Posts

Showing posts from December 20, 2013

FIFA WAMETIA BARAKA OKWI KUUZWA YANGA

Image
The Acting Competitions Director of the Uganda FA, Decolas Kiiza, has clarified that FIFA cleared striker Emmanuel Okwi to join Tanzanian league champs Young Africans FC. (HM) "Yes we wrote to FIFA and they said the player was free to transfer," Kiiza told MTNFootball.com. Early this week the FA's Chief Executive Officer, Edgar Watson, said they had contacted FIFA to get more clarification on the issue. Young Africans signed Okwi early this week on a two-year deal and yet FIFA had provisionally released the player to join local side SC Villa from Tunisia's Etoile du Sahel. But Okwi's former team, Simba SC in Tanzania, is also unhappy that the Tunisian giants did not pay the full transfer package when Okwi moved early this year. Okwi is expected to fly out to Dar es Salaam on Friday

ANGALIA PICHA ASKARI WAMPA KIPONDO DEREVA DALADALA

Image
Polisi akimpa kichapo dereva daladala. WAKAZI  wa  mjini hapa wamekilaani kitendo cha askari wa kituo kikuu cha polisi baada ya kumpa kipondo na kumkwida hadi kumvua nguo hadharani dereva wa daladala aliyefahamika kwa jina la Bello.Tukio hilo lililojaza umati wa watu lililoshuhudiwa na paparazi wetu lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya stendi ya daladala mjini hapa.Mashuhuda wa tukio hilo walisema Bello aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Hiace inayofanya safari zake kati ya Mjini na Mazimbu, alikamatwa kwa kudaiwa kuegesha gari vibaya. “Stendi ni ndogo Bello aliegesha gari lake akisubiri foleni yake ili apakie, cha ajabu askari akafika na kumpa kibano kabla ya kumsweka ndani,” alisema Wamaga Juma na kuongeza: Kutokana na kichapo kutoka kwa polisi, nguo za dereva daladala zilivuka. “Wananchi wenye hasira walitaka kumzingua askari yule, akapiga simu na kuwaita wenzake wa kikosi cha usalama barabarani, walipofika walimbeba Bello na kumpeleka ki

AJIMWAGIA PETROLI NA KUJIWASHA MOTO MBELE YA KANISA

Image
Mtu huyo mara baada ya kuokolewa na wasamaria. Mwanaume mmoja amejimwagia petroli na kisha kujilipua moto nje ya Kanisa Kuu la Mt. Petro mjini Vatican mapema jana asubuhi, maofisa walisema. Sababu za hatua hiyo binafsi bado haijafahamika, isipikuwa tu kwamba mtu huyo ambaye hakutajwa jina alikuwa amebeba kipande cha karatasi chenye namba ya simu ya binti yake. Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 51 alikuwa akiungua moto kwenye eneo hilo ndipo padri Myahudi alipokimbilia kwenda kumsaidia kuzima moto huo kwa kutumia jaketi. Padri huyo baadaye aliungana na maofisa wawili wa polisi ambao walitumia kifaa maalumu cha kukabiliana na moto kuzima moto huo. Mtu huyo ambaue hakutambuliwa alipatiwa matibabu katika hospitali moja ya jirani na kuhamishiwa kwenye hospitali nyingine kubwa zaidi, akiwa na majeraha makubwa ya moto katika sehemu ya juu ya mwili wake. Maofisa hao wa polisi walitibiwa katika hospitali hiyo kutokana na kuvuta moshi mzito na majeraha kwenye mikon

RACHEL ASAKA BWANA WA KULALA NAYE KWA NGUVU

Image
dai kwamba siku hiyo baada ya shoo yao akiwa na Kundi la Kigoma All Stars mjini Nairobi alikuwa akitafuta bwana wa kumpa kampani usiku bila mafanikio. Rachel akijiachia na shabiki wake stejini. Mtandao mmoja wa Kenya wa Standard Digital News uliandika kuwa, siku hiyo baada ya shoo akiwa anazungumza na mapaparazi wa huko binti huyo alisema alikuwa akitaka mtu wa ‘kujivinjari naye’ lakini akafedheheka kwa kumkosa yule wa kumpa furaha ya kimahaba. Rachel akiwa kazini. Ijumaa lilimtafuta Rachel kupitia simu yake ya mkononi kuzungumzia hilo na  alipopatikana alisema: “Mimi kuongea hivyo si kitu cha ajabu kiasi cha kuifanya mitandao ya Kenya inicharukie. Kwani kuna ubaya gani kusema natafuta mtu wa kuniridhisha? Ile ni mbinu tu ya kuwateka mashabiki

MKASA MWANAFUNZI D ABAKWA NA KUPEWA MIMBA

Image
Denti huyo akiwa na mwanaye MWANAFUNZI wa kidato cha tatu katika shule ya Bujingwa, iliyopo Nyakato Mwanza (jina linahifadhiwa), mkazi wa Mabatini jijini Mwanza, alibakwa, kutoroshwa nyumbani kwao na hatimaye kupewa mimba na mtu aliyefahamika kwa jina la Roja (27). Akizungumza  na mtandao wa GPL hivi karibuni jijini Mwanza akiwa hoi kimaisha baada ya kufukuzwa kwa mwanaume huyo, denti huyo ambaye sasa ana mtoto mwenye umri wa miezi saba, alisema baada ya kutoroshwa kwao, mwanaume huyo alimpa mateso mengi, ikiwa ni pamoja na vipigo vya mara kwa mara. Mtuhumiwa aitwaye Roja Akisimulia kwa masikitiko, alidai kuwa Roja alimpa mimba akiwa bado mwanafunzi wa kidato cha tatu mwaka 2012 na kumshawishi atoroke nyumbani kwao ili akaishi naye. Alidai kuwa, usiku wa Desemba 9 mwaka huu, Roja akiwa na baba, alifika nyumbani na kumtaka aondoke mara moja huku akimtupia virago vyake nje ya nyumba bila kujali kuwa na kitoto kichanga. Hati

AMANDA AANIKA USAGAJI WA MASTAA ULIVYO

Image
MSANII wa filamu, Tamrina Poshi ‘Amanda’ amefungukia sababu za baadhi ya mastaa kujiingiza kwenye tabia chafu ya usagaji akidai kuwa, kutendwa na wanaume ndiyo chanzo cha yote. Tamrina Poshi ‘Amanda’. Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Amanda alisema maudhi ambayo baadhi ya mastaa wamekuwa wakiyapata kutoka kwa wapenzi wao waliotokea kuwapenda ndiyo husababisha baadhi yao kuona suluhisho ni kuhamia kwenye usagaji. “Wasanii wanajiingiza huko sababu wanaumizwa na wanaume, wanadhani usagaji ni raha, wanaona hii ni njia sahii ya kujituliza,” alidai Amanda huku akikwepa kujibu swali la kama naye yumo kwenye kundi la wasagaji ama laa.

UPANDAJI NYASI KATIKA KIWANJA CHA WA KUMBUKUMBU YA SOKOINE JIJINI MBEYA WAENDELEA

Image
HII NI HALI YA UWANJA WIKI ILIYOPITA  WATAALAMU WA KICHINA WAKIJADILIANA JAMBO FULANI KUHUSU UWANJA HUO MWALUKA MENEJA WA UWANJA WA SOKOINE AKIONYESHA MAJANI YATAKAYOPANDWA UWANJANI HAPO MWALUKA MENEJA WA UWANJA WA SOKOINE AKIELEZEA JINSI ZOEZI LA UAPANDAJI NYASI UNAVYOENDELEA NA KUAHIDI KUWA ZOEZI HILO LA UPANDAJI NYASI LITAMALIZIKA BAADA YA WIKI MBILI ZIJAZO SINGUNDALI AFISA UTAMADUNI WILAYA YA MBEYA   HII NDIYO HALI HALISI YA UWANJA WASOKOINE KWA SASA NYASI ZINAENDELEA KUPANDWA PICHA NA MBEYA YETU

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATUNUKU SHAHADA ZA UZAMILI WAHITIMU KATIKA TAASISI YA NELSON MANDELA ARUSHA

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal ambae pia ni Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknologia ya Nelson Mandela iliyopo Arusha, akiwa  kwenye maandamano ya wahitimu wa shahada ya uzamili kwenye Mahafali ya kwanza ya Taasisi hiyo iliyofanyika leo Disemba 19-2013.   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal ambae pia ni Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknologia ya Nelson Mandela iliyopo Arusha, akimtunuku Clarence Msafiri mhitimu wa shahada ya uzamili kwenye Mahafali ya kwanza ya Taasisi hiyo iliyofanyika leo Disemba 19-2013.   Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknologia ya Nelson Mandela iliyopo Arusha akimkabidhi zawadi maalum Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal ambae pia ni Mkuu wa Taasisi hiyo kwenye Mahafali ya kwanza ya Taasisi hiyo iliyofanyika leo Disemba 19-2013. Makamu wa Rai

JESHI LA POLISI MKOANI KILIMANARO, LIMEWATIA MBARONI WATU 4 KWA TUHUMA ZA KUSHIRIKI KATIKA MATUKIO MBALI MBALI YA UHALIFU NA UNYANGAJI WAKUTUMIA SILAHA

Image
  Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Koka Moita akionesha Vocha  za mitandao mbalimbali walizokutwa nazo watu hao. Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Koka Moita akionesha  bunduki aina ya Shotgun waliyokutwa nao watu hao.    Vifaa mbalimbali vya kubomolea.   Laptop mbili pia zilikuwa ni miongoni mwa vitu walivyokutwa navyo.   Afisa wa polisi katika ofisi ya kamanda wa polisi  akipanga vitu mbalimbali walivyokutwa navyo watu  hao wanaotuhimiwa kuwa majambazi. ---   Na Dixon Busagaga-Globu ya Jamii Moshi   JESHI la polisi mkoani Kilimanaro, limewatia mbaroni watu 4 kwa tuhuma za kushiriki katika matukio mbali mbali ya uhalifu na unyangaji wakutumia silaha yaliyotokea mkoani hapa. Kaimu kamanda wa jeshi hilo, Koka Moita, alisema jeshi hilo lilifanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa hao baada ya kukamata gari lenye namba za usajili T564 AUW aina ya Grand Mark 2 wenye rangi ya siliva, katika maeneo ya Kiusa Manispaa ya Moshi

DIAMOND ADONDOSHA PATI LA UFUSKA MTUPU .... ONA WATU WALIVYOJIACHIA, VYOMBO NJE NJE

Image
KUFURU ya kufunga mwaka! Dogo anayejua kuzitumia vyema fursa muhimu, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ amefanya yake kwa mara nyingine, safari hii amefanya pati iliyojaa ufuska, Ijumaa linaibumburua.  Burudani zikitolewa na Kundi la Kibao Kata. Msanii huyo kwa ‘kolabo’ ya swahiba wake mkuu ndani ya anga la muziki Bongo, Omari Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ alifanya tukio hilo lililoacha watu midomo wazi mwanzoni mwa wiki hii ndani ya Ukumbi wa Business Park uliopo Kijitonyama, Dar. Pati hiyo ilikuwa ya kumpongeza mtu wake wa karibu katika Wasafi Classic Baby (WCB), Halima Haroun ‘Halima Kimwana’. Halima Kimwana akionyesha baadhi ya manoti aliyotunzwa. FUNUNU ZA PATI Ngoma za masikio ya ‘viranja’ wetu yalinasa fununu za kuwepo kwa kufuru hiyo mapema mwishoni mwa wiki iliyopita na kuanza kuandaa ‘patroo’ maalumu ili kunasa matukio muhimu. SIKIA FUNUNU ZENYEWE Akizungumza na waandishi wetu kwa usiri na sauti ya ‘kimbeya’, mmoja wa rafiki wa Diamond (jina kapu