Posts

Showing posts from June 20, 2017

WATOTO WA BOSI WA FREEMASON WAFUNGUKA HAYA BAADA YA KIFO CHA BABA YAO

Image
Takriban miezi miwili baada ya kifo cha aliyewahi kuwa Bosi wa Jamii ya Siri (Secret Society) ya Freemason kwa Afrika Mashariki, Jayantilial Andy Chande ‘Sir Chande’, aliyefariki dunia Aprili 7, mwaka huu, watoto wake wawili wamefunguka mazito juu ya jamii hiyo. Kabla ya kupata neno la watoto hao, kufuatia kifo cha Sir Andy, kumekuwa na maswali mengi juu ya nini kinaendelea kwenye jamii hiyo kwa sasa hivyo  Wikienda  lilijipa kazi ya kutafuta majibu ya maswali. NINI KINAENDELEA FREEMASON? Katika nusanusa yake,  Wikienda  lilifika kwenye Hekalu la Freemason lililopo Mtaa wa Sokoine, mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar, jirani na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kutaka kujua kinachoendelea kwa kujigeuza mhitaji wa kujiunga na jamii hiyo. Gazeti hili lilipofika mahali hapo mishale ya mchana, hakukuwa na pilikapilika nyingi zaidi ya mama ntilie aliyekuwa akisubiria wateja wa msosi. Baada ya kuona kimya, ‘pandikizi’ wetu alijari

Kabila Linalohusudu Vitambi Linalotembea Utupu

Image
B AADA ya wiki zaidi ya 20 kukuletea kabila la wala watu lililopo Papua New Guinea, leo tutaanza kukuleta kabila dogo nchini Ethiopia katika Bara la Afrika ambalo ni la ajabu kutokana na vitendo vyao visivyo vya kawaida katika jamii yetu. Naamini utafuatilia habari za kabila hilo kuanzia leo hadi nitakapofika tamati ambapo utakuwa umeelewa mila na desturi za baadhi ya makabila yaliyopo barani Afrika. Kabila hilo kama nilivyosema hapo juu, linaitwa Bodi ama hapa kwetu tungewaita Wabodi lakini pia huitwa Wame’en, jamaa hawa huishi katika Bonde la Omo Kusini mwa Ethiopia na baadhi ya wanaume hutembea uchi wa nyama; wanapofika sehemu zilizostaarabika hushangaza wengi. Kwenye bonde hilo hawapo peke yao kwani kuna makabila mengine mengi madogomadogo arobaini na tano lakini kwa mila na tabia wanafanana na Wabodi japokuwa hao wengine hawana tabia ya kipekee ya Wabodi ya kujinenepesha kwa sababu maalum kama tutakavyoona mbele. Arbore ni moja ya kabila linaloishi katika

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA NIGERIA MHE. OLUSEGUN OBASANJO IKULU DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimlaki Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na  Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsindikiza Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun Obasanjo baada ya kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Juni 20, 201 PICHA NA IKULU

Jaji Mwengine wa Mahakama kuu ajiuzulu

Image
Rais John Magufuli ameridhia ombi la  Kujiuzulu kuwa Jaji wa Mahakama kuu Nchini Mwenda Judith Malecela. Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu inasema Leo Juni 20, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli ameridhia ombi hilo.

Urusi yatoa onyo kali dhidi ya Marekani

Image
Urusi imeonya kuwa itashambulia ndege za muungano unaoongozwa na Marekani nchini Syria iwapo ndege hizo zitapaa katika maeneo ambayo jeshi lake linahudumu. Hii ni baada ya ndege ya kivita ya Marekani kutungua ndege ya kivita ya serikali ya Syria. Muungano huo unaoongozwa na Marekani ulisema ndege yake moja  ilitungua ndege ya Syria aina ya Su-22 baada ya ndege hiyo kuwaangushia mabomu wapiganaji  waasi wanaoungwa mkono na Marekani katika mkoa wa Raqqa, Jumapili. Urusi, mshirika mkuu wa serikali ya Syria, imesema pia kwamba itakatiza mawasiliano yote na Marekani ambayo lengo lake huwa kuzuia ajali angani. Syria imeshutumu shambulio hilo la Marekani na kusema litasababisha "matokeo mabaya sana". "Ndege yoyote, ikiwa ni pamoja na ndege za kawaida na ndege zisizokuwa na rubani ambazo ni za muungano wa kimataifa unaohudumu magharibi mwa mto Euphrates, zitafuatiliwa na majeshi ya kukabiliana na ndege angani na ardhini na zitachukuliwa kama kitu kinacho

Mganga aua, aondoka na kiganja cha mkono

Image
WATU watatu wamefikishwa mahakamani akiwemo mganga wa kienyeji kwa tuhuma za mauaji ya Elizabeth Charles (45), mkazi wa kijiji cha Tambalale kata ya Nsimbo wilayani hapa. Waliofikishwa mahakamani hapo ni Juma Idd(25), Tatu Juma (20) wote wakazi wa kijiji cha Tambalale pamoja na mganga wa kienyeji, Shida Mwanansimbila (54) mkazi wa kijiji cha Kipungulu kata ya puge wilayani Nzega. Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi wilaya, Mengo Kamangala alidai mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi, Ajali Milanzi kuwa Mei 25 mwaka huu majira ya saa 5:00 usiku katika kijiji cha Tambalale Tarafa ya Nsimbo wilaya hapa, washitakiwa wote kwa pamoja walimpiga kisha kumuua na kuondoka na kiganja chake cha mkono wa kulia. Alisema washitakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo kinyume na kifungu 196 kanuni ya adhabu sura ya 16 mapitio ya 2002 inayozuia kutenda makosa kama hayo. Hata hivyo, washitakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shauri hilo

Aliyetaka Kuingiza Simu Gerezani afahamika

Image
DAR ES SALAAM: Kijana mmoja, Ramadhan Nombo, mkazi wa Jiji la Dar jana amenaswa na askari magereza katika Gereza la Mahabusu la Keko akitaka kuingiza simu tano alizokuwa amezificha ndani ya mapande ya nyama yaliyorostiwa. Tukio hilo la ajabu limetokea jana baada ya Nomba kuwapelekea ndugu zake chakula. Kwa mujibu wa chanzo, Nombo alipanga kuingiza simu tano ambazo alizipachika kwenye mapande ya nyama iliyorostiwa kisha kuwapelekea ndugu zake walioko gerezani hapo.  Hata hivyo, haikufahamika alikuwa anawapelekea kwa sababu gani, na wafungwa wa kesi zipi. Mtandao huu ulimtafuta Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza, ASP Lucas Mboje ili kuzungumzia tukio hilo ambapo alikiri kutokea na akaelekeza aonwe Mkuu wa Magereza wa Dar. Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, DCP Augustine Mboje alipoulizwa alisema ni kweli kijana huyo amekamatwa. Kama akikutwa na hatia atakuwa amevunja Kifungu cha 86 (1) cha Sheria za Magereza sura ya 58 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, in

Kauli ya Kubenea Kuhusu Kukamatwa Kwa Meya wa Ubungo

Image
TAARIFA KWA UMMA* NIMEPOKEA kwa masikitiko makubwa taarifa kuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Yakoub amekamatwa na jeshi la polisi kwa amri ya "wanaodai wako madarakani." Kukamatwa kwake kunatokana na hatua yake ya kumpokea Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Pwani, waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye. Mhe. Sumaye alikuwa na ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za Manispaa za Dar es Salaam ambazo ziko chini ya vyama vinavyounda umoja wa UKAWA. Napenda kuufahamisha umma kuwa amri; na au maelekezo yoyote yaliyotolewa iwe na polisi au mkuu wa mkoa ama wilaya juu ya kukamatwa kwa Meya ni batili na haikubariki. Hivyo basi, ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunapigana kufa na kupona kutetea haki za wananchi waliotuchagua na kuhakikisha Meya wetu anakuwa huru kwa gharama yoyote ile. Ninawaomba wanachama, viongozi na wananchi wa jimbo la Ubungo na Kanda ya Pwani kusimama nasi, pamoja na Meya wetu katika kipindi kigumu cha kudai demokrasia ya kweli ndani

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA HAI ASHIKILIWA NA POLISI KWA SAA TANO BAADA YA KUMALIZA KIKAO CHA BARAZA

Image
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ,Helga Mchomvu akieleka kito cha Polisi huku akisindikizwa ana askari Polisi. Mwenyekiti wa Halmahauri ya wilaya ya Hai ,Helga Mchomvu akiingia kituo cha Polisi Bomang'ombe. Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Hela Mchomvu (Kulia) akiingia katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Hai kwa ajili kuongoza kikao cha baraza hilo.Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Yahana Sintoo. Mwenyekiti wa Baraza la Halmashauri ya wilaya ya Hai,Hela Mchomvu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ,Yahana Sintoo wakati wa kikao cha baraza la Madiwani. Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Yohana Sintoo akizungumza wakati wa kikao cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo. Baadhi ya Madiwani wanaounda baraza la Halmashauri ya wilaya ya Hai. Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Helga Mchomvu akizungumza wakati wa kikao cha baraza hilo. Baadhi ya watend