Posts

TANESCO Wakata Umeme Kambi ya JWTZ , Magereza na Polisi.......Ofisi ya Mkuu wa Mkoa nayo Nusura Ikatiwe

Image
Agizo la Rais Dk. John Magufuli la kulitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuzikatia umeme taasisi za Serikali zinazodaiwa jumla ya Sh bilioni 8.6 limeanza kufanya kazi mkoani  Arusha. Ofisi zilizoanza kuonja machungu ya kukosa umeme kuanzia jana hadi zitakapolipa madeni ni Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Oljoro, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Magereza, Hospitali za Serikali na Taasisi za Maji. Nyingine zilizokatiwa umeme ni Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha ikiwamo Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha na Kituo Kikuu cha Polisi cha Arusha. Wakati ofisi hizo zikikosa umeme, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ilinusurika baada ya kuanza kulipia deni lake la Sh milioni sita 6 kwa awamu. Akithibitisha kufanyika kwa operesheni hiyo iliyotajwa kuwa endelevu kwa ofisi hizo mkoa mzima, Ofisa Uhusiano wa Tanesco mkoani hapa, Saidy Mremi, alisema inalenga kukusanya madeni yote ya miaka iliyopita. “Tunatekeleza agizo la R

Sugu Amvaa ‘Bashite’ Bungeni

Image
MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amemshambulia Bashite huku akisema kuwa mtu huyo alipaswa awe mahakamani na sio ofisini kwa madai kuwa amefoji vyeti vya elimu ya sekondari jambo ambalo ni kosa kisheria. Hayo ameyasema leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia hoja kuhusu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Aidha Sugu amemtaka Rapa ROMA Mkatoliki ajitokeze hadharani aeleze wazi kuhusu alivyotekwa na nani alihusika ili jamii ielewe na mamlaka husika iweze kuchukua hatua ikiwemo kuwabaini waliyotekeleza tukio hilo ambalo si la kibinadamu. Sugu aliwageukia wasanii wa Filamu Bongo ambao hivi karibuni waliandama wakipinga uingizwaji holela wa filamu za nje ambazo wanadai zinaporomosha soko la filamu za ndani. Sugu amewataka wasanii hao waache kutumika kisiasa na badala yake wafate misingi ya kazi zao.

Zitto: Tumethibitisha Kampuni ya Boeing wametuuzia ndege ya mwaka 2009

Image
Kwa Mujibu wa Zitto Kabwe ameandika Taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Facebook "Tumeshathibitisha bila mashaka kuwa Kampuni ya Boeing wametuuzia ndege ya mwaka 2009 Kwa bei ya mwaka 2017. Kazi Kwa Watanzania ni kuishinikiza Serikali iseme imelipa kiasi gani? Nukuu kutoka mtaalamu wa ndege na picha ya uthibitisho wa terrible teen hiyo. Ninasikitika Sana kuwa Rais mwenyewe na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha ndio walikutana na watu wa Boeing kuhusu dili hili. Ina maana Boeing wamemdanganya Rais wetu. Sio sawa hata kidogo "Terrible Teen" LN19 iliondolewa kutoka was 45-12 na itakabidhiwa Air Tanzania itakapokuwa imemalizika mwishoni mwa Mwaka huu "

UMUHIMU MKUBWA WA KOMAMANGA (POMEGRANATE) JUU YA MARADHI YA KANSA

Image
Uchunguzi mpya umeonyesha kwamba, katika tunda la komamanga kuna kemikali zinazozuia kansa ya matiti isitambae mwilini. Uchunguzi huo uliochapishwa katika jarada la Utafiti la kuzuia Kansa umeonyesha kwamba, kemikali ziitwazo ellegitannins zinazopatikana kwa wingi kwenye komamanga, zinaweza kuzuia kimeng’enyo (enzyme) aina ya aromatase, suala ambalo huzuia kukua kwa Homoni ya estrogen inayopatikana katika kansa ya matiti. Shiuan Chen Kiongozi wa uchunguzi huo amesema kwamba, kemikali hizo hupunguza uzalishwaji wa estrogen, na kusaidia kuzuia seli za kansa ya matiti zisizaliane mwilini, pamoja na tezi la ugonjwa huo lisikue. Aromatase, ni kimeng’enyo ambacho hugeuza Homoni ya androgen kuwa estrogen, na kushambulia kimeng’enyo hicho ndio lengo kuu la dawa za kupambana na kansa za matiti zinazosababishwa na homoni ya etrogen. Huko nyuma pia uchunguzi ulionyesha kwamba tunda la komamanga lina faida kubwa kiafya hasa kwa kuwa na  anti Oxidant nyingi na vitamin mbalim

Bunge lafuta maneno kwenye hotuba ya Sugu kabla ya kusomwa

Image
Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu ameagiza Hotuba ya Kambi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ihaririwe na kufuta maneno yote katika kurasa 17. Zungu ametoa uamuzi huo leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu, hata kabla ya bajeti yenyewe kuwakilishwa na Waziri Dk Harrison Mwakyembe. Zungu amesema amezipihitia hotuba zote na kubaini kuwa ile ya upinzani itakayowalishwa na Joseph Mbilinyi 'Sugu' ina masuala yaliyopo mahakamani ambayo yamekwishazuliwa katika bajeti zilizotangulia. Amesema maneno yenye mwelekeo huo yakisomwa atachukua hatua.

Faida ya majani ya mparachichi

Image
Siku chache zilizopita tuliangazia macho katika kuona faida za kula parachichi, ni amani yangu kwamba ulijifunza jambo kubwa sana, hivyo naomba siku ya leo naomba tuangalie faida majani ya mmea wa parachichi katika mwili wa mwadamu. Zifuatazo ni faida ya majani ya mparachichi. Majani ya parachichi humsaidia mwanamke ambaye hupata maumivu wakati wa hedhi. Unachotakiwa kufanya ni; Chukua majani kiasi ya mparachichi, kisha yachemshe kwenye maji lita moja, ukijiridhisha yamekwisha chemka epua kisha yaache yapoe, kisha anza kunywa maji hayo kiasi cha nusu kikombe cha chai, kunywa muda wa asubuhi na jioni kwa muda wa wiki moja utaona mabadiliko. 1. Majani ya mparachichi  husaidia sana kuongeza kiwango cha maziwa kwa kinamama. 2. Unachotakiwa kufanya ni Tatatafuna jani moja la parachichi kila siku, lakini hakikisha jani unalotafuna liwe katika hali ya safi na umeliosha vizuri. 3. Pia majani haya ya mparachichi ni msaada sana katika kutibu majeraha, il

Njia 10 muhimu ukitaka kuondoa sumu mwilini mwako

Image
Mwili wa binadamu unaweza kupatwa na sumu au takataka zisizohitajika na kwa namna mbili; kupitia mazingira tunayoishi kama vile viwanda, migodi na maeneo mengine hatarishi ama kupitia vyakula na vinywaji ambavyo tunatumia kila siku. Sumu au takamwili,zinaweza kuingia mwilini kupitia dawa mbalimbali hasa za kizungu tunazotumia kujitibu magonjwa mbalimbali. Mwili huzalisha sumu au takamwili (free radicals) kila mara kunapofanyika mmeng’enyo wa chakula mwilini mwako. Hizi ni ishara zinazoweza kuashiria mwili wako umeingiwa na takamwili: -Uchovu sugu -Maumivu ya maungio -Msongamano puani -Kuumwa kichwa kila mara -Tumbo kujaa gesi -Kufunga choo au kupata choo kigumu -Kukosa utulivu -Matatizo mbalimbali ya ngozi ikiwemo chunusi -Pumzi mbaya -Mzunguko wa hedhi usio sawa -Kuishiwa nguvu -Kushindwa kupungua uzito -Kupenda kula k

Watumishi wa zahanati mbili wote feki"

Image
Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali amefunguka na kusema zahanati mbili katika halimashauri yao zimefungwa kutokana na watumishi wake wote kukutwa na vyeti feki, jambo ambalo linapelekea wananchi katika kata hizo kukosa huduma.  Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali. Hamidu Bobali alisema hayo jana bungeni na kusema sakata la vyeti feki limeleta athari katika halimashauri yao "Hili suala la vyeti feki Mh. Mwenyekiti limeleta athari kubwa sana katika halimashauri yetu, hivi hapa napoongea kuna zahanati mbili zote zimefungwa kutokana na ukweli kwamba watumishi wake wote wameonekana na vyeti feki" alisema Hamidu Bobali  Mpaka sasa sakata la vyeti feki limeanza kuleta athari katika baadhi ya maeneo baada ya watumishi wengine kuamua kujiondoa wenyewe makazini kama amri ya Rais Magufuli ilivyoagiza kuwa wajiondoe wenyewe na kuachia nafasi hizo. 

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFUNGUA KUTANO WA ROTARY CLUB ARUSHA

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akivishwa beji ya uanachama wa Rotary Club na Dk. Manoj Desai kwenye mkutano wa 92 wa mwaka unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Rotary Club kwenye mkutano wa 92 wa mwaka unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifungua mkutano wa 92 wa mwaka wa Rotary unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha Mei 4, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Washiriki wa Mkutano mkutano wa 92 wa mwaka wa Rotary unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) wakishangilia mara baada ya Waziri Mkuu kutangaza kuwa yeye na mke wake, Mary Majaliwa wanajiunga na Rotary Club katika ukumbi wa AIC

Faida za kutumia juisi ya miwa katika kuimarisha afya zetu

Image
Bila shaka unaifahamu juisi ya miwa, watu wengi tumekuwa tunakunywa na wengine tukiwa tunaibeza pia, hii ni kwasababu tumekuwa hatujui faida zitokanazo na unywaji wa huisi hiyo. Leo nataka nikupashe japo kwa uchacje faida za kunywa juisi ya miwa katika afya zetu. Kunafaida nyingi za juisi ya miwa. Baadhi ya faida hizo ni kama zifuatazo; 1. Juisi ya miwa inauwezo mkubwa wa kuipatia miili nguvu kwa haraka na kukata kiu ya maji.  Hii ni kwa sababu juisi ya miwa ina sukari "sucrose" ambayo kazi yake kuu ni kutengeneza nguvu mwilini. Kwahiyo wakati mwingine ukiwa na nguvu au uchovu, badala ya kunywa vinywaji vya viwandani tafuta juisi ya miwa. 2.  Husaidia figo kufanya kazi vizuri. Juisi ya miwa inasaidia kuongeza kiwango cha protein mwilini na ku-imarisha ufanyaji kazi wa figo. Juisi a miwa iliyochanganywa na maji ya Nazi husaidia kupunguza maumivu hasa yanayosababishwa  na mawe yaliyopo kwenye figo. 3. Hupunguza uwezrkano wa kupata ugonjwa wa kansa. Ju

MFAHAMU JOHN STEPHEN ,MTANZANIA MAARUFU ULIMWENGUNI KULIKO HAPA TANZANIA

Image
John Steven Akhwari ni mwanariadha mstaafu. Alizaliwa mwaka 1938 kule Mbulu- Mkoani Manyara. Aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Olimpic mwaka 1968 nchini Mexico, katika mashindano ya riadha ya kilomita 42. Washiriki walikuwa 75, lakini waliomaliza shindano ni 57 pekee, huku John Steven Akhwari akimaliza wa mwisho kabisa. Kwa nini alimaliza wa mwisho?   Baada ya mbio kuanza, walipofika kilomita ya 19, mshiriki mojawapo alimparamia, kumsukuma na kuanguka vibaya mno. Aliumia begani, na goti la mguu wa kulia lilitenguka. Gari la huduma ya kwanza lilimfikia na kumpa matibabu, akaweza kusimama tena na kuendelea na riadha. Umaarufu wake duniani. Watu waliomhudumia walimlazimisha kuaihirisha shindano na apande kwenye gari lakini alikataa katakata. Aliendelea na riadha huku akichechemea. Alifanikiwa kumaliza kilomita zote 42, jioni ya saa 1 kwa saa za Mexico. Watu wachache waliokuwa wamebakia uwanjani walimshangilia sana. Mwishoni kabisa, waandishi wa habari

Kiama kingine cha Majina wenye vyeti feki J’tano

Image
WAKATI watumishi wa umma 9,932 wakiwa wamebainika kuwa na vyeti feki mpaka sasa, idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka Jumatano ijayo, siku ambayo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi itatangaza majina zaidi. Ijumaa iliyopita, serikali ilitangaza kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa vyeti vya kuhitimu kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wa Sekretarieti za Mikoa, Tawala za Mikoa, Wakala wa Serikali, Taasisi za umma na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema uhakiki wa vyeti unaendelea kwa watumishi wa wizara zilizosalia na taasisi mbalimbali. Alisema uhakiki huo wa awamu ya pili na ambao utafuatiwa na awamu ya tatu, unatarajiwa kukamilika Jumatano. Alisema baada ya matokeo ya uhakiki huo kuwekwa hadharani, uamuzi wa serikali utatolewa. “Maamuzi ya watumishi 9,932 waliobainika kuwa na vyeti vya kugushi ili

WAZIRI LUKUVI AMTUMBUA AFISA MIPANGO MIJI LINDI

Image
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsimamisha kazi  Ndugu Castory Manase Nkuli Afisa Mipango Miji wa Lindi kuhusu tuhuma za kumilikisha ardhi kinyume cha sheria. Na. Hassan Mabuye & Muhammad Salim Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameamuru kusimamishwa kazi Afisa Mipango Miji wa Lindi Ndugu Castory Manase Nkuli baada ya kunyang`anya ardhi ya vijiji vya Ruvu na Mchinga hekari 4000 na kumilikisha kampuni ya Azimio Housing Estate kinyume cha sheria ya Ardhi. Mhe. Lukuvi aligundua hayo baada ya kuona utaratibu wa umilikishaji wa ardhi haukufuatwa  na badala yake kuonekana kuwa na mianya ya rushwa kwa kuwa ardhi hiyo imehamishwa kutoka ardhi ya kijiji hadi kumilikishwa kwa kampuni ya Azimio ambapo kisheria ilitakiwa hati ya eneo hilo itoke kwa idhini ya Rais. Aidha, Afisa Mipango Miji huyo aligundulika kuwa na kosa la kughushi kwa kujifanya ni Afisa ardhi baada ya kuandika barua na kuisai

JB RAY NA RICH WAFUNGUKA MAZITO KUHUSU TUHUMA ZA KUHONGWA VIWANJA NA PESA

Image
Baada ya kuwepo kwa madai kuwa mastaa wa filamu Bongo, Jacob Steven (JB), Single Mtambalike (Rich) na Vincent Kigosi (Ray) walihongwa fedha na viwanja ili ‘kuinjinia’ maandamano ya hivi karibuni kupinga sinema za nje, mastaa hao wamebanwa na hatimaye kufungukia ishu hiyo inayowatafuna, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili. Chanzo kilicho karibu na tasnia hiyo kililiambia Risasi Mchanganyiko kuwa kampuni moja ya usambazaji filamu (jina kapuni kwa sasa), iliwapa fedha baadhi ya waigizaji ili wafanye maandamano ya kuziondoa sokoni filamu hizo za nje, zinazodaiwa kukingiwa kifua na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba. Inadaiwa kuwa baada ya kampuni hiyo ya usambazaji ‘kupenyeza sumu hiyo’ waigizaji hao walikwenda kwa kigogo mmoja wa kisiasa na kumshawishi kuwaunga mkono, ambaye naye alikubali na kuwaomba waigizaji hao kufanya kila wawezalo, kumtoa kwenye kiti chake, Simon Mwakifwamba, kwani ana ukaribu na hasimu wake wa siasa. “Kuna watu w

Hali ya Mbunge wa Chadema Tarime si Shwari

Image
Hali ya Mbunge wa Tarime Vijijini Mh. John Heche imebadilika usiku wa kuiamkia leo na amekimbizwa hospitalini Dodoma.  Huenda akahamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Tumuombee comrade Heche na pole sana kwa familia na wabunge wenzake.

SPIKA JOB NDUGAI ATOA MAANA YA "FALA"BUNGENI

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai jana ameonyesha aliumizwa na kitendo cha Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA Mh. Halima Mdee kumwambia 'fala' bungeni na kusema hata kama mtu humpendi lakini si vyema kumtusi matusi. Job Ndugai alisema hayo alipokuwa akitoa maana ya neno fala bungeni ambapo ilibidi arejee maana hiyo kwa kusoma kupitia kamusi ya Kiswahili ambayo ilitoa maana kuwa fala ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri. "Kwa neno ambalo alilisema Halima Mdee humu ndani, kamati imeenda kwenye tafsiri ikachukua Kamusi kwa neno lile alilosema ambalo maana yake kwa yule unayemwambia 'Fala' ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri, ni mtu mpumbavu, ni mtu bwege, ni mtu mjinga, ni mtu bozi, ni gulagula. Ndiyo maana nikasema sisi Waafrika hata kama humpendi namna gani mwenzako huwezi kumfanyia hivyo"  alisisitiza Job Ndugai

Dk Mwakyembe: Televisheni, Redio kusoma vichwa vya habari tu kwenye magazeti kuanzia kesho

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe   Mwanza.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amezitaka Televisheni na Redio kuanzia kesho kusoma vichwa vya habari vya magazeti tu ili kuwavutia wasomaji kununua magazeti kwa habari kamili. Dk Mwakyembe amesema hayo leo jijini Mwanza katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari nchini ambapo pia amesema ataendelea kutetea na kulinda haki za waandishi wa habari huku akiwahakikishia ulinzi waandishi wa habari za uchunguzi. Pamoja na mambo mengine Dk Mwakyembe amehakikisha kuwepo kwa ushirikiano wa kutosha kwa wamiliki wa vyombo vya habari  na kwamba ameagiza idara ya mawasiliano kutengeneza mawasiliano ya kudumu na wawe wanakutana angalau mara moja kwa mwezi kujadili udhaifu unaoweza kujitokeza na kuchukua hatua lengo ni kuwekana  sawa.

SAMATTA AMEANZA KUIKAMATA KRC GENK, SHABIKI AINGIA NA BANGO AKIOMBA JEZI

Image
Ukisema mambo yanaanza kunyooka, baada ya mashabiki wengi wa KRC Genk kuonyesha imani kubwa kwa mshambulizi, Mbwana Samatta.Samatta anaonekana kuwa bora zaidi kutokana na kuwa tegemeo katika kikosi cha Genk cha Ubelgiji.Imeonekana mmoja wa shabiki akiwa na bango uwanjani, akiomba jezi ya Samatta.Imekuwa kawaida kwa mashabiki wa Ulaya kuomba jezi kwa wachezaji wanaowapenda wakitumia mabango kama shabiki huyo wa Genk. Samatta amekuwa akifunga mfululizo na wakati mwingine kushindwa kufanya hivyo kwa kipindi fulani lakini imani kwa benchi la ufundi na mashabiki inaonekana kupanda kwa kiwango cha juu kabisa.

CHADEMA wateua majina mapya ya Wagombea wa Bunge la Afrika Mashariki

Image
Chadema wafanya uteuzi wa wagombea Ubunge EALA.   Tazama majina yao: 

Faida za Mchaichai kiafya

Image
Faida za mchachai zipo nyingi sana wengi wetu hudhani mchaichai ni kuongo cha kuweka kwenye chai pekee, au ni dawa kwa ajili ya kuua mbu pekee, ila mchaichai huwa na faida lukuki zaidi ya hizo tu. Naomba uweze kusoma makala haya ili uone faida nyinginezo za mchaichai. Zifuatazo ni faida za kutumia mchaichai kiafya. 1. Mchaichai ni kinga dhidi ya saratani. Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa kwenye kila gram 100 ya mchaichai, kuna viondosha sumu ambavyo vina uwezo wa kuukinda mwili dhidi ya ugonjwa wa saratani. Mwaka 2006, timu ya watafiti kutoka Chuo kikuu cha Gurion, Israel waligundua mchaichai un uwezo wa kuua seli zinaweza kusababisha saratani. 2. Hutibu magonjwa ya kuhara. Husaidia umeng’enyaji wa chakula Chai ya mchaichai hurahisisha utaratibu wa mmeng’enyo wa chakula na pia hutibu magonjwa ya kuhara na maumivu ya tumbo ikiwamo kujaa gesi. Hurahisisha utaratibu wa kuondoa uchafu mwilini Katika matibabu, unatibu magonjwa mengi ikiwemo kushusha joto, hasa