Posts

Showing posts from August 2, 2016

EXCLUSIVE…MWANA DADA WA CHADEMA JOYCE KIRIA AMKATAZA MUMEWE KUSHIRIKI KAMPENI YA UKUTA.

Image
HIVI NDIYO ALIVYO ANDIKA KUPITIA MTANDAO WAKE WA FACEBOOK Nimeshamuomba sana shemeji yenu asome alama za nyakati jamani..Mkuu wa Kaya wa sasa kwa kweli hapanaaaaa wasimshike sharubu pls…. Hii UKUTA uuuuuwiiii nimemwomba jamani waipige chini watafute njia nyingine ya kumaliza migogoro ya kisiasa . . Kinamama wenzangu Hasa WAKE wa hawa wanaUKUTA pls tuwashauri waume zetu jamani tusisubiri mambo yaharibike kisha ndo tuanze kulia wakati tunaweza kuwazuia wasifanye jazba jamaniii… Hats kwenye nyumba hamuwezi wote kuwa wa babe jamani lazima mmoja awe chini jamaniii … . . Kiukweli wamefanya kazi kubwa nzuri katika Taifa hili na mbinu zao zilifanikiwa sana kwa serikali iliyopita kwa sababu Dady alikuwa hana neno mkwere wa watu, anawachekea na kuwapa nafasi ya kuwasikiliza na juice wanapewa, lakini sasaivi uuuuuuwiiiii wapunguze spidi na wasome sana mchezo, HUU MCHEZO HAUHITAJI HASIRA huyu BABA hacheki jamaniiiii .. Wasimjaribu jamaniiiii . . Yaani ki

MO Dewji aikabidhi Simba Mil. 100 za usajili, asema akiipata bajeti ya usajili itakuwa zaidi ya Bilioni

Image
Hatimaye ahadi ya shabiki wa Simba, ambaye ni Mkurugenzi wa Makampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group), Mohammed Dewji amekamilisha ahadi aliyoisema kabla ya mkutano mkuu wa Simba kwa kukabidhi Milioni 100 kwa uongozi wa Simba kwa ajili ya kufanya usajili. MO amekabidhi pesa hizo baada ya kueleza mipango yake kwa Simba ya kuwa kama wanachama wa Simba wataridhia kufanya mabadiliko basi atachangia pesa ya usajili jambo ambalo katika mkutano wake wa Jumatatu na waandishi wa habari kuwa ahadi yake ni kweli na ataikamilisha kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Akizungumza baada ya kupokea cheki kutoka kwa MO, Rais wa Simba, Evans Aveva, amemshukuru MO kwa msaada huo na sasa wanasimba watatembea kwa kujiamini kwani wamepata pesa ya kufanya usajili. “Nakushukuru MO kwa msaada ambao umetupatia tunaamini ni mapenzi ambayo unayo kwa Simba ndiyo umefanya uwe tayari kutoa pesa hizi na sisi tunaamini zitaweza kutusaidia kupiga hatua na hata tuweze kutembea

WASANII, WATANGAZAJI NA WATU MAARUFU KUVUNA MAPESA KUPITIA MITANDAO YAO YA JAMII.

Image
Katibu Mkuu wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel (katikati) akimsifia msanii Diamond Platinumz kwa jinsi ambavyo amekuwa akiitanga Tanzania nje ya nchi kwa muziki wake. Mkurugenzi wa Kampuni ya Aggrey and Clifford, Rashid Tenga alielezea machache mbele ya wageni na waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo juu ya huduma mpya ya matangazo katika bara la Afrika utakaowanufaisha watangazaji, wasanii na watu maarufu uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel na Kulia ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara wa Binary, Eni Kihedu.  PICHA ZOTE NA CATHBERT KAJUNA WA KAJUNASON BLOG. Katibu Mkuu wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabrielakimsifia Wema Sepetu jinsi ambavyo amekuwa akilitunza jina lake. Msanii Diamond Platinuz akitoa shukrani zake za pekee kwa niaba ya wasanii walihudhuria ha