Posts

Showing posts from August 4, 2017

NIMEKUWEKEA VICHEKESHO NILIVYOVISIKIA MTAANI: VUNJA MBAVU!

Image
MWALIMU : Alex, simba akianza kukufukuza utafanya nini? Alex: Nitapanda juu ya mti. Mwalimu: Je, na simba naye akipanda juu ya mti? Alex: Nitakimbilia mtoni niogelee. Mwalimu: Je simba naye akikufuata mtoni? Alex: Mwalimu uko upande wangu au wa simba? Maana sikuelewi kabisa, kila ninavyojaribu kumkwepa simba we unamwelekeza niliko, kama hunipendi sema tu. Kama hukuwahi kupata mia darasani usijali, utapata ukiwa unachaji simu. Ukimpa ‘demu’ hela mzazi wake hata hamuulizi, mpe mimba uone, utatafutwa hadi ‘Google’. Kumbe bangi haina madhara… nimetoka kuvuta pafu moja nipo fresh kabisa bila tatizo..saivi nimekaa juu ya tv naangalia makochi. Dua zenu jamani nipo ugenini nimefumwa naongeza maji ya ugali nijitetee vipi? Nimepika ugali ya watu wawili nikakula ya mtu mmoja nikashiba alafu nikatoka nje nikabisha mlango kama mgeni, nikaingia na nikakula iyo ingine! Mwili haijengwi na mbao. Mnamkumbuka yule Subira aliyekuwa anavuta her

WAZIRI MWAKYEMBE AWAPA ‘DAWA’ WASANII BONGO

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wasanii. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe  amewataka  Wasanii wa Muziki wa Kizazi   kipya  nchini kuanzisha mfuko wa wasanii kwa lengo la kutatua changamoto ya udhamini inayowakabili. Ameyasema hayo  Jijini Dar es Salaam  katika kikao kazi na Wasanii hao ambacho kilijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili na namna ya kukabiliana nazo hivyo kuwataka kutokata tamaa Amesema kuwa kutokana na malalamiko na changamoto mbalimbali zinazowakabili Wasanii, ambazo nyingi zinasababishwa na mikataba inayowanyonya Wasanii katika kazi zao, ni vema sasa Wasanii hao kupitia Chama chao cha Tanzania Urban Music Association (TUMA) kuanzisha mfuko ambao utakua unatoa mikopo kwa Wasanii ili kuwezesha utendaji wa kazi zao pasipo kutegemea wadhamini. Dkt. Mwakyembe akisalimiana na wasanii. “Ninafikiri dawa tunayohitaji ni kuanzishe mfuko wa Wa

Ofisa wa tume ya uchaguzi ya Kenya aliteswa na kunyongwa

Image
Uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa aliyekuwa mkuu wa idara ya Tehama ya tume ya uchaguzi ya Kenya Bw Chris Msando, umeonyesha kuwa aliteswa na kuuawa. Kwa mujibu wa mwanapatholojia mkuu wa serikali Dk Johansen Oduor na daktari wa familia Dk Bessie Byakika, mwili wa Bw Msando umeonesha kuwa wauaji walitumia mikono kumnyonga na pia walimpiga na kitu chenye ncha kali na kumsababishia jeraha. Matokeo ya uchunguzi wa kipatholojia umekuwa ni msingi wa uchunguzi kufuatia kifo chake, na tayari watu watatu wametiwa mbaroni kuhusiana na kifo cha Bw Msando, lakini bado haijulikani walihusika vipi na kifo chake. Mwili wa Bw Msando pamoja na wa msichana mwanafunzi mwenye umri wa miaka 21 uliokotwa jumamosi kwenye msitu wa viunga vya Nairobi.

Sakata la Acacia, Bangi Vyawaweka Matatani Wabunge Wawili wa Mara

Image
John Heche. Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche anashikiliwa na Jeshi la Polisi Tarime, huku Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko naye akisakwa. John Heche amekamatwa na kushikiliwa na Jeshi hilo kwa madai alizungumza bungeni kuhamasisha wananchi kuzuia shughuli za kampuni ya ACACIA huko Nyamongo, North Mara.   Esther Matiko. Jeshi hilo pia linadai Heche kupitia mkutano wa hadhara alisema atapeleka hoja bungeni ili bangi ihalalishwe kuuzwa nje ya nchi, Polisi wanasema kauli hiyo inachochea ulimaji bangi. Halikadhalika linamsaka Esther Matiko ili kumuunganisha katika madai hayo kuwa alizungumza katika mkutano huo kauli zinazochochea kilimo cha bangi. Polisi wamechukua simu za alizokuwa nazo, pia wameagiza simu nyingine iliyopo Dar es salaam kwenye matengenezo pia ipelekwe Tarime. -Makene

RAIS MUSEVENI AWASILI JIJINI TANGA TAYARI KWA SHEREHE ZA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI LA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI HAPO KESHO

Image
  Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akiwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga akiwa ameongozana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (haonekani pichani) na kupokewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa tayari kwa Sherehe za Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi toka Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania utakaofanyika Agosti 5 2017 katika eneo la Chongoleani. Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akiwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga akiwa ameongozana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na kupokewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa tayari kwa Sherehe za Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi toka Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania utakaofanyika Agosti 5 2017 katika eneo la Chongoleani.

HUU NDIO MUONEKANO WA MFANYABIASHARA YUSUPH MANJI LEO MAHAKAMANI

Image
   August 4,2017 Upande wa serikali umewasilisha pingamizi la awali Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga maombi ya dhamana ya mfanyabiashara Yusuf Manji. Pingamizi hilo limewasilishwa leo na wakili wa serikali, Paul Kadushi mbele ya Naibu Msajili, Sian Mustafa kutokana na Jaji Isaya Arufan anayesikiliza maombi hayo kutokuwepo. Katika pingamizi hilo, wakili Kadushi amedai kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi ya dhamana ya Manji. Pia kiapo kilichowasilisha cha kuhusu dhamana kinadosari kisheria, pamoja na kuwepo kwa vifungu visivyo sahihi. Baada ya kuwasilisha pingamizi hilo, Msajili Mustafa ameahirisha kesi hiyo hadi August 7/2017 kwa ajili ya kusikilizwa. millardayo.com  imezinasa picha hizi ambazo zinamuonesha Mfanyabiashara Yusuph Manji akiwa amefuga ndevu ikiwa ni tofauti na ambavyo amekuwa akionekana.                  

Polisi limetangaza Msako mkali kuanzia jumatatu kwa wafanyabiashara wa TV, Simu na Computer “USED”

Image
Jeshi la Polisi kanda maalum Dsm limetangaza Msako mkali kuanzia jumatatu ijayo kwa wafanyabiashara na wauzaji wa television,Computer na simu za Mkononi zilizotumika maarufu Used’ baada ya kubaini katk maduka hayo kumekuwa maficho ya mali zinazoibiwa katika maeneo mbali mbali jijini dsm. Akizungumza na waandishi wa habari jijini dsm Kaimu Kamanda wa Polisi kanda Maalum Dsm Lucas Mkondya amesema katika miezi ya hivi karibu kumeibuka wizi wa Uvunjaji majumbani ambao wahalifu huchuku Tv hasa zile Flat screen ambapo jeshi hilo limebaini hupelekwa katika maduka hayo. Jeshi hilo pia litawakamata watu wote wanaoendesha biashara ya magari yasiokuwa katika yard katika maeneo ya jiji la Dsm. Aidha jeshi hilo pia kuanzia jumatatu litaendesha Msako wa Kukamata magari yote yenye Vioo vyeusi maarufu TINTED baada ya kubaini kuwa baadhi ya wahusika hujihusisha na Uhalifu na Uporaji,kuficha mali za wizi lakini pia kufanyia vitendo visivyofaa vya Uzinzi. Akizungumzia matukio y

Wanaomuua Jini Kabula Wajulikana!

Image
WAKATI hali ya staa wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ikiwa bado si shwari, watu ambao wanatajwa kuzidi kumuweka kwenye wakati mgumu na kumsukumizia kwenye kifo wamejulikana, Ijumaa linakupa habari hii ya kusikitisha. Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Jini Kabula anayedaiwa kuwa na tatizo la kuchanganyikiwa, alisema anashangaa wakati yuko kwenye matatizo hayo mazito ndipo ndugu na marafiki zake wanamtenga, hali ambayo inaweza kukatisha uhai wake. Alisema anapitia kwenye changamoto nzito kimaisha ambapo anahitaji msaada kutoka kwa watu wake wa karibu lakini kinachomsikitisha ni kwamba, anakimbiwa na kupewa kila aina ya jina baya likiwemo la kuitwa kichaa. “Nimeteswa na kuumizwa sana, eti mimi naitwa kichaa, kweli mimi naweza kuwa kichaa, ama kweli hii dunia ni katili sana na kwa hali hii nitakufa. “Naomba ifahamike kwamba nina matatizo makubwa sana, napitia mateso mazito, nimetengwa na watu wananikimbia, hata wale ambao tulikuwa tunasaidiana

KINANA AWASILI TANGA KUSHIRIKI UZINDUZI WA UJENZI WA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA UGANDA

Image
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Henry Shekifu baada ya kuwasli kwenye mkutano wa hadhara wa Rais Dk. John Magufuli uliofanyika katika Wilaya ya Muheza mkoani Tanga, leo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya hiyo Mwanasha Tumbo  Mbunge wa  Viti Maalum mkoa wa Tanga, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Ummy Mwalimu akisalimia wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigela  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Henry Shekifu akisalimia wakati wa mkutano huo  Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akienda jukwaani kusalimia wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Rais Dk Magufuli  Katbu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza alipoalikuwa kuzungumza wakati wa mkutano huo.  Wananchi wakiwa kwenye mkutano huo  Mke wa Rais Mama Janet Magufuli akisalimia kwenye mkutano huo  Rais Dk John Magufuli na viongozi wengine wa meza kuu akiwemo Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahm

HATIMAYE Aliyekuwa MKE wa Mbunge Sugu Faiza Ally Apata Mtoto Mwingine

Image
Leo ipo good news inayomuhusu Faiza Ally baada ya kujifungua salama mtoto. Kupitia Instagram yake leo August 3, 2017 Faiza Ally amethibitisha kuwa amebahatika kujifungua mtoto, akiweka picha ya mtoto huyo na kuweka maneno ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuandika>>>”ALHAMDULILLAH @lijunior_well come to the world baby

CUF Wazichapa Kavukavu Mahakama Kuu ya Tanzania DSM

Image
Wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF) wanaomuunga mkono Mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Msajili wa Vyama, Prof. Ibrahim Lipumba na wanaomuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif, wamezichapa konde Mahakama Kuu Kanda ya Dar leo wakati wa kesi ya wabunge waliofutwa uanachama  Aidha wabunge hao waliiomba mahakama kuzuia utekelezaji wa Uamuzi wa Baraza Kuu la CUF kuwavua uanachama. Kesi hiyo inatarajiwa kutolewa uamuzi leo amahakamani hapo.

Msitumie hati ya kusafiria kama kitambulisho

Image
Idara ya Uhamiaji nchini imewataka wananchi kutambua kuwa paspoti siyo kitambulisho ndani ya nchi na kwamba kisitumike kwa matumizi hayo kwa sababu siyo utaratibu uliopangwa kisheria ndani ya mipaka ya nchi. Pia amesema kuwa ikibainika kuwa mtu amepoteza paspoti hiyo kizembe hatopewa nyingine. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Uhamiaji- Pasi na Uraia, Gerald Kihinga wakati alipofanya mahojiano maalumu na gazeti hili, na kuwaomba wananchi kutambua kuwa paspoti zinazotolewa zinapaswa kutunzwa na kutumika kwa lengo lililokusudiwa la kusafiria nje ya nchi. Kihinga alisema kumekuwa na maombi ya kutengenezewa paspoti baada ya kupotezwa, lakini wengi wamekuwa wakitoa sababu ambazo zinatilia shaka umakini wa mtu kwenye utunzaji wake. “Naomba mfahamu kuwa paspoti pia zinazotolewa siyo vitambulisho ndani ya nchi hivyo visitumike kama vitambulisho na tena si vizuri kutembea nayo kila mahali kama huna safari ya nje ya nchi. Paspoti au hati ya kusafiria z