Posts

Showing posts from January 6, 2017

HUMPHREY POLEPOLE ATOA MSIMAMO WAKEKUHUSU KATIBA MPYA

Image
Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye kwa sasa ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole ameweka wazi msimamo wake kuhusu mchakato wa katiba mpya, na kusema kuwa hajalitelekeza suala hilo. Humphrey Polepole akiwa Kikaangoni Polepole aliyekuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV kupitia facebook.com/eatv.tv, katika mahojiano yake na East Africa Radio amesema kuwa mchakato wa kuipata katiba mpya kwa Tanzania uko kwenye mikono salama chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, na kuwataka watanzania waiache serikali irekebishe kwanza baadhi ya mambo ili mchakato huo utakapoanza usikumbwe na vikwazo. Polepole amesema kwa uzoefu wake kama mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa chini ya Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba, anafahamu mambo ambayo watanzania waliyataka na kwamba mambo hayo ndiyo ambayo yameanza kutekelezwa na serikali ya awamu ya tano ikiwemo kuwa kujali utu, kudhibi

Gigy Money Afunguka Suala la Kuwa Ana Ukimwi, Orodha ya Wanaodaiwa Kutoka Naye Yatajwa

Image
Video queen matata ambaye pia ni mtangazaji wa kituo cha redio moja jijini hapa, Gift Stanford ‘Gigy Money’, ametema cheche akisema kuwa, watu wote wanaomsema kwamba kutokana na kuvaa nusu utupu na kujiachia na midume mbalimbali huenda ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi, waache kwani kama ni kweli basi wengi wangekufa kwa sababu ameshatembea na mastaa kibao Bongo. Gigy Money Akizungumza na gazeti hili juzi, Gigy alisema kwamba amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mastaa mbalimbali wakubwa Bongo akiwemo Mbongo Fleva, Ali Kiba na kudai kuwa, kama kuambukizwa virusi angeanza yeye na wengine wangefuata. “Unajua watu wanashangaza sana. Kama mtu ana virusi vya Ukimwi hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu anayempenda, ningependa watu waache unyanyapaa. Ninachojua mimi sina Ukimwi kwa kuwa nilipima kwa shinikizo la mpenzi wangu wa sasa (Moulad Alpha ‘Moj’) na watu niliotembea nao wanaendelea vizuri tu, wengine wachumba zao wananyonyesha,” alisema Gigy.

Hali si Shwari Wolper na Harmonize….Meseji Aliyopost Wolper Yaonyesha Wameachana

Image
Jacline Wolper ame post hii halaf ghafla kafuta, hii maana yake nini wadau? Jisomee alichoandika kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram:

WAZIRI MKUU AIPONGEZA BIMA YA AFYA KWAJINSI INAVYO SAIDIA KUTOA HUDUMA KATIKA KITUO CHA AFYA CHA MADABA SONGEA

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimjulia hali Sophia Mgeni ambaye ametoka kujifungua mtoto wa kike, Waziri mkuu alitembelea Zahanati ya Madaba iliyopo wilaya ya Songea ili kuwasikiliza wagonjwa katika zahanati hiyo Waziri mkuu yupo Mkoani Ruvuma kwa ziara ya kukagua shughuli za maendeleo  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wauguzi wa zahanati ya Madaba huku akiwataka waendelee na moyo waliokuwa nao wa kuwapenda wagonjwa na kuwahudumia, kwani serekali inatambua mchango wao wanaoutoa kwa taifa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwahutubia wananchi wa madaba waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza,Waziri Mkuu alitumia nafasi hiyo kuwaelezaa Wananchi hao juhudi za serekali za kuwasaidia katika sekta mbali mbali ikiwemo Huduma ya bima ya afya. Waziri mkuu yupo mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi.Picha na Chris Mfinanga