Posts

Showing posts from November 24, 2017

Kinana, Nape waunganisha nguvu tena

Image
 Arumeru. Katibu mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na mbunge wa Mtama, Nape Nnauye wameunganisha nguvu katika Kata ya Makiba ambako wanampigia debe mgombea wa chama hicho, Samson Laizer. Kinana na Nape wanachukuliwa kama wanasiasa waliofanya kazi kubwa ya kuhuisha nguvu ya CCM kabla ya Uchaguzi Mkuu uliopita baada ya kuzunguka karibu nchi nzima kupiga siasa na wakati mwingine kudiriki hata kuwasema hadharani mawaziri wa Serikali ya CCM, wakiwaita mizigo. Jana wawili hao waliungana na Mrisho Gambo, ambaye ni mkuu wa mkoa wa Arusha na Alexander Mnyeti (Manyara) kuipigia debe CCM. Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Kijiji cha Makiba wilayani Arumeru, Kinana alisema ni vigumu vyama vya upinzani kushika nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu ujao. Kinana alisema akiwa katibu mkuu wa CCM ametembelea mikoa, wilaya na kata tofauti ambako ameona wananchi wana imani kubwa na chama hicho. Kinana alisema katika uchaguzi mkuu uliopita wananchi wa eneo hilo walipig

Alichokisema Dk Slaa baada ya kuteuliwa

Image
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo, Dkt. Wilbroad Peter Slaa, amemshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumteua kuwa Balozi wa Tanzania na kusema kuwa yuko tayari kutoa mchango wake katika kulijenga taifa la Tanzania. “Kwa sababu Ubalozi uko kwenye Idara za moja kwa moja za mkuu wa nchi, na bila shaka hakukuwa na sababu mkuu wangu kutotaka kuniteua, ninamshukuru kwa uteuzi huo kwa kuniona, ninachoweza tu kusema katika hatua hiyo ni kwamba ninao wajibu mkubwa hasa katika kipindi hichi cha kulijenga taifa letu,” amesema Dkt. Slaa. Dkt. Slaa ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, na ambaye aliwahi kugombea nafasi ya Urasi kupitia chama hicho, alijiuzulu nafasi yake hiyo kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na kuondoka nchini. Muda mfupi baadaye Dkt. Slaa alitangaza kutojihusisha tena na siasa za hapa nchini na akawa anaishi nchini Canada pamoja na mpenzi wake Josephine Mushumbusi. Dk. Slaa, ambaye kwa sasa ana

BREAKING : AJALI MBAYA YAUWA WATU 10 NA KUJERUHI 24 MKOANI SINGIDA

Image
Gari aina ya Noah iliyopata ajali kwa kugongana na lori katika eneo la Kijiji cha Isuna , mkoani Singida na kusababisha vifo vya abiria 13, jana. Picha na Gasper Andrew <span data-mce-type="bookmark" style="display: inline-block; width: 0px; overflow: hidden; line-height: 0;" class="mce_SELRES_start"></span> Watu kumi wamekufa na wengine 24 kujeruhiwa baada ya gari aina ya Toyota Hiace kugongana uso kwa uso na gari aina ya Toyota Noah, katika eneo la Ihuka mkoani Singida. Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo, dereva wa gari aina ya Toyota Hiace alikuwa akijaribu kulipita gari jingine bila mafanikio, ndipo alipogongana na gari hilo nakusababisha maafa makubwa. Gari aina ya Noah iliyopata ajali kwa kugongana na lori katika eneo la Kijiji cha Isuna , mkoani Singida na kusababisha vifo vya abiria 13, jana. Picha na Gasper AndrewBRE

Rais Magufuli Amtumia Spika Wa Bunge Salamu Za Rambirambi Kifo Cha Gama

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Mh. Leonidas Tutubert Gama. Mhe. Leonidas Tutubert Gama amefariki dunia jana tarehe 23 Novemba, 2017 saa 4:25 usiku katika hospitali ya Mtakatifu Joseph ya Peramiho, iliyopo Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma ambako alikimbizwa kwa matibabu baada ya kuugua ghafla. “Nimepokea kwa mshtuko na majonzi taarifa za kifo cha ghafla cha Mhe. Leonidas Tutubert Gama, nakupa pole Mhe. Spika Job Ndugai, Wabunge na wafanyakazi wa Ofis yako, na kupitia kwako naomba uzifikishe salamu zangu za pole kwa familia ya Marehemu, wananchi wa Jimbo la Songea Mjini na Mkoa mzima wa Ruvuma, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu” amesema Mhe. Rais Magufuli. Aidha,, Mhe. Rais Magufuli amem

Wolper Alia Kutengwa na Mastaa

Image
Jacquline Wolper. STAA wa Bongo Movies, Jacquline Wolper amesema kuwa mastaa wengi hawapendi kupeana ‘sapoti’, kiasi kwamba hata kama staa mwenzao akiwa na biashara yake wapo radhi kununua kwingine lakini si kwake, ili tu wamkomoe. Akichonga na gazeti hili, Wolper alijitolea mfano kwa kusema kuwa tangu amejiingiza kwenye biashara ya ushonaji, watu wengi ambao wamekuwa wateja wa biashara zake ni wa kawaida tu na wasanii wenzike hawazidi hata watatu. “Unapofanya maendeleo kwa sisi mastaa wenzako si kwamba wanapenda. Wananuna ndiyo maana huwezi kuwaona wakikusapoti,” alisema Wolper.

Tabia 6 za kufuata kupata ngozi laini bila madoa/beauty habits to get glowing skin

Image
1.TUMIA ANTIOXIDANT SERUM. Sio kila mtu ana bahati ya kupata ngozi laini na nyororo bila kuifanyia kazi. Kwa wengine it a must to work hard ili kupata that perfect skin you have always wanted. So Ladies you have to change your beauty routine, unatakiwa uanze asubuhi yako in a healthy way. Jinsi unavyoanza siku yako itaonesha kwenye uso wako. Antioxidants kama vile Vitamin C&E hulinda ngozi yako ili isi dehydrate na pia zile aging radicals zitalindwa from UV-ray pollution na bad dietary habits(kula vibaya). Paka antioxidant serum baada tu ya kutoka kuoga, subiri dakika chache then paka moisturizer yako. 2.KULA PROTEIN YA KUTOSHA. Kula breakfast ambayo ipo high in protein, husisha mayai, karanga, yogurt nk. Hivi husaidia kujenga collagen ambayo ndio kitu kikubwa ambacho hukusaidia ngozi yako isizeeke mapema. Ngozi yako haitokuwa na mikunjo wala kutepeta. Watu ambao hula protein for breakfast hula kidogo for the rest of the day, na pia protein husai

ANGALIA WEMA SEPETU ALICHOSEMA USIKU HUU AKIWA RWANDA,ATOA YA MOYONI

Image
    Spotted walking out of RBA Television earlier today… This will be the last pic I post kwa Leo… For all my Updates fanya kuDownload app yangu mwenyewe… (Feels good to say that)… Goodnyt World

BREAKING : MBUNGE WA JIMBO LA SONGEA MJINI AFARIKI DUNIA

Image
Taarifa zimetufikia asubuhi hii,zikieleza kuwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Songea Mjini,Mh Leonidas Gama amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.Mbunge wa Songea Mjini Leonidas Gama amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Peramiho alikokuwa anapatiwa matibabu. Marehemu alipata kuwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya kadhaa zikiwemo Ilala, Muheza, Nachingwea, Newala na Mbeya.Tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu zaidi wa taarifa hiyo.MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMINA Post Views: 47

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 24.11.2017

Image
                                     

MAGAZETI YA UDAKU LEO STORI KUBWA LULU AIBUA MAZITO JELA,MKUU WA MAGEREZA AONGEA

Image
      Post Views: 68

MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI

Image
          Post Views: 16