Posts

Showing posts from June 16, 2018

Messi ataweza Kujibu mabao HAT-TRICK za Ronaldo leo dimbani?

Image
Cristiano Ronaldo jana alifanikiwa kufunga mabao matatu pekee 'Hat-trick' katika mchezo wake wa kwanza wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu dhidi ya Spain nchini Urusi. Mabao hayo yaliisaidia Ureno kwenda sare ya 3-3 dhidi ya mabingwa hao wa Kombe la Dunia kwa mwaka 2010 huko Afrika Kusini. Hattrick hiyo imekuwa ya 51 kwa Ronaldo katika soka la ushindani huku akiifunga akiwa na umri wa miaka 33, moja ya wachezaji wenye umri mkubwa katika mashindano hayo. Rekodi hizo kadhaa za Ronaldo zinamfanya Messi ambaye hajawahi kutwaa ubingwa wa taji hilo kujipanga kwa ajili ya kulipiza mapigo. Mara nyingi wawili hawa wakiwa viwanjani wamekuwa ni watu wa kuvunja na kuandika rekodi za aina yake na kipekee. Messi atakuwa anashuka dimbani kuingoza Argentina kucheza kibarua chake cha kwanza leo dhidi ya Iceland. Pengine anaweza akajibu kwa kufunga pia mabao kama aliyofunga mpinzani wake ingawa huu ni mchezo wa soka mambo yanaweza kuwa tofauti. Tusubiri tuone n

Zitto amsifu Peneza kubadili taswira ya bajeti

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amempongeza Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Kigoma Upendo Peneza (CHADEMA) kuwa amefanikiwa kuacha alama ndani ya bunge la Tanzania akiwa na muda mfupi ndani ya bunge. Zitto ametoa pongezi hizo ambapo amesema Peneza anaingia katika rekodi za Wabunge waliotumia nafasi yao kushawishi jambo lenye faida kubwa kwa jamii na likafanikiwa ikiwa ni baada ya Serikali kutangaza kuondoa kodi ya VAT kwenye Taulo za Kike zinazotumika na Wanawake kipindi cha hedhi. “Kumekuwa na juhudi za kuleta mabadiliko haya miaka mingi kutokana na kazi za Mashirika kama TGNP Mtandao, SNV, Msichana Initiative nk. Upendo, licha ya kuwa na miaka 2 tu Bungeni aliweza kubeba hoja hii na kuiingiza Bungeni na kuunganisha Wabunge wote kutoka Vyama vyote.” ameandika Zitto Ameongeza “Licha ya kwamba kampeni yake ilikuwa ni Watoto wa shule wapewe Taulo hizi bure ( litafika tu hilo kupitia mamlaka za Serikali za Mitaa ), amepata mafanikio

ZARI: Nilikutana na Diamond ‘DM’

Image
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ H AKUNA ufalme unaodumu milele hapa duniani kwa sababu unaambiwa hata ile iliyokuwa ‘kapo’ matata Afrika Mashariki ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ bado hali ni tete. Karibu mpenzi msomaji wa Gazeti la Ijumaa katika safu yetu hii mpya ya The First We Met (Tulivyokutana Siku Siku ya Kwanza) ambapo utawasikia wanandoa mbalimbali wakiwemo mastaa na wasiokuwa mastaa wakielezea namna walivyokutana na kuunda muungano wa kimapenzi. Hii itakupa uzoefu wewe msomaji juu ya namna watu wanavyokutana na kuyajenga maisha. “Bado nakumbuka siku ya kwanza tulipokutana, kila mmoja alikuwa na aibu kumsemesha mwenzake,” hivyo ndivyo alivyoanza kusimulia Zari juu ya namna alivyokutana na Diamond kisha kufurahia maisha kabla ya hivi karibuni jahazi kwenda mrama. Katika mahojiano na kituo kimoja cha redio nchini mwake, Uganda alikozaliwa mwanamama