Posts

Showing posts from September 4, 2017

HAMISA MOBETO KUZAA NA BWANAKE… ZARI THE BOSS LADY ATINGA BONGO KUPATA UKWELI

Image
                      Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ . BAADA ya maneno mengi kusemwa Bongo kufuatia madai ya bwana’ke kuzaa na mwanamitindo mwenye jina kubwa, Hamisa Hassan Mobetto, mwanamama mjasiriamali mwenye jina kubwa Afrika Mashariki, Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuendelea kuliamsha dude baada ya kutinga Bongo na kuanza kudodosa ili kupata ukweli wa ishu hiyo. Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni makini, awali Zari alitinga Bongo mapema wiki iliyopita na kupigwa chabo na ‘wadakuz’ AKIWA KATakiwa nyumbani kwa jamaa huyo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva huko Madale jijini Dar. Akiwa katika pozi. Ilidaiwa kwamba, hata hivyo, hakukaa sana kwani aliondoka kwenda kwenye kumbukumbu ya siku 40 za kifo cha mama yake, Halima Hassan nchini Uganda kabla ya kurejea Bongo wikiendi iliyopita.             Kwa taarifa yenu Zari amejaa tele Bongo na lengo lake ni kuchimba na kupata ukweli juu ya madai ya Hamisa kuzaa na bwana’ke.Unajua akiwa

Polisi wamkamata Mtekaji Watoto

Image
POLISI mkoani Geita kwa kushirikiana na wenzao wa Mkoa wa Arusha wamemtia mbaroni mtuhumiwa wa utekaji watoto akiwa na mtoto mwenye umri wa miaka miwili katika nyumba ya kulala wageni ya Shitungulu, Katoro Wilaya na Mkoa Geita aliyekuwa akimshikilia akidai apewe Sh milioni nne. Samson Peter amekamatwa usiku wa kuamkia jana baada ya timu maalumu ya Polisi ya askari tisa, watano kutoka Arusha wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi Amani na wa Geita askari wanne wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi, James, kuizingira nyumba ya wageni aliyokuwa amejificha mtuhumiwa na mtoto aliyemteka tangu Septemba Mosi. Akithibitisha hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema mtuhumiwa alikamatwa saa mbili usiku juzi katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Shitungulu katika Mtaa wa California, Kata ya Katoro wilayani Geita akiwa chumba namba 11 na mtoto huyo Justine Ombeni (2) aliyemteka, akiwa hai na afya njema. Kamanda Mwabulambo alisema mtoto huyo alitekwa Sept