MIMBA YA JOKATE KIDOTI YAZUA BALAA,MAZITO YAFICHUKAKUHUSU KIBA
Jokate na mpenzi wake, Alikiba Saleh Na Waandishi wetu Kizaazaa! Kufuatia mwanamitindo nyota Bongo na Miss Tanzania Namba 2, 2006, Jokate Mwegelo āKidotiā kudaiwa kuwa na ujauzito wa Mbongo Fleva, Alikiba Saleh, mazito yameibuka kwa mademu waliowahi kusemekana ni āzilipendwaā wa msanii huyo kusemwa kwamba, hawakuwa na uwezo wa kumzalia, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukudondoshea. Chanzo makini kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa, warembo wanaodaiwa kuwa ni wapenzi wa zamani wa Kiba ni Gift Stanford āGigy Moneyā, Lulu Euggen āAmber Luluā na Sabrina Omar āSabby Angelā kwamba hawakuwa na uwezo wa kuzaa, ndiyo maana hawakuweza kushika ujauzito wa staa huyo na kuishia kuachika tu. MSIKIE HUYU HAPA āWapenzi wa zamani kina Gigy Money, Sabby Angel na Amber Lulu hawakuwa na uwezo wa kuzaa ndiyo maana hawakuwahi kuonekana wakiwa na ujauzito au kusikika kwamba walikuwa na mimba ikaharibika na sasa hivi hawataki hata kusikia habari za ujauzito wa Jokate hivyo tu...