwasi. Mtuhumiwa wa utekaji. Wakizungumza na mwandishi wetu, wazazi wa mtoto huyo walisema waliamua kutoa taarifa polisi na

Msanii wa bongo movie anusurika kuliwa KIBOGA.....Alizidisha pombe na kujikuta chooni akiwa mtupu.

Image
Muigizaji wa filamu za kibongo anayejulikana kwa jina la Danny Cloud maarufu kama Danny mtoto wa mama ambaye alipata umaarufu wa jina hilo kupitia filamu ya mtoto wa mama amenusurika kubakwa ( kuliwa kiboga ) Akizungumza na mpekuzi wetu, rafiki wa karibu wa msanii huyo alidai kwamba Danny alikuwa maeneo ya Bilcanas ambapo alipewa ofa ya pombe na jamaa zake... Rafiki huyo alidai kuwa, baada ya kupewa ofa hiyo adimu, msanii huyo alianza kuiparamia pombe mfano wa mtu mwenye kiu kali ya maji, hali iliyomfanya asijitambue na kuanza kuvua nguo... "Kuna wakati Danny alinyanyuka na kuelea chooni huku akipepesuka...Alipofika huko alidondoka na kulala huko huko chooni, hali iliyowafanya vibaka watake kumla kiboga"...Alisema huyo rafiki yake na kuongeza: "Baada ya kimya kirefu, ilibidi tukamwangalie ambapo tuliwakurupusha vijana watatu wakiwa wameshamvua nguo"