TAGCO NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZAPONGEZWA KWA UTENDAJI

4 (1)
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza kuhusu namna Halmashuri hiyo ilivyojipanga katika kuimarisha mawasiliano ya kikakati hasa kutangaza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.
1
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando akisisitiza jambo kwa ujumbe wa chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashauri hiyo kukagua na kujionea jinsi maafisa Habari wanavyotekeleza jukumu la kuisemea  Serikali katika Mikoa na Halmashuri zao.
2 (1)
Kiongozi wa Ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza jambo kwa  Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bw. Chiza Marando wakati wa ziara ya ujumbe huo katika Halmashuri hiyo uliolenga kukagua na kuweka mikakati ya pamoja katika kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma.
3 (2)
Mwakilishi wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Casmir Ndambalilo akisisitiza umuhimu wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kuwajibika katika kuisemea Serikali hasa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mikoa na Halmashuri zao, hiyo ilikuwa katika ziara iliyoandaliwa na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) kwa kushirikiana na Idara ya Habari MAELEZO.
Frank Mvungi- MAELEZO, Tunduru
 Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) vimepongezwa kwa kubuni na kuweka utaratibu wa kufuatilia utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini hadi katika ngazi ya Halmashuri.
Akizungumza na Ujumbe wa chama hicho uliofika Ofisini kwake mapema wiki , Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw.  Chiza Marando  amesema kuwa hili ni jambo la kihistoria ambapo ufuatiliaji wa utendaji wa Maafisa Habari unafanyika katika ngazi zote.
“Tangu nimeanza kazi sijawahi kushuhudia ufuatiliaji wa namna hii na sisi tuko tayari wakati wote kutoa ushirikiano utakaosaidia Afisa Habari katika Halmashauri yetu atekeleze majukumu yake vizuri hasa katika kutangaza miradi ya maendeleo” Alisisitiza Marando
Akifafanua Bw.  Marando amesema kuwa Halmashuri yake inatambua umuhimu wa mawasiliano kati ya Serikali na Wananchi hivyo imeweka kipaumbele katika kuwezesha  utoaji wa taarifa za maendeleo kwenda kwa wananchi ili waweze kushiriki katika kujiletea maendeleo.
Kwa  upande wake Kiongozi wa Msafara wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini  (TAGCO) na Idara ya Habari – MAELEZO Bi. Gaudensia  Simwanza amesema kuwa maafisa habari wanalo jukumu kubwa katika Halmashauri na Mikoa katika kutangaza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao.
Aliongeza kuwa  kutokana na jukumu hilo wanapaswa kutumia rasilimali zilizopo kutekeleza jukumu hilo kwa weledi.
Ziara ya Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini na Idara ya Habari MAELEZO inafanyika katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kufuatilia na kuona utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini katika ngazi zote ili kutoa msukumo na kuweka mikakati ya pamoja katika kuimarisha Mawasiliano ya Serikali kwa umma ili kuchochea maendeleo na ustawi wa wananchi.

Comments

Popular posts from this blog