Posts

Showing posts from February 17, 2015

Gadner alitongoza na kuwashika makalio wanawake mbele yangu – Lady Jaydee

Image
Wiki hii Lady Jaydee amewapa nafasi mashabiki wake kumuuliza maswali naye kuyajibu kupitia akaunti yake ya Instagram. Ameulizwa maswali mengi, na miongoni mwa maswali hayo ni la kuhusu ndoa yake na mtangazaji wa Radio E-FM Gadner G. Habash. Haya ni maswali na majibu kama alivyopost Instagram. Tunasikia umeachana na mume ni kweli au uzushi? JIBU : Hatuja achana niliamua kumuacha   Kwanini umeachana/umemuacha mume? JIBU : Nimemuacha kutokana na kuwa Ndoa inatakiwa iwe na maelewano, furaha, amani na upendo. .. ila kwa bahati mbaya vyote hivyo havikuwepo , sikuwa tayari kuendelea kuishi kwa maumivu huku niki pretend ili kuiridhisha jamii.    Huoni kama umejishushia heshma kuachana na mume? JIBU : Sioni hivyo, ila naona nilikuwa najishushia heshma zaidi kuishi na mume asie na heshma, anaeweza kutongoza na kushika wanawake makalio wakati mi niko jukwaani naimba. Kuwapa mademu magari yangu waendeshe na kuyagonga wakati niko safarini . Ukiachilia

'Magaidi wa Tanga' Watiwa Mbaroni.....Mwili wa Mwanajeshi wa JWTZ Aliyeuawa katika Mapigano hayo Waagwa

Image
Serikali imetoa taarifa rasmi kuhusu uhalifu uliotikisa mkoani Tanga, ikisema hali ni shwari na umma wa Watanzania upuuze taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikitia hofu. Aidha, imesema  watu kadhaa wanashikiliwa wakihusishwa na uhalifu huo.   “Tunawashikilia ila mpaka sasa siwezi kukueleza idadi yao na kwamba ni wa kikundi cha ugaidi au la. Hao watu tunafanya nao mahojiano ili kuweza kuelewa kama wanahusika kwenye tukio hilo,”  alisema Kaimu Kamanda wa Polisi  wa Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki.   Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Ndaki alisema hali katika kitongoji cha Majimoto, Amboni na mkoa wa Tanga kwa ujumla iko shwari. “Tunaendelea kufanya uchunguzi kubaini hao wahalifu pamoja na silaha zilizoibwa,” alisema.   “Tunaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano wao hasa wanapoona watu wenye majeraha au wanaowahisi kwamba ni wahalifu ili nasi tuweze kuwachunguza kama wanahusika kwenye tukio hili”, alisema.   Ingawa Kamanda hak

YAMOTO BAND LIVE KWA MARA YA KWANZA KWENYE JIJI LA LONDON

Image
  YAMOTO BAND   COMFIRMED  will performing all their major hits including NITAJUTA, NISEME, WAMBEA, NITAKUPWELEPWETA and many more @ The Royal Regency Banquet Hall, Sat 21 Feb 2015 From 8pm to 3:30am, there are limited VIP Tables available book yours now for ultimate VIP treatment or individual place your booking early to avoid disappointment. Table bookings please call 07405824696/ WhatsApp +447557304940 info@bongodeejays.com or jestinageorge@gmail.com Ukumbi wa Royal Regency ndio sehemu pekee ambayo utawaona YAMOTO BAND kwenye jiji la LONDON usiku wa 21. Feb 2015 Usiku wa tarehe 21 February 2015 The Royal Regency patakuwa hapatoshi. Kwa kuondosha usumbufu wahi ticket yako mapema  Kiingilio ni: £25 kwa Ticket ya kawaida £35 kwa VIP ticket Kama Unahitaji VIP table for 10 people piga simu  07405824696  kwa maelezo zaidi au tuma email kwenda: info@bongodeejays.com or jestinageorge@gmail.com YAMOTO BAND  will be  alongside supported artist such as Sultan King,

MUUZA MISHIKIKA AKAMATWA NA NYAMA YA PAKA NA KISHA KUSULUBIWA NA WATEJA WAKE

Image
Muuuza mishikaki maarufu Temeke stand ya mabasi anayejulikana kwa jina maarufu la Said mishikaki amekamatwa na nyama ya paka na kisha kusulubiwa na binadamu wenye hasira. Hivi mtu huruhusiwi kuwa na nyama ya paka

Masikini..Kijana Aingizwa Mochwari Akinizaniwa Amekufa

Image
Kijana mmoja, Omary Ramadhani, 28, (pichani) mkazi wa Sinza Madukani, Dar amenusurika kifo baada ya kupata ajali ya kugongwa na ‘Break Down’ alipokuwa akiendesha Bajaj katika makutano ya Barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi, Mwenge, jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwa masikitiko, Omary alisema kuwa alipogongwa na gari hilo hakuweza kujitambua kwani hata wasamaria wema walivyomchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, walijua alifariki dunia hivyo wakamuingiza moja kwa moja mochwari, lakini kwa bahati nzuri alitokea nesi mmoja aliyeshauri asiwekwe kwanza kwenye friji mpaka apimwe. Akiendelea kuzungumza kwa tabu kutokana na maumivu ambayo anayo, Omary alisema baada ya nesi huyo kumpima aligundua alikuwa akipumua kwa shida. Alisema hata ndugu zake walijua ameshafariki dunia kutokana na alivyokuwa, kwani alivunjika mgongo mara sita na mfupa wa mkono ulitoka nje na kupasuka kichwani jambo lililosababisha kuvuja damu nyingi. Al

ANGALIA KINACHOENDELEA TANGA

Image