Posts

Showing posts from January 18, 2014

MKE WA MTU AKUTWA NYUMBA YA KULALA WAGENI AKIFANYA BIASHARA YA KUUZA NDOA KINYUME CHA SHERIA MJINI MOROGORO. P

Image
MAKUBWA madogo yana nafuu! Kwenye kamatakamata na fumuafumua ya magenge ya biashara haramu ya ngono mjini hapa imemkumba bonge la jimama ambalo lilinaswa gesti likisubiri mteja. Tukio hilo lilijiri hivi karibuni wakati vijana wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers ilipopata mwaliko maalum kutoka jeshi la polisi Moro kwa ajili ya kufichua biashara hiyo haramu ambapo mwanamke huyo alinaswa kauchapa usingizi chumbani huku kitandani kukiwa na kondomu kibao. Hapa akiwa kitandani.  Ndani ya gesti maarufu ya Itigi iliyopo maeneo ya Msamvu, inayotumiwa zaidi na madereva wa malori ya masafa marefu ndipo alipobambwa bonge ambaye katika utetezi wake alidai kuwa ni mke wa mtu. “Naombeni mnisamehe nilikuwa najitafutia riziki, baba J akijua ataniua jamani amesafiri, akirudi nimekwisha,” alisema kwa aibu mwanamke huyo. aliyejulikana kwa jina la mama J. ... bonge akiwa katika pozi la aibu baada ya kubanwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Pu

HATIMAYE, MASOGANGE AMUANIKA MTU ALIYEMTUMA ABEBE MADAWA YAKE

Image
HATIMAYE yule Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ aliyepatikana na hatia ya kuingiza nchini Afrika Kusini malighafi haramu aina ya ephedrine, amemtaja mtu aliyemtuma mzigo huo kuwa ni Mkongomani, Risasi Jumamosi limedondokewa na ‘kismati’. Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’. Katika mahojiano ‘spesho’ na gazeti hili yaliyofanyika kwenye ofisi za Global Publishers, Bamaga, Mwenge, Dar es Salaam, juzi, Masogange aliamua kumwanika kigogo huyo huku akimtaja jina bila kuuma maneno. Melisa Edward. TWENDE PAMOJA Risasi: Masogange tumekuita leo hapa kwa ajili ya mahojiano maalum. Tangu umerudi Bongo toka Afrika Kusini ulikokutwa na ule msala wako, naamini hujawahi kuzungumza na chombo chochote cha habari. Uongo, kweli? Masogange: Kweli kabisa. Risasi: Risasi linakukaribisha tuzungumze mambo muhimu, lakini kubwa kuliko yote, hebu mtaje mtu aliyekutuma kubeba ule unga ambao ulikamatwa nao Afrika Kusini. Masogange: (akionesha sura ya umak

MWASITI AANIKA MAISHA YAKE ! AZUNGUMZIA UMRI,NDOA,KUZAA NA KUANZA MAPENZI 

Image
 MKONGWE katika gemu la muziki wa Bongo Fleva, Mwasiti Almas amefunguka ‘exclusive’ kuhusiana na maisha yake kwa jumla ambapo kwenye masuala ya uhusiano amebainisha kuwa alimjua mwanaume mara baada ya kumaliza kidato cha nne. Mkongwe katika gemu la muziki wa Bongo Fleva, Mwasiti Almas. Alisema alijitunza sana akiwa shule ya msingi, akaendelea hivyo hadi alipomaliza masomo ya sekondari ndipo alipolegeza uzi na kujikuta ameanza kuvunja amri ya sita na kujua thamani ya mwanaume. “Nilikuwa muoga sana, tangu shule ya msingi hadi sekondari sikuweza kabisa kufanya mambo ya kikubwa,” alisema. Akizungumza na Weekly Star Exclusive, Mwasiti alifungukia umri wake ambapo alikiri ‘eji’ imeenda lakini suala la kuolewa ataendelea kusubiri hadi muda muafaka utakapofika. “Kuhusu umri kwa sasa nipo katikati ya 25 hadi 30, umri umeenda kidogo siyo mdogo mimi. Nitaolewa tu muda ukifika, sina haja ya kuharakisha,