Posts

Showing posts from March 4, 2016

MADHARA YA MATUMIZI YA MIRUNGI KIAFYA

Image
   Mtumiaji wa mirungi yupo katika hatari ya kupata vidonda vya tumbo. - Kupungukiwa msukumo wa kufanya tendo la ndoa (low sex drive) na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu. 2. Ukosefu wa haja kubwa (constipation) 3. Utumiaji wa muda mrefu husababisha ini kushindwa kufanya kazi, pia meno kubadilika rangi, kudhoofika, fizi kuuma na harufu mbaya mdomoni. 4. Upungufu wa usingizi. 5. Humpelekea mlaji kutawaliwa nayo. (addiction) 6. Madhara ambayo bado kinamama walaji Mirungi hawajagundua ni kwamba mtoto anayezaliwa na mama mlaji Mirungi mara nyingi hukataa kunyonya titi la mama yake kwa sababu ladha ya maziwa inabadilika kwa ajili ya utumiaji wa madawa (pesticides) unaotumiwa na wakulima wa Mirungi kama inavyoeleza utafiti uliofanyika na Chuo Kikuu Cha Aden (Aden University). 7. Utafiti mwengine kule Ethiopia unatueleza ya kuwa mtoto wa mama mwenye kula Mirungi kwa wingi huwa hana uzito wa kawaida wakati wa kuz

Rais Magufuli, Kenyatta waweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Arusha

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Tengeru nje kidogo ya Jiji la Arusha mara baada ya kuwasili kwa ajili ya Uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Uganda Yoweri Museveni kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la A

Simba kushuka kijeshi, Kaseja azua hofu Mbeya City

Image
Wachezaji wa Simba wakifanya yao. Nicodemus Jonas, Dar es Salaam BAADA ya kuwa mafichoni kwa takriban wiki moja mkoani Morogoro, kikosi cha Simba sasa kipo fiti, tayari kuwavaa Mbeya City katika mchezo utakaopigwa keshokutwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar. Simba wanashuka dimbani wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 kwenye mzunguko wa kwanza uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya lakini Simba ilikuwa chini ya Muingereza, Dylan Kerr wakati kwa sasa ipo chini ya Mganda, Jackson Mayanja. Meneja wa Simba, Abbas Ally ‘Gazza’ amewahakikishia Wanasimba kuwa kwa mazoezi waliyofanya, wana uhakika wa ushindi. “Kikosi kipo vizuri, bahati nzuri wachezaji karibia wote wapo, isipokuwa Hija Ugando ambaye alibaki Dar akiuguza majeraha, lakini wengine wote wapo kambini katika maandalizi ya mchezo huo,” alisema Gazza. Kipa wa Mbeya City, Juma Kaseja. Aidha, upande wa Mbeya City, kikosi chao kimekuwa kikiwasili Dar kimafungu ambapo kundi moja la wachezaji tayari lilit

KILIMO CHAMKOMBOA MAMA MJANE MWENYE ULEMAVU WA MIGUU BUMBULI WILAYANI LUSHOTO

Image
 Bi. Zaharia Ally (54) akiwa na wajukuu zake nyumbani kwake. Bi. Zaharia Ally ambaye hayupo pichani hutembea umbali wa Kilometa zaidi ya Tatu  kutoka kwake kufika katika eneo hili  kufuata kuni kwa Mahitaji ya Nyumbani ikiwemo kupikia. Eneo hili ni Shamba la Bi. Zaharia Ally kwa ajili ya Kilimo cha Maharagwe na Mahindi Hapa ni Nje ya nyumba ya Bi. Zaharia (Ambaye hayupo pichani) akionesha mzigo wa kuni …………………………………………………………………………………………………….   Na Blogs za Mikoa Tanzania. Kuna haya maneno yanasema kuwa Ardhi ni moyo wa mwanamke katika kujikomboa kimaisha Pamoja na jitihada mbalimbali za kumwendeleza mwanamke katika kujikwamua na umaskini raslimali ya ardhi ndiyo chachu kubwa ya kuwawezesha wanawake kujikwamua na umaskini hapa nchini. Mwanamke mwenye umri wa miaka 54 anaetambulika kwa jina la Zaharia Ally mkazi wa Bumbuli wilayani Lushoto, mkoani Tanga ni miongoni mwa wanawake wanye changamoto za maisha na wanaopambana kujenga familia zao. Mwanamke h

NACTE YAFUNGUA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017 .

Image
Kaimu Katibu Mkuu wa  Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dk. Adolf Rutayuga, (Kulia) akisisitiza jambo wakati alipokuwa ikitangaza wa kuzindua Mfumo wa Udahili wa Pamoja (Central Admission System (CAS)) kwa mafunzo yanayoratibiwa na Baraza kwa mwaka wa masomo wa 2016/17. Mfumu huo, utatumika kuratibu maombi ya kujiunga na mafunzo ya Astashahada (Cheti), Stashahada (Diploma) na Shahada ya kwanza (“Bachelor Degree)   Katikati ni Mkurugenzi Udhibiti Ubora Rasmalimali watu , Edmund Kinwasi na Kaimu Mkurugenzi  Idara ya  Ufuatiliaji  Tathimini na Uthibiti wa baraza hilo , Christina Kumwenda. Uzinduzi huo ulifanyika leo jijini Dar es Salaam.  Kaimu Katibu Mkuu wa  Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dk .Adolf Rutayuga,  akipofya kitufe cha komputa  kuashiria Uzinduzi  rasmi wa Mfumo wa Udahili wa Pamoja (Central Admission System (CAS)) kwa mafunzo yanayoratibiwa na Baraza kwa mwaka wa masomo wa 2016/17. Mfumu huo, utatumika kuratibu maombi ya kuj

DAR ES SALAAM KUWA JIJI LA 12 KWA UCHAFU DUNIANI

Image
This was the world dirty city league table drawn by Forbes: 1. Baku, Azerbaijan 2. Dhaka, Bangladesh 3. Antananarivo, Madagascar 4. Port au Prince, Haiti 5. Mexico City, Mexico 6. Addis Ababa, Ethiopia 7. Mumbai, India 8. Baghdad, Iraq 9. Almaty, Kazakhstan 10. Brazzaville, Congo 11. Ndjamena, Chad 12. Dar es Salaam, Tanzania 13. Bangui, Central African Republic 14. Moscow, Russia 15. Ouagadougou, Burkina Faso 16. Bamako, Mali 17. Pointe Noire, Congo 18. Lome, Togo 19. Conakry, Guinea Republic 20. Nouakchott, Mauritania 21. Niamey, Niger 22. Luanda, Angola 23. Maputo, Mozambique 24. New Delhi, India 25. Port Harcourt, Nigeria

RC DAR ES SALAAM APIGA MARUFUKU UTOAJI WA VIBALI VYA MALORI YA MIZIGO YENYE UZITO WA ZAIDI YA TANI 10 KUINGIA KATIKATI YA JIJI.

Image
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Mecki Sadiki akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Dar es salaam kwenye kikao cha kwanza cha Bodi hiyo kwa mwaka 2016. Kulia ni Zungu Azzan na Kushoto ni Bw. Edward Otieno Kaimu Katibu Tawala wa mkoa huo. Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw.Isaya Mngurumi akichangia jambo kuhusu uboreshaji wa miundombinu ya barabara katika Manispaa yake wakati wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Dar es salaam. Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema akichangia jambo wakati wa wakati wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Dar es salaam kwa mwaka 2016. Baadhi ya Wabunge wa jiji Dar es salaam wakifuatilia kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Dar es salaam. Kutoka kulia ni Mhe. Bonnah Kalua – Mbunge wa Segerea, Mhe. Faustine Ndugulile – Mbunge wa Kigamboni, Mhe. Zungu Azzan – Mbunge wa Ilala na Mhe. Abdallah Mtolea – Mbunge wa Temeke. Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Dar es salaam Muhandisi J

Balaa Jipya Makalio ya Kichina

Image
Stori: Hamida Hassan na Boniface Ngumije D ar es Salaam: Tabia ya baadhi ya wasichana hasa wa mjini kuwa na tamaa ya kuwa na makalio makubwa na hivyo kulazimika kutumia dawa mbalimbali, imekuwa ikishamiri kila siku licha ya serikali kupiga marufuku uingizwaji wa dawa hizo.   Jayjay Gazeti hili matoleo yaliyopita liliwahi kuandika jinsi mastaa wengi Bongo wanavyotumia dawa hizo lakini uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, kasi ya matumizi ya dawa hizo yamekuwa yakishamiri huku waathirika wengi wakijiuguza kwa siri baada ya kupata madhara. Gilla . Katika tukio jipya la hivi karibuni, mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Hamisa ambaye alidai ni mke wa mtu alisema kuwa, alishawishiwa na rafiki yake kutumia dawa hizo ili naye awe na ‘zigo’ lakini ameanza kuona zinamletea matatizo. “Nimekuwa nikisikia kuwa dawa hizi zina madhara lakini kuna rafiki yangu mmoja ambaye aliwahi kutumia na yuko poa ndiye aliyenipeleka kwenye duka moja lililopo Ki

Jack: Wakwe mnisamehe kwa uvaaji wangu

Image
Na Imelda Mtema Mrembo ambaye ni zao la Maisha Plus, Jacqueline Dustan amefunguka kuwa wakati akielekea kufunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi, kwa upande wa nguo fupi wakwe zake wamsamehe kwani hataacha. Jack alisema kuwa anaipenda ndoa ila linapokuja suala la kuvaa mavazi ya nusu utupu wakweze wasimmaindi kwani ameshazoea kujiachia. “Uvaaji wangu unajulikana, eti nibadilike maana naolewa, hee..mniache na hao wakwe wanizoee kwa hilo,” alisema Jack.

Hivi ndivyo raha na hasira vinavyoweza kukupa madhara kwenye moyo na kuwa ugonjwa

Image
Msongo wa mawazo ambao husababisha maumivu katika kifua na mtu kushindwa kupumua hutokea wakati wa raha na hasira, huzuni na hofu, utafiti nchini Uswizi umebaini. Robo tatu ya visa vya ugonjwa wa Takotsubo ambao hubadili umbo la moyo na kusababisha kifo hutokana na msongo wa mawazo. Utafiti huo uliofanywa katika hospitali ya Zurich na kuchapishwa katika jarida la moyo barani Ulaya,unasema kuwa kila kisa kimoja kati ya 20 husababishwa na raha. Tatizo hilo huwa ni la mda na watu hurejelea hali yao ya kawaida baadaye. Katika utafiti huo wa wagonjwa 1750,watafiti walibaini matatizo ya moyo yanayosababishwa na: Sherehe ya kuzaliwa Harusi ya mtoto wa kiume Kukutana na rafiki baada ya miaka 50 Kufikia umri wa kuitwa bibi. Timu unayoipenda kushinda mechi. Kushinda bahati nasibu. Utafiti huo pia umesema kuwa visa vingi huwatokea wanawake waliomaliza kuzaa. Daktari Jelena Ghadri,mmoja ya watafiti anasema:Tumebaini kwamba ugonjwa huo unaweza kusababishwa na sababu

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA NA MBUNGE JOSEPH HAULE WAPIGA KAZI PAMOJA MIKUMI

Image
  Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh Mwigulu Nchemba akizungumza mbele ya wakazi wa kata ya Kidodi,kijiji cha Tungu-Mikumi  (hawapo pichani),kwenye mkutano wa kusikiliza na kutoa majibu kuhusu wakulima wa Miwa,pichani shoto ni Mbunge wa Mikumi, Mh Joseph Haule   Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh Mwigulu Nchemba akizungumza jambo na Mbunge wa Mikumi, Mh Joseph Haule katika Mkutano wa kusikiliza na kutoa majibu kuhusu wakulima wa miwa uliofanyika katika  kata ya Kidodi,kijiji cha Tungu-Mikumi . Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh Mwigulu Nchemba akiwa na Mbunge wa Mikumi, Mh Joseph Haule wakifurahia jambo kwa pamoja katika  katika Mkutano wa kusikiliza na kutoa majibu kuhusu wakulima wa miwa uliofanyika katika  kata ya Kidodi,kijiji cha Tungu-Mikumi .

Afya ya Mr. Nice Kuteteleka… Simulizi Yake Inasikitisha

Image
  Hali ya Mkongwe wa Muziki wa Takeu, Lucas Mkenda ‘Mr. Nice’. Stori:  Mwandishi wetu, Ijumaa D AR ES SALAAM: SIKU chache baada ya kusambaa kwa picha yake inayomuonesha akiwa amepungua mwili na kuzua mjadala mitandaoni huku wengi wakimuonea huruma, mkongwe wa Muziki wa Takeu, Lucas Mkenda ‘Mr. Nice’ ameibuka na kufungukia afya yake. Picha inayomuonesha Nice akiwa amepungua mwili ilizagaa mapema wiki hii kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengi waliochangia mjadala wa picha hiyo, walisema staa huyo aliyetikisa kwa utajiri enzi hizo, kwa sasa atakuwa anaumwa sana huku mjadala mkubwa ukawa ni ya lini?   Mr. Nice akiwa katika pozi, enzi zileee. Baada ya Ijumaa kuinasa picha hiyo, lilifanya jitihada za kumpata msanii huyo kwa kumvutia waya alipopatikana, alifunguka kwa kirefu kuhusu afya yake: “Kwanza hiyo picha ni ya kitambo sana. Si unakumbua lile sakata langu la mimi kulishwa sumu kwenye chakula? Basi ndiyo kipindi kile. “Namshukuru Mungu niliiwahi ile s

Madaktari 2 na Wauguzi 4 Wasimamishwa kazi Jijini Mwanza Kwa Kukataa Kumzalisha Mjamzito Ambaye Alijifungua Mapacha Wawili Chooni Wakafariki

Image
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Baraka Konisaga, amemwamuru Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Adam Mgoyi kuwasimamisha kazi madaktari wawili na wauguzi wanne katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana iliyopo Kata ya Butimba kwa kushindwa kumuhudumia mama mjamzito aliyefikishwa hospitalini hapo na kusababisha kujifungua watoto mapacha na baadaye kufariki. Hatua hiyo imesababishwa na tukio la mgonjwa Suzana John (27) mkazi wa Kata ya Mkolani kufikishwa na ndugu zake katika Hospitali hiyo, aliyekuwa mjamzito na kupokelewa na Dk Norin Magesa na Muuguzi, Janet Foya waliokuwa zamu ya usiku siku ya Machi Mosi, mwaka huu majira ya saa 4:00 usiku na kushindwa kumuhudumia zaidi ya kutoa lugha isiyoridhisha, pamoja na uzembe. Akielezea tukio hilo, mwanamke huyo ( Suzan John ) alidai kuwa alianza kusikia uchungu na kuomba msaada kutoka kwa madaktari na wahudumu wa afya waliokuwa hospitalini hapo bila mafanikio.   “Nilifika nikiwa hoi, nikawaambia muda wa

Tungeshangilia Filamu za Bongo Kama Tulivyofanya Kwa Ray na Hadithi yake ya Maji na Weupe Wake, Tungekuwa Mbali

Image
Ray alitengeneza headlines sana hivi karibuni kwa kauli yake kuwa weupe wake umetokana na kunywa maji mengi. Story ilikuwa viral na ilisambaa kwenye mitandao yote. Watu walianza kupost picha wakinywa maji kuutafuta weupe kama wa Ray kama njia ya kumtania kwa kauli yake hiyo. Sikumbuki mara ya mwisho ni lini muigizaji huyu alikuwa gumzo kama hivi. Hadi kuna tetesi kuwa kutokana na kauli yake kusambaa kwa ukubwa usioelezeka, makampuni ya maji yanataka yampe mchongo. Hatua hiyo ilinifanya nianze kujiuliza maswali mengi. Ni lini Ray amekuwa midomoni kwa watu kwa filamu aliyoifanya? Ni kwasababu Ray ana filamu yake mpya iitwayo Tajiri Mfupi ambayo ajabu haizungumzwi kama inavyozungumzwa kauli yake hiyo ya maji na weupe wake. Utasema kuwa filamu za Bongo sio nzuri ama hazina viwango kama za nje lakini kumbe tunawafahamu waigizaji hawa na tunawafuatilia. Tunapenda kujua maisha yao lakini hatupendi kuangalia filamu wanazofanya. Kwahiyo huenda wachawi wa filamu za Tanzan

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFANYA ZIARA BARIADI NA KUZINDUA BWAWA NA OFISI YA CCM.

Image
 Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akisalimiana  na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Dutwa  akiwa katika ziara ya mkoa wa Simiyu Machi3, 2016.Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum , Esther Midimu.   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitaka maelezo kutoka kwa Kamanda wa Polisi  wa Mkoa wa Simiyu, Onesmo Lyanga kuhusu madai kuwa askari wa Usalama Barabarani mkoani  humo wanawatoza faini kubwa hadi sh 300,000/= waendesha bodaboda. Alikuwa katika mkutano wa kuwaslimia wananchi kwenye kijiji cha Dutwa wilayani Bariadi Machi 3, 2016.  Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akikagua ujenzi wa nyumba ya kuishi ya Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi akiwa akika ziara ya mkoa wa Simiyu Machi 3, 2016.  Wasanii wa Bariadi wapiga ngoma wakati Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa alipowasili kwenye bwawa la Ng'wansubuya wialayani Bariadi kufungua bwawa hilo Machi 3, 2016.   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akifurahia baada ya  kufu