Posts

Showing posts from March 29, 2018

Nafasi za Kazi 30 Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma

Image
Mkurugenzi  wa Halmashauri  ya Manispaa ya Dodoma , kupitia kibali cha Ajira anapenda kuwatangazia wananchi wote wa Tanzania wenye sifa za kuajiliwa katika Utumishi wa Umma kuleta maombi ya kazi kwa nafasi ya Mtendaji wa Kijiji kama ifuatavyo

Madhara ya kujichubua

Image
Katika baadhi ya sehemu duniani watu wanaamini kuwa ngozi angavu huashiria uzuri, utajiri na uwezo(kifedha) alionao mtu.Katika baadhi ya sehemu watu wenye ngozi nyeusi huchukuliwa kuwa wapo chini ya kiwango, hii hupelekea watu hawa kutumia ving´arisha ngozi kama krimu, vidonge au nyenzo zingine kubadilisha ngozi zao.  Tafiti zinaonyesha kwamba wavulana na wasichana hupendelea kutumia bidhaa zinazong´arisha ngozi ili waweze kupata hadhi nzuri katika kundi la familia zao, na jamii. Kwa kweli,hata matangazo yanayoonyeshwa kwenye televisheni mbalimbali huonyesha kitu hiki. Mambo hayo yote huwa na athari kubwa juu ya mawazo ya vijana wa kiume na wakike ambayo hupelekea kuwafanya wachague chochote wanachomudu kati ya krimu au vidonge. Madhara ya kujichubua ni yapi? Mtu anaeyejichubua anaweza kupata kansa ya ngozi, chunusi, uvimbe katika ngozi, ngozi kuwa nyembamba,Kuongezeka kwa hamu ya kula na uzito,kutokwa na mabaka, pumu, kupata watoto wenye kasoro, kupata ma

MAGAZETI YA LEO 29/3/2018

Image

ANGALIA MAELFU WAMZIKA KIJANA ALIYEDAIWA KUUAWA KWA KIPIGO CHA POLISI

Image
Maelfu ya vijana mbeya wamemsindikiza kwenye makazi ya milele kijana Allen Mapunda (20) aliyekuwa mfanyabiashara wa machungwa mkoani Mbeya anayedaiwa kufariki muda mfupi baada ya kuachiwa na polisi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amesema Jeshi hilo halihusiki kwa namna yoyote na kifo cha Allen ambaye anadaiwa alitoka rumande Machi 25, saa 4 asubuhi na ilipofika saa 12 alifariki dunia. Awali, Mkuu wa Mkoa Mbeya, Amos Makala alimuagiza RPC Mohamed Mpinga kuunda kikosi kazi kitakachochunguza tukio zima lilipolekea kifo cha Allen Mapunda. Amesema kikosi hiko kijumuishe wanafamilia na jamii ambayo inamfahamu Allen kisha kumkabidhi ripoti ili hatua zichukuliwe kwa mujibu wa sheria. Kijana Allen Mapunda ambaye alikuwa mkazi wa Kata ya Iyela, anadaiwa alifariki Machi 25, 2018 saa chache baada ya kuachiwa kutoka Kituo Kikuu cha Polisi mkoani Mbeya alipokuwa amekamatwa na jeshi hilo.

NORAH: NAMZIMIA KWELI GABO!

Image
Nuru Nasoro ‘Norah’. MKONGWE wa sinema za Kibongo, Nuru Nasoro ‘Norah’ amesema kati ya waigizaji wa kiume anaowakubali kutoka Bongo Movies ni muigizaji Gabo Zigamba. Norah alifunguka hilo hivi karibuni alipokuwa akipiga stori mbili tatu na mwanahabari wetu ambapo alipoulizwa kuhusu listi ya wasanii wa kiume anaowakubali Bongo, moja kwa moja alianza kwa kumtaja Gabo. Gabo Zigamba. “Wapo wengi ninaowakubali na listi yangu inaongozwa na Gabo namzimia kweli. Wengine ninaowakubali ni JB, Frank Mwikongi, Chiki Mchoma na Dude,” alisema Norah. Alipoulizwa nini kinamvutia zaidi kwa waigizaji hao, alisema ni namna wanavyojua kubadilika kulingana na matakwa ya filamu husika.