Posts

Showing posts from May 20, 2015

WATEJA WA VODACOM KUPERUZI INTANETI BURE

Image
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa akisisitiza jambo. Dar es Salaam, May 20, 2015: Zaidi ya watumiaji milioni 13 wa mtandao wa simu za mkononi kuanzia leo wataweza kuperuzi internet inayofikia MB100 kwa masaa mawili bure kuanzia saa 12 alfajiri hadi saa 2 asubuhi kutokana na ofa inayojulikana kama " Good Morning Tanzania" inayotolewa na Vodacom Tanzania. Promosheni hii imeanzishwa kutokana na kuonenakana kuwepo kwa mahitaji makubwa ya matumizi ya data katika kupata  taarifa kupitia mtandao wa intaneti. Vodacom Tanzania siku zote imekuwa mstari wa mbele kubuni huduma zinazoendana na matakwa ya wateja wake na kuwarahisishia maisha katika nyanja ya elimu, afya,… Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa akisisitiza jambo. Dar es Salaam, May 20, 2015: Zaidi ya watumiaji milioni 13 wa mtandao wa simu za mkononi kuanzia leo wataweza

ABBAS MTEMVU AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MAENEO YALIYOHARIBIWA NA MVUA

Image
  Diwani wa Soko la Tazara Vetenary Zahoro Maganga akitoa maelezo kwa Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu alipotembelea maeneo yaliyoharibiwa  na mvua akiongozana na  viongozi wa Wakala wa Serikali wa Barabara (TANROADS) jinsi maji yanavyotakiwa kufata mfereji huo ambao haupitishi maji kupeleka katika mfereji huo.  Abbas Mtemvu (kulia) akizungumza na viongozi wa Wakala wa Serikali wa Barabara (TANROADS) …   Diwani wa Soko la Tazara Vetenary Zahoro Maganga akitoa maelezo kwa Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu alipotembelea maeneo yaliyoharibiwa  na mvua akiongozana na  viongozi wa Wakala wa Serikali wa Barabara (TANROADS) jinsi maji yanavyotakiwa kufata mfereji huo ambao haupitishi maji kupeleka katika mfereji huo.  Abbas Mtemvu (kulia) akizungumza na viongozi wa Wakala wa Serikali wa Barabara (TANROADS)  katika ziara ya kutembelea maeneo yaliyo haribiwa na mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam (kushoto) ni Meneja wa Tanro

JE,NI KWELI WEWE HUJITAMBUI? NA KWANINI UNATAKIWA KUJITAMBUA?

Image
Kujitambua ni uwezo na uelewa wa kujua wewe ni nani, una kusudi gani, wapi na watu gani kwa muda upi. Ni uwezo wa kujua wapi ulikotoka na wapi unaelekea na unatakiwa uwe kwenye eneo gani. Je unajitambua? Asili yako ni nini? Katika harakati za kujitambua unaanzia kwenye asili yako, asili yako ni utu wako, kusudi lako na mpango mzima wa maisha yako. Kama umeelewa asili yako vizuri ni rahisi kujua wewe unapaswa kufanya nini wapi na watu gani, ingawa tumekuwa na tatizo la kutokujua wapi tunatoka na tuelewe wapi tunakwenda na watu gani? Bila kujua tumepoteza mwelekeo wa kile ambacho tunapaswa kufanya kila siku kufikia kule tunanatakiwa kufika katika maisha yetu. Je Utu wako ni nini na unajengwa na nini? Vijana wengi tumejikuta tukipoteza dira na maisha wakati mwingine kwa sababu utu wetu tumewauzia watu wengine kwa kubadilishana na fedha au umaarufu. Baada ya kuuza utu wetu tumelazimika kufanya mambo ambayo yatamfurahisha mtu fulani au au watu

PICHA TATA ZA KIMAHABA NIUE ZA WEMA NA KADINDA ZAWAPA WENGI MASWALI VICHWANI.

Image
 BONYEZA KUONA PICHA MATATA ZAIDI

AUNTY EZEKIEL NA WEMA SEPETU VILIO TUPU, WAKUTANISHWA LAIVU NA KUAMUA YAFUATAYO

Image
Imelda Mtema Baada ya kula viapo vya kutozikana, wasanii wawili wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Aunt Ezekiel Grayson wamejikuta wakiangua vilio wakati wakipatanishwa na rafiki yao mkubwa ambaye ni pedeshee anayejulikana kwa jina la Daudi Mambya. Habari kutoka kwa shuhuda wetu zilieleza kwamba, tukio hilo lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Ufukwe wa Coco jijini Dar ambapo Daudi aliwaita kwa mwaliko wa mishikaki bila wenyewe kujua kinachoendelea. Habari zilieleza kuwa, Daudi ambaye kwake huwa hawafurukuti, amekuwa akiumizwa mno na tofauti ya wasanii hao kwa sababu ni watu walikuwa wakipendana hivyo kugombana kwao kulikuwa kunaleta shida kwa marafiki zao wengine. Imefahamika kwamba, Daudi alitumia ujanja wa kuzungumza na kila mmoja kwa wakati wake ambapo alibaini kuwa hakuna aliyekuwa tayari kupatana na mwenzake. Ilisemekana kuwa, Daudi alitumia ujanja wa kitaalamu ili kila mmoja kumuweka sawa bila kujijua. “Unajua Daudi ni rafiki ya

JOKETI KIDOTI KAACHIA PICHA MPYA AKIONYESHA UMBO LAKE LILIVYO BOMBA

Image
Instagram umekuwa ni mtandao ambao hakika umeleta upinzani mkubwa kwenye mitandao mingine ya kijamii diniani kwa sasa mastar na wasio mastar wamekuwa wateja wa mtandao huu sasa tukutane na picha hizi toka kwa JoketTanzania singer and model Jokate "Kidoti" Mwagelo shared this images today oops!! OMG men will flaunts after see this.

MAHAKAMA YA HAKI ZA BINADAMU YA AFRIKA YAWANOA WAANDISHI WA HABARI ARUSHA

Image
Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya kimataifa la Ujerumani(GIZ)inayosaidia kujenga uwezo wa taasisi za Uongozi na Utawala bara la Afrika,Dk Iris Breutz akizungumza wakati wa semina ya siku nne ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kutoka nchi za Afrika Mashariki namna Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCPHR) inavyofanya kazi zake leo jijini Arusha,kushoto ni Jenerali Ulimwengu ambaye ni mwezeshaji na Mkuu wa Mawasiliano wa AfCPHR,Chatbar Sukhdev. Mkuu wa Mawasiliano wa AfCPHR,Chatbar Sukhdev akitoa nasaha zake kwenye semina hiyo itakayowapa waandishi wa habari uelewa mpana wa Mahakama hiyo yenye makao yake jijini Arusha. Baadhi ya waandishi wa habari wakijifunza mambo mbalimbali yanayohusu kulinda Haki za Binadamu barani Afrika.

RAIS WA MSUMBIJI FELIPE JACINTO NYUSI ALIHUTUBIA BUNGE DODOMA

Image
Rais Wa Msumbiji Felipe Jacinto Nyusi akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo mjini Dodoma huku Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Spika wa Bunge hilo Mh.Anna Makinda wakisikiliza. Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais wa Msumbiji Felipe Jacinto Nyusi,Waziri Mkuu Mizengo Pinda,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi waandamizi katika serikali ya Msumbiji wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Rais wa Msumbiji kulihutubia Bunge lao mjini Dodoma. Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikweteakimtambulisha katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa Rais wa Msumbiji Felipe Jacinto Nyusi wakati Rais huyo wa Msumbiji alipowasili katika makao makuu ya CCM m.Jakayajini Dodoma na kuzungumza na viongozi waandamizi .Kushoto ni Naibu katibu Mkuu wa CCM Bwana Mwigulu Nchemba .

MANISPAA YA KINONDONI YAENDELEA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS LA KUONDOA MAJI KWENYE MAKAZI YA WATU TEGETA, BUNJU NA KUNDUCHI NA KUJENGA MFEREJI WA KUDUMU KUPITISHA MAJI KUELEKEA BAHARINI.

Image
Mkuu wa mkoa wa Dar es slaam,Saidi Meck Sadiki(katikati) akiangalia athari ya maji yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni jijini Dar es slaam akiwa ameambatana na wakazi wa eneo hilo la Kunduchi Ununio.Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na DAWASA inaendelea na zoezi la kuyaondoa maji hayo pamoja na ujenzi wa mfereji mkubwa kuelekea baharini utakaokusanya maji kutoka Bunju na Kunduchi na kuyapeleka bahari ya Hindi. Kazi ya ujenzi wa mfereji huo mkubwa wenye urefu wa kilometa 2.1 ikiendelea katika eneo la Kunduchi Ununio. Maji yaliyotuama yakiwa bado yamezingira nyumba na makazi ya watu eneo la Boko jijini Dar es salaam ambayo harakati za kuyaoondoa zinaendelea kufanywa na manispaa ya Kinondoni. Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadiki ( katikati ) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni Musa Nati wakati akikagua utekelezaji wa zoezi la kuondoa maji katika makazi ya watu eneo la Basihayo Tegeta. …

UANDIKISHAJI WANACHAMA 'TANZANIA BLOGGERS NETWORK' (TBN),

Image
Chama cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Jamii nchini 'Tanzania Bloggers Network' - TBN kilichosajiliwa rasmi na Serikali Aprili 2015 na kupewa namba ya usajili; S. A 20008 kinapenda kuwajulisha wanaotaka kujiunga na chama hicho kuwa fomu za kujiunga zinatolewa.  Wahusika ni wamiliki na waendeshaji wote wa mitandao ya kijamii (blogs na forums) Tanzania na Watanzania wanaofanya kazi kama hiyo nje ya nchi. Sifa kuu kwa mwanachama ni kuwa na blog ambayo ina umri wa miezi sita tangu ianze kuendeshwa mfululizo ambayo ipo hai. Kwa wakazi wa Dar es Salaam wenye sifa na wanataka kujiunga na TBN fomu zinapatikana kwenye Ofisi za Muda za Tanzania Bloggers Network (TBN) kwenye Jengo la Dar Free Market lililopo mkabala na Barabara ya Ally Hassan Mwinyi. Mwanachama muitaji wa kujiunga kabla ya fomu atatakiwa kutoa shs 25,000/- ikiwa ni Kiingilio cha mwanachama, shs 15,000/- yakiwa ni malipo ya ada ya miezi mitatu kwa mwanachama na shs 10,000/- ikiwa ni ma

MAOFISA WANANE WA BENKI KUU TANZANIA (BOT) KIZIMBANI KWA MASHITAKA 14 YA KUFOJI VYETI VYA KIDATO CHA NNE

Image
Habari na Mwene Said wa Globu ya Jamii .  Maofisa wanane wa Benki Kuu Tanzania (BOT) wamekutwa na kesi ya kujibu na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salam, dhidi ya mashitaka 14 ya kughushi na kuwasilisha vyeti vya kidato cha nne vilivyoghushiwa.   Uamuzi huo ulitolewa na Hakimu Mkazi Nyigulila Mwaseba baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wao, dhidi ya washtakiwa Justina Mungai, Christina Ntemi, Siamini Kombakono, Janeth Mahengena Beatha Masawe, Jacquiline Juma, Philimina Mutagurwa na Amina Mwinchumu.   Hakimu Mwaseba alisema baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wa Jamhuri bila kuacha shaka washtakiwa wana kesi ya kujibu na kwamba wanatakiwa kupanda kizimbani kujitetea dhidi ya mashitaka yao. Hakimu alisema kesi hiyo itaanza kusikilizwa utetezi wao Juni 16 hadi 17, mwaka huu. Watumishi hao wa Benki Kuu wanadaiwa kuwa katika kitengo cha kuhesabu fedha vya BoT. Mapema Septemba 19, mwaka 2008, upande wa Jamhuri uliwasomea washtakiwa ha