Posts

Showing posts from June 6, 2017

Wafahamu Wanawake 4,000 Wanaojifunza Kuwa Maninja Iran

Image
 Miongoni mwa wanawake 4,000 wanaochukua mafunzo ya uninja jangwani nchini Iran. WANAWAKE nchini Iran hivi sasa wanajifunza mbinu za wapiganaji wa Ninja kupitia mbinu za Ninjutsu katika klabu ya mafunzo hayo iliyofunguliwa mwaka 1989 iliyopo Jughin, kilomita zipatazo 52 kutoka jiji la Tehran. Mafunzo hayo yanayofanyika jangwani,  yamelenga kuwafanya wanawake hao kuwa ‘kunoichi’, yaani maninja wa kike.  Katika mafunzo yao wanawake hao wanafanya mazoezi ya kupanda na kuruka kutoka katika kuta mbalimbali, kujificha katika milima na kuweza ‘kukata’ shingo ya adui bila kelele yoyote.

Kibiti: Askari Mgambo Auawa kwa Risasi Uvunguni mwa Kitanda

Image
RUFIJI: Mkazi wa Kitongoji cha Kazamoyo, wilayani hapa,  Erick Mwarabu (37) ameuawa kwa kupigwa risasi usiku akiwa nyumbani kwake. Watu wa karibu katika eneo hilo wamesema marehemu huyo aliyekuwa askari mgambo alipigwa risasi tatu akiwa uvunguni mwa kitanda alikokuwa amejificha. Mkazi mmoja wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Simon amesema watu hao wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walivunja mlango wa nyumba yake saa 9.00  usiku kisha kuingia ndani na kutekeleza mauaji hayo. Simon amesema baada ya watu hao  kuingia ndani walipitiliza moja kwa moja hadi kwenye chumba chake ambapo walimkuta mkewe marehemu na kumhoji alipo mumewe. Amesema baada ya kuona mkewe hataji mahali alipo mumewe walianza kumtafuta ndani ya nyumba yake na kufanikiwa kumuona akiwa amejificha uvunguni mwa kitanda ndipo wakamfyetulia risasi na kuondoka. Simon amesema baada ya kutekeleza mauaji hayo hawakuchukua kitu chochote. Mganga mkuu wa kituo cha afya Ikwiriri, Dk Iddy Malin

Yanayojiri Moshi Kwenye Mazishi ya Mzee Ndesamburo

Image
MOSHI, KILIMANJARO: Viongozi wa CHADEMA pamoja na wananchi wakiwasili katika Usharika wa Kiboriloni kwa ajili ya ibada ya kumuombea aliyekuwa Mbunge wa Muda Mrefu wa Moshi Mjini na Muasisi wa chama marehemu Mzee Philemon Ndesamburo. Maandalizi kanisani hapo. Viongozi wa Chadema wakiwa wamejiandaa kuupokea mwili wa marehemu. Kaburi ambamo atazikwa mzee Ndesamburo.

ANGALIA PICHA WACHEZAJI WA ENGLAND WALIVYOPELEKWA KWENYE MAZOEZI YA JESHI

Image
Kawaida ya mazoezi ya mpira wa miguu ni tofauti sana na mazoezi ya Vyombo vya Usalama kwa sababu hata mazoezi ya Vyombo hivyo ni tofauti na ya mpira wa miguu ingawa pia navyo huwa na michezo mbalimbali.Story kubwa iliyonifikia leo June 6, 2017 ni hii ya wachezaji wa Timu ya Taifa la Englandkupelekwa jeshini ambapo unaambiwa wamelekewa kwenye Kambi ya kijeshi kujifunza uzalendo kwa saa 48 wakati wakijiandaa na mechi ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Scotland Jumamosi ijayo.Washuhudie kwenye hizi picha saba ujionee namna Gary Cahill, Harry Kane, Dele Alli,Raheem Sterling na wengine walivyopigishwa matizi ya kijeshi… 

Wolper atoa onyo hili kali

Image
MUIGIZAJI mwenye jina Bongo, Jacqueline Wolper ‘Wolper’ amefunguka kuwa kuna watu wamekuwa wakipiga pesa kwenye mitandao ya kijamiii kwa njia mbalimbali kupitia jina lake jambo ambalo hapendezwi nalo. Akichonga na Uwazi Showbiz, Wolper aliongeza kuwa taarifa juu ya watu hao anazo na anazifanyia kazi, upelelezi wake ukikamilika atawafikisha kwenye vyombo husika ili wakacheze na mkono wa sheria. “Kuna watu mitandaoni wanapiga pesa kupitia jina langu kwa njia mbalimbali ambazo nimeshazifahamu. Sasa mimi nawaonya tu na kuwataka waache mara moja maana dawa yao inachemka jikoni,” alisema Wolper.

RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA ANNA MGHWIRA KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira akila kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakishuhudia tukio hilo Ikulu jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira akila kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira akisaini Hati ya Kiapo cha Udilifu kwa Viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira akizungumza mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira Ikulu jijini Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimpongeza Mkuu wa Mkoa w