Posts

Showing posts from January 19, 2016

WATU WAWILI WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA BAADA YA KUKUTWA WAKIWA NA DAWA ZA KULEVYA

Image
Madawa ya kulevya yaliyokamatwa mkoani Mbeya. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA.   TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 19.01.2016. KATIKA TUKIO LA KWANZA, MWANAMKE MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA NURU ISMAIL [31] MFANYABIASHARA NA MKAZI WA JIJINI DAR ES SALAAM ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BHANGI UZITO KILO 7 NA GRAMU 100 ZIKIWA ZIMEHIFADHIWA KWENYE MABEGI YA NGUO. MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 18.01.2016 MAJIRA YA SAA 05:30 ASUBUHI HUKO CUSTOM MPAKANI MWA TANZANIA NA ZAMBIA KATIKA MJI MDOGO WA TUNDUMA, WILAYA YA MOMBA, MKOA WA MBEYA. AIDHA MTUHUMIWA ALIKAMATWA AKIWA SAFARINI AKITOKEA SOUTH AFRIKA KUELEKEA JIJINI DSM AKIWA NA PASSPORT NO. AB.767234 ILIYOTOLEWA DSM TAREHE 21/10/2015 NA KUSAFIRI KWENYE BASI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.595 BPR MALI YA KAMPUNI YA FALCON IKITOKEA LUSAKA KU

Breaking News: Ghorofa Latitita Kariakoo, Dar

Image
WANANCHI waishio maeneo ya Mtaa wa Mchikichini na Livingstone, Kariakoo jijini Dar es Salaam, wamekumbwa na taharuki baada ya ghorofa linalojengwa eneo hilo kutitia leo. Chanzo: ITV

MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU LETICIA NYERERE NCHINI MAREKANI.

Image
Misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki kutok kila kona ya Marekani. Mwili wa marehemu Leticia Nyerere unatarajia kufika Tanzania kesho Jumanne January 19, 2016 na utaagwa Dar es Salaam na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika Butiana. Picha na Iska Jojo. Wana familia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Kutoka kushoto ni Bi. Kijogoo kutoka Arizona,,Margareth Mageni na ,Flora Mageni Wanafamilia wakiwemo watoto wa marehemu kutoka kushoto ni Julius Nyerere, Helena Nyerere na Julia Nyerere kulia ni Edlaila  Nyerere ambaye ni wifi wa marehemu kutoka Atlanta jimbo la Georgia nchini Marekani  wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa mama yao Leticia Nyerere aliyeaga Dunia siku ya Jumapili Jan