Posts

Showing posts from January 28, 2017

Ten(10)Foolish Things to Say or Not to Say When Texting Boys

Image
We live at a time when most of our daily interactions happen through texts. That’s right, we rarely even call people anymore. We just text everyone. So it’s not surprising that a lot of our dating and flirting also happens through text. When you give a guy your phone number you don’t even expect him to call, you know he’ll text. It takes a bit of the pressure off, since you don’t have to speak your mind immediately, you can take your time and write out a perfect response. But texting boys can be tricky, there’s a balance you have to strike. That’s why we compiled a couple of pointers to help you figure out what you should and shouldn’t say when texting boys. 1. You never want to come off as clingy when texting a new boy . It might be a good idea to avoid texts like “I miss you”, and instead text him something like “ Wait till you see what I’m wearing” or “I can’t wait to take you home” . This way you’ll keep him interested and he’ll know you’re thinking of him.

Mwanamke Asimulia Alivyokuwa Akimshushia Kipigo Mumewe kwa Miaka 30 Mfululizo

Image
Mara nyingi vitendo vya ukatili na unyanyasaji kijinsia vimezoeleka kufanywa na wanaume dhidi ya wanawake na watoto. Hata hivyo, kampeni ya “Tunaweza” inayoratibiwa na shirika lisilo la kiserikali la Kivulini jijini Mwanza kwa lengo la kutokomeza ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, imebaini kuwa vitendo hivyo pia hufanyika dhidi ya wanaume. Mkazi wa Mtaa wa Mwananchi, Kata ya Mahina jijini Mwanza, Ernest Kibinzaroya (78) ni mfano wa ukatili unaofanywa na wanawake dhidi ya wanaume. Yeye pamoja na mkewe, Maria Kibinzaroya (57) wamejitokeza hadharani kueleza walivyopitia maisha hayo. Inaelezwa kwamba Maria alikuwa akimpa kipigo cha mara kwa mara mumewe kabla ya ‘kuokoka’ na kuwa mke mwema. ‘Wokovu’ huo ni baada ya kampeni hiyo inayofanyika katika wilaya za Ilemela, Nyamagana, Magu, Misungwi, Sengerema mkoani Mwanza kuwafikia wanadoa hao na wote hivi sasa wana mabadiliko na wanapiga vita ukatili na unyanyasaji wa kijinsia. Akizungumza mbele ya mumewe wakati wa mahoji

BREAKING NEWS : KIONGOZI WA WALINZI WA IKULU YA GAMBIA ATOROKA

Image
Kamanda wa Polisi wa Jeshini (MP) katika ikulu ya Gambia, Luteni Nuha William Jammeh, yasemekana yupo mafichoni. Inasemekana alitoroka Gambia siku chache zilizopita. Kamanda huyu alitoa amri ya kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa jeshi la nchi hiyo walioonekana kumpinga Rais aliyemaliza muda wake, Yahya Jammeh. Kwa sasa Luteni Nuha Jammeh hajulikani alipo. Amekimbia mji mkuu wa Banjul na inaaminika kuwa amekimbilia nchini Senegal. Namba yake rasmi ya simu inayojulikana inaonesha kuwa yupo nchini Senegal ingawa simu yake imezimwa. Akimzungumzia Nuha Jammeh, mtu aliyewahi kusoma nae darasa moja alisema: ” Alikuwa mkimya sana na anayependa sana dini. Ilikuwa ni rahisi sana kuzoeana naye kipindi kile. Baada ya kukutana na Yahya Jammeh, huwezi jua, kwa maana yule dikteta alikuwa na uwezo wa kugeuza watu wazuri kabisa kuwa mashetani.”

KIPIGO CHA WANAJESHI CHA SABABISHA KIFO CHA KONDA WA DALADALA TANGA

Image
Kondakta wa daladala linalofanya safari zake kati ya Nguvumali hadi Raskozone, Salim Kassim amefariki dunia baada ya kudaiwa kushambuliwa ndani ya kambi ya jeshi jijini hapa. Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, kondakta huyo alikufa wakati akipelekwa katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo na chanzo cha kifo bado kinachunguzwa.Mwananchi ilielezwa kuwa tukio hilo lilitokea juzi usiku, ambapo mashuhuda walidai kuona kondakta huyo akichukuliwa na wanajeshi na kuingizwa kambini na baadaye alitolewa akiwa hajitambui Akizungumzia tukio hilo, Khalid Juma mkazi wa Nguvumali jijini hapa alisema askari hao wamekuwa na desturi ya kuwapiga wananchi bila kuchukuliwa hatua zozote za kisheria. “Tumekuwa tukipata vipigo kila wakati, licha ya viongozi kupata taarifa za matukio hayo wamekaa kimya na hili tukio ni la tatu kutokea hapa,” alidai Khalid. Diwani wa Kata ya Nguvumali ambaye pia ni Meya wa Jiji