Posts

Showing posts from July 31, 2017

WEMA: NISIPOPATA MTOTO NAFUNGA KIZAZI

Image
Wema Abraham Isac Sepetu. Exclusive! Hapo nyuma kumepita matukio mengi yaliyomhusu staa mwenye jina lake kwenye tasnia ya sinema za Kibongo, Wema Abraham Isac Sepetu , lakini mwenyewe hakuwa tayari kufungua kinywa kutoa ufafanuzi na hisia zake. Ni kupitia Ijumaa Wikienda ambalo limethubutu kufanya naye mahojiano maalum ambayo ndani yake alifunguka mambo mazito kuhusu maisha yake ya sasa na kuelezea dhamira yake ya kutaka kufunga kizazi endapo safari hii hatajaliwa kupata mtoto baada ya kupata mpenzi mpya. NYUMBANI UNUNIO Katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Wema, Ununio jijini Dar, staa huyo ambaye ni Miss Tanzania 2006/07, aliweka wazi mambo ambayo watu wamekuwa wakiyasema bila mpangilio wala kusikia kauli yake. UNGANA NA WEMA Ijumaa Wikienda: Mambo vipi Wema? Ni muda mrefu sana mashabiki wako hawajakusikia. Je, ni kwa nini umeamua kuwa kimya kiasi hicho? Wema: Sasa hivi nimebadilisha ratiba nzima ya maisha yangu. Kuna vitu ambavyo

Mwana FA: Kuoa mapema kuna faida kubwa

Image
Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hip, Mwana FA amedai amegundua kuoa mapema kuna faida nyingi ambapo amedai humfanya mtu atulie na kuanza kufocus katika maisha mapema. Rapa huyo ambaye aliingia kwenye maisha ya ndoa mwaka mmoja uliopita, amesema ni kweli msanii akioa anatakiwa kubadiika kutoka katika mfumo wa maisha yake ya kawaida ili kuendana na mfumo mpya wa maisha ndani ya ndoa.

Mbunge Aliyeondolewa CUF Azuiwa Kuingia Kwenye Kikao cha Madiwani

Image
Salma Mwasa . Mbunge wa Viti Maalumu ( CUF ) aliyevuliwa ubunge hivi karibuni Salma Mwasa amesikitishwa na kitendo cha askari wa Manispaa ya Ubungo cha kutaka kumzuia asikanyage kwenye halmashauri hiyo. Mwasa ni miongoni mwa wabunge kumi waliovuliwa uanachama sanjari na madiwani wawili wa CUF kwa madai ya kukihujumu chama hicho, hali iliyosababisha kukosa fursa za kuwa wabunge. Akisimulia tukio hilo lililotokea leo Jumatatu, Julai 31, Mwasa amesema aliitwa na askari hao na kuambiwa hatakiwi kuonekana katika eneo hilo la manispaa na kwamba, hiyo ni amri kutoka juu kwa wakubwa. “Mimi ninachojua amri zipo kumi tu, sasa hiyo 11 inatoka wapi? Lakini niliwaeleza kwamba mimi ni mkazi wa Ubungo sasa mnaponizuia nisije hapa hamnitendei haki kwa sababu nakuja kufanya mahitaji mbalimbali,” amesema.   “Mimi nimekuja kama mwananchi wa kawaida. Naomba umma utambue mimi bado ni mbunge hapa nilipo nina barua ya uteuzi na sina barua ya utenguzi,” anasema Mwasa. Hata hiv

MAJADILIANO SERIKALI NA BARRICK GOLD YAANZA RASMI

Image
Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi (wa pili kulia) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa na Rais. John  Magufuli kujadiliana na uongozi wa Barrick Gold Corporation akiwa na ujumbe wa kampuni hiyo kabla ya kuanza  mazungumzo hayo leo  jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU Majadiliano kati ya kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli na wawakilishi kutoka kampuni ya Barrick Gold Corporation kuhusu madini yanayochimbwa  na kampuni hiyo nchini yameanza leo, Julai 31 jijini Dar es Salaam. Prof. Kabudi akiwaelekeza jambo. Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa,  imesema kamati ya Tanzania inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi na kamati kutoka Barrick inaongozwa na Ofisa Mwendeshaji Mkuu, Richard Williams. Prof. Kabudi akiwa na wageni hao. Profesa Kabudi amekaririwa katika taarifa hiyo akisema wamejipanga vizuri kujadiliana na Barrick juu ya

CHADEMA Yalia na Ugumu wa Maisha kwa Wananchi

Image
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema Serikali imeshindwa kusimamia mfumuko wa bei ya chakula nchini kwa sababu haitambui umuhimu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA). Mbowe amesema mwakà 2015, NFRA ilihifadhi tani 446,000 za chakula lakini kufikia mwaka huu wakala huyo amehifadhi tani 74,826 za chakula. Mbowe amesema chakula kinapanda bei kwa sababu hakuna mkakati wowote wa Serikali kuwainua wakulima kwa kuwapatia pembejeo za kilimo. "Usalama wa taifa ni usalama wa chakula, kama hakuna usalama wa chakula hakuna usalama wa Taifa. "Mtakubaliana na mimi kuwa kwa miaka hii miwili vitu vimepanda bei lakini kipato cha wananchi hakijaongezeka "Bei ya mahindi kwa mwakà 2015 ilikuwa ndogo lakini mwaka huu imefika zaidi ya 90,000. Wananchi wanapata shida kwa sababu Serikali yao imewatupa wakulima." Amesema Mbowe