Posts

Showing posts from December 21, 2015

KIMENUKA..Wema Sepetu Atimuliwa Kwenye Nyumba..Aliyodai Kainunua Kwa Sh Million 280

Image
Mizigo ikipakizwa kutoka kwenye nyumba hiyo. Musa Mateja UFALME umeanguka! Unaweza kusema hivyo! Hatimaye Miss Tanzania 2006, aliye pia staa wa filamu za Bongo, Wema Isaac Sepetu amedaiwa kutimuliwa kwenye nyumba ambayo alipanga kwa mbwembwe na kualika waandishi wa habari ili watoe ‘nyuzi’ hewani, akidai ni yake kwa kuinunua kwa shilingi milioni 280, fuatana na Ijumaa Wikienda. Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Wema amekumbwa na kadhia hiyo ya kuhamishwa kwenye nyumba hiyo iliyopo Makumbusho jijini Dar, usiku wa Desemba 18, mwaka huu. SIKIA CHANZO “Jamani mmesikia kilichomtokea Wema Sepetu? Yaani huyu dada anaishi kwa maigizo hadi basi. Lile sakata lake la kudaiwa kutumia umeme na maji kimagumashi limemtokea puani, maana kwenye umeme pekee yake nasikia anadaiwa zaidi ya shilingi milioni nane (8,000,000) fedha ambazo imekuwa shida kulipa.” Mizigo ikiwa kwenye gari. BABA MWENYE NYUMBA AINGIA KATI “Sasa baba mwenye nyumba ameingilia kati. Ameamua kulipa ye

CCM yanyakua ubunge jimbo la Masasi

Image
Mbunge Mteule wa Jimbo la Masasi kwa tiketi ya CCM, Bw. Rashid Chuachua. Chama cha Mapinduzi kimeweza kutetea jimbo lake la Masasi katika uchaguzi ulifanyika jana baada ya kuahirishwa Okt. 25 mwaka huu kutokana na kifo cha aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha NLD, Dkt. Emamanuel Makaidi kufariki Dunia huko Nyangao mkoani Lindi. Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya jimbo la Masasi, Fortunatus Kagoro amesema kuwa Bw. Rashid Chuachua amepata kura 16,597 akifuatiwa na Ismail Makombe maarufu kama Kundambanda wa CUF, aliyepata kura 14,019. Wengine walioshiriki katika uchaguzi huo ni Swaleh Ahmad wa CHADEMA, aliyepata kura 512, Omary Timothy wa ACT-Wazalendo aliyepata kura 347, na Angelus Thomas wa NLD aliepata kura 70. Wakati huo huo katika harakati za Uchaguizi wa Ubunge katika jimbo la Ludewa Wafuasi watatu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Jimbo la Ludewa wameshambuliwa na watu wanao daiwa kuwa ni w

Rais Magufuli Akutana na Maalim Seif Ikulu leo Kuongelea Mgogoro wa Uchaguzi wa Zanzibar

Image
Rais Magufuli amekutana na kuzungumza na mgombea urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif juu ya mgogoro wa uchaguzi wa Zanzibar TOA MAONI YAKO HAPA CHINI