Posts

Showing posts from February 28, 2017

Waziri Nape: Sikupinga vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali nilishauri busara itumike

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametoa ufafanuzi juu ya kauli iliyonukuliwa ikionyesha kuwa alipinga vita dhidi ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Amedai kuwa hakupinga vita hiyo bali alitaka busara itumike kwa washukiwa. Waziri Nape alitoa ufafanuzi huo katika kipindi cha dakika 45 cha ITV, alipoulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho kutaka kujua kuhusu kauli yake iliyoonesha kupinga utaratibu uliotumika wa kuwakamata au kuwapata watuhumiwa wa dawa za kulevya. “Niseme kwanza ilitokea nilikuwa na mkutano na waandishi wa habari, ukienda leo ukanitaja Nape ukaniambia baada ya siku mbili njoo kituoni, hata kama nilikuwa na madawa ya kulevya nyumbani kwangu hivi unayakutaje?  'Kwasababu kwa vyovyote vile nitayachukua, ntayaficha, ntakuja kituoni ntaripoti utanibana ntakwambia twende nyumbani kwangu ukakague mnaenda mnakagua mnakuta hamna, si basi!  &q

MKUU WA JESHI LA ULINZI TANZANIA NA MNADHIMU MKUU WALA KIAPO CHA UADILIFU KWA VIONGOZI WA UMMA

Image
 Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (CDF), Jenerali Venance Salvatory Mabeyo akila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma leo Jijini Dar es Salaam. Kulia anayeshuhudia ni Kamishna wa Maadili wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold Nsekela leo Jijini Dar es Salaam.  Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (CDF), Jenerali Venance Salvatory Mabeyo akitia saini katika Hati ya Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma leo Jijini Dar es Salaam. Kulia anayeshuhudia ni Kamishna wa Maadili wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold Nsekela leo Jijini Dar es Salaam.  Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (CDF), Jenerali Venance Salvatory Mabeyo akipokea Hati ya Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kutoka kwa Kamishna wa Maadili wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold Nsekela leo Jijini Dar es Salaam.  Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Tanzania, Luteni Jenerali James Alois Mw

WAZIRI NAPE ATUMA SALAMU ZA POLE KWA SHIRIKISHO LA RIADHA NCHINI

Image

MSANII YUSUPH MLELA ATOA MANENO HAYA KWA WASANI WENZAKE

Image
Msanii mkongwe wa filamu Yusuph Mlela amewataka wasanii wenzake wa filamu kuacha kulalamika na kufanya kazi kwa bidii kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuikomboa tasnia ya filamu. Akiongea na Bongo5 wiki hii, Mlela amedai kuwa wasanii wengi wanatakatamaa kwa kauli ya soko limeyumba wakati wao ndiyo watu pekee ambao wanaweza kuikomboa tasnia ya filamu. “Suala la soko wadau wanasema limeyumba, lakini naweza kusema huu ni wakati wa kuamka na kuanza kufanya kazi upya kulikomboa soko la filamu, kama wanasema kazi ni mbaya tufanye kazi nzuri, kila kitu tunaweza kufanya. Mimi nadhani huu ni wakati wa wasanii wa filamu kuamka na kufanya kazi kwa bidii ili kuirudisha ile hali ya zamani,” alisema Mlela. Muigizaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri ndani ya tamthilia ya Kashfa inayorushwa na Azam TV, anajipanga kuachia filamu yake mpya ‘Mr Bodaboda’ Machi mwaka huu.

MREMBO BATULI AMLIPUA LAIVE WEMA SEPETU

Image
Muigizaji wa filamu nchini, Yobnesh Yussuf maarufu kama Batuli amekanusha taarifa iliyotolewa na Wema Sepetu kuwa CCM haijawalipa pesa za kampeni ya Mama Ongea na Mwanao kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Akizungumza na wanahabari kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Protea, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ akiwa na Ndumbangwe Misayo ‘Thea’,amesema madai aliyoyatoa Wema Sepetu hayana ukweli wowote kwa sababu wasanii wote walilipwa. “Nikiwa kama makamu mwenyekiti wa group hili la Mama Ongea na Mwanao kwa muda ni kweli inasemekana kwenye mitandao kuwa tulifanya kampeni na hatukulipwa, mimi kama mwenyekiti msaidizi wa muda nakanusha taarifa hizo kuwa si za kweli. Ingawa kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani,wapo wanaoshawishiwa kulichafua kundi letu, kumchafua Makamu wa Rais Bi Samia Suluhu na kuichafua CCM, mimi nakataa, sote tumelipwa na mikataba ipo, haiwezekani we staa mkubwa unakaa kwenye media unaongea uongo kwamba wasanii hatujalipwa.” Ameongeza, “Zipo simu za kutus