Posts

Showing posts from November 7, 2013

Agness Masogange apiga picha za ufukwe baada ya kutoka gerezani na kuzua gumzo

Image
SIKU chache baada ya kutoka lupango kwa msala wa madawa ya kulevya, ‘video queen grade one’ Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ ametupia picha za utupu mtandaoni.   Agnes Gerald ‘Masogange’ katika pozi. Masogange na mwenzake, Melisa Edward walikamatwa nchini Afrika Kusini Julai 5, mwaka huu wakidhaniwa kuwa na madawa haramu ya kulevya na baadaye mahakama kuu ya nchini humo ikawaachia kwa dhamana ikidai unga waliokutwa nao si madawa ya kulevya bali ni mali ghafi zijulikanazo kama Methamphetamine.   Baada ya kuachiwa huru, Masogange anayesifika kwa kuwa na figa matata, alitupia picha hizo katika mtandao wa Instagram akiwa amevalia sidiria na nguo ya ndani pekee hali iliyowafanya wafuasi wa mtandao huo wamshangae huku wengi wakimlaumu kuwa alichokifanya hakifanani na maadili ya Mtanzania. “Sasa huu upuuzi gani unatuwekea humu, kwani kila kitu unachofanya ni lazima sisi tuone? Hivi kwa nini mastaa wa Bongo wanapenda kujirahisi kiasi hiki?” alihoji mm

Blundering hunter leaves deer wandering with an arrow through its head

Image
'Shocked': Susan Darrah said she took this photo of a deer impaled by an arrow in her New Jersey back yard This horrifying picture was taken of a deer that wandered into a New Jersey garden. This deer with an arrow shot cleanly through its head was spotted and photographed by resident Susan Darrah.She says she was shocked to see the deer at her home in Boonton with a dart wedged through its muzzle. 'Want to know what sucks? THIS!' She posted on her Facebook page, 'Tried to capture him to no avail... he can eat, run and there's no blood, less chance of infection. I just feel so bad for him.' The animal wasn't bleeding and didn't appear to be frightened, she claimed. Ms Darrah immediately contacted animal control and they turned up the same day but were unable to catch the animal. She said the deer was a regular visitor to her back garden. Read mo

PITIA MEZA YA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 07.11.2013

Image
PI MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI MAGAZETI YA UDAKU LEO  

RAIS KIKWETE KUHUTUBIA BUNGE LEO

Image
Rais Jakaya Kikwete, leoo anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Habari zilizopatikana Mjini Dodoma jana na kuthibitishwa na uongozi wa Bunge pamoja na Ikulu, Dar es Salaam zinasema atahutubia mchana. Kutokana na ujio huo, Serikali imewaelekeza Mawaziri na Manaibu Waziri kutotoka nje ya Dodoma hadi hapo Rais atakapokuwa amehutubia Bunge. Kadhalika safari zote za Kamati za Bunge ambazo zilikuwa katika mchakato wa kutekelezwa zimeahirishwa hadi baada ya leo, ili kutoa fursa kwa wabunge wote kuwapo wakati wa hotuba hiyo. Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana kuwa hata yeye amesikia taarifa kuwa Rais atazungumza bungeni lakini hajui atazungumza kitu gani... "Hata mimi nimesikia kuwa atazungumza lakini sijui atazungumza jambo gani kwa kuwa siyo miongoni mwa watu wanaomwandalia hotuba," alisema Balozi Sefue. Kadhalika, Mkurugenzi w

Watu 35 wakamatwa baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya waandishi wa habari wawili ya RFI mjini Kidal kakazini mwa Mali

Image
Na Ali Bilali Operesheni maalumu ya jeshi la Mali na vikosi vya Ufaransa nchini Mali, imefanikisha kukamatwa kwa watu zaidi ya 35 wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji ya waandishi wawili wa habari rais wa Ufaransa, Ghislaine Dupont na Claude Verlon waliouawa mwishni mwa juma mjini Kidal.  Kukamatwa kwa watu hawa kunakuja saa chache baada ya kuwasili kwa miili ya waandishi wa habari jijini Paris tayari kwa taratibu nyingine za mazishi. Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keita wakati akitoa heshima zake za mwisho kabla ya kusafirishwa kwa miili ya waandishi hao, alielezamaskitiko yake na kulaani kundi lililohusika kwenye mauaji yao. Kwa upande wake mkurugenzi anayehusika na masuala ya Afrika kwenye idhaa ya RFI, Yves Rocles amesema kuwa RFI imepoteza watu muhimu kwenye tasnia ya habari lakini amefarijika kwakuwa msiba huu haukuwa wa nchi ya Ufaransa pekee bali kwa dunia. Katika hatuwa nyingine, serikali ya Ufaransa imesema kuwa imepel

AUWAWA KWA KUCHOMWA MOTO KWA WIZI WA PIKIPIKI MBALIZI MBEYA

Image
Wananchi wakishuhudia  mwili wa mtu aliyetuhumiwa kuiba pikipiki ukiteketea kwa moto Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtakuja Mbalizi Mbeya vijijini, Ambonisye Masinga mwenye koti wakiwa eneo la tukio Polisi wakiondoka na mwili wa marehemu MTU mmoja asiyefahamika jina wala makazi yake, amepoteza maisha baada ya kupigwa na kuchomwa moto na wananchi ambao wameamua kujichukulia sheria mkononi. Wananchi hao ambao ni wakazi wa eneo la Mtakuja Mbalizi, walifanya tukio hilo jana majira ya saa mbili asubuhi. Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtakuja Mbalizi Mbeya vijijini, Ambonisye Masinga, alisema kuwa  marehemu huyo alidaiwa kuiba pikipiki  eneo la Utengule. Alisema, baadhi ya madereva wa bodaboda(pikipiki) walianzisha msako na kufanikiwa kumtia nguvuni marehemu huyo na kuanza kumshushia kipigo huku mwili wake ukiwa umefungwa kwenye pikipiki na kuuburuza barabarani umbali wa kilomita moja. Alisema, mwili huo uliburuzwa na kufikish

MKUTANO WA KIMATAIFA WA ADHABU MBADALA YA KIFUNGO GEREZANI WAFUNGULIWA DAR ES SALAAM

Image
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi, akiisoma hotuba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi ambaye alimuakilisha katika mkutano wa siku tatu wa masuala wa adhabu mbadala wa kifungo gerezani unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Holiday Inn, jijini Dar es Salaam. Watatu kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo uliojumusiha nchi ya Ethiopia, Kenya, Malawi, Rwanda, Afrika Kusini, Sudani ya Kusini, Uganda, Zambia, Zimbabwe na wenyeji Tanzania. Kulia ni Jaji wa Mahakama Kuu nchini, Shabani Lila na Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Jamii, Fidelis Mboya. Mkutano huo umeandaliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Huduma kwa Jamii, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na Maboresho ya Sheria za Adhabu la Penal Reform International. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Wacheza ngoma wa

Mbunge wa CHADEMA afutiwa dhamana na kutupwa selo kwa siku 14

Image
  DHAMANA ya  mbunge wa  jimbo la Ukerewe, Salvatory Machemli (CHADEMA) imefutwa na ameamuriwa na mahakama kwenda rumande  siku 14 kwa kuwa wadhamini wake wamekosa sifa baada ya mshitakiwa na wadhamini wake watatu kushindwa kufika mahakamani ili kuwezesha kesi ya  uchochezi  inayomkabili kusikilizwa kama ilivyopangwa.   Pia, Mbunge huyo ametakiwa  kuwasilisha  vitambulisho vyake katika kituo cha polisi na amezuiliwa kutoka nje ya wilaya  bila  kibali cha mahakama.    Hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo Faustine Kishenyi alitoa uamuzi huo jana baada ya upande wa mashitaka kuomba mshitakiwa afutiwe dhamana.  Wadhamini ambao ni Shellifu Ngelezya, Max Mhogo na Konsolata Machemli wamepoteza sifa hivyo udhamini wao umefutwa. Mwendesha mashitaka wa jeshi la  polisi, Inspekta   Samweli Onyango  amesema mshitakiwa kwa makusudi  ameshindwa kufika mahakani  zaidi ya mara tano bila kutoa taarifa wakati  kesi yake  ikitajwa. Mwishoni mwa mwezi  uliopita, h

WADAU WA MFUKO WA BIMA YA AFYA MKOA WA NJOMBE WATAKA KUWEPO KWA UTARATIBU WA KUUNGANISHWA KTK MFUKO HUO

Image
Kaimu Mkurugenzi mkuu  wa NHIF Hamisi Mdee akitoa taarifa ya Utekelezaji ya kuanzia 2001 hadi June 2013, Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF Balozi Ali  Mchumo akitoa salamu za NHIF kwa washiriki wa mkutano Meneja uendeshaji wa NHIF, Salome Manyama akiwasilisha mada katika mkutano huo, picha ya tano wadau wa mkoa a Njombe wakifuatilia mada.. Na FrancisGodwin Blog Njembe Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Njombe, wameushauri kuwepo kwa utaratibu wa kuunganisha huduma za Mfuko huo na ule wa Afya ya Jamii (CHF) ili kuondoa dhana ya ubaguzi katika ugawaji wa dawa kwenye vituo vya matibabu. Ushauri huo umetolewa mjini Njombe katika mkutano wa wadau wa NHIF wa mkoani humo. Kukosekana kwa dawa kwa wanachama wa CHF wakati wale wa NHIF wanapata dawa hizo kumeonekana Kuwa Kero kwa Wananchi Wengi Mkoani Njombe Katika Mpango wa Kujiunga na Mifuko Hiyo Hali Inayopelekea Wanachi Wengi kusita Kujiunga na Mifuko Hiyo. Akizungumza Wakati wa Kufu