Posts

Mwanzilishi wa JamiiForums, Maxence Melo Akamatwa na Polisi, Anyimwa Dhamana

Image
  DAR ES SALAAM: Mwanzilishi, Mmiliki na Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo, ameitwa na baadaye kuwekwa selo katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam (Police Central) leo Desemba 13, 2016. Polisi wameeleza muda huu kwamba leo atalala ndani (selo) hadi kesho atakapofikishwa mahakamani. Imeelezwa kuwa, kosa la kushikiliwa na Jeshi la Polisi ni kukataa kutoa taarifa binafsi zilizohitajika za wateja wa mtandao anaoumiliki wa JamiiForums. Maxence ameendelea kushikilia msimamo wake kuwa, kufanya hivyo ni uvunjwaji wa sheria na haki za wananchi. Maxence Melo amekamatwa huku kukiwa na Kesi ya Kikatiba dhidi ya taarifa ambazo Jeshi la Polisi wanazitaka, kesi namba 9 ya mwaka 2016 dhidi ya Jamii Media dhidi ya Polisi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kesi ambayo mahakama kuu itatolea hukumu, tarehe 20 Februari. CHANZO: JAMII FORUMS

MSANII CHUCHU HANS ASEMA HAYA BAADA YA KUSHINDA TUZO

Image
  Ushindi wa tuzo ya Muigizaji bora wa kike wa Tuzo za EATV 2016 kumemtoa machozi Chuchu Hansy na kumkumbusha mambo mengi aliyopitia kwenye maisha yake. Muigizaji huyo ambaye hakuwepo kwenye usiku huo wa tuzo na kuwakilishwa na meneja wake, ametoa ya moyoni kupitia Instagram kwa kusema ushindi huo umemfanya akumbuke maneno aliyokuwa akipewa na mama yake katika kipindi cha ukuaji wake. “Naamini kuna uwepo wangu kwa kila hatua tupigayo, ama hakika usitamalaki ya moyoni kwa kuyadhihaki ya machoni. Hii imenipa funzo zaidi ya lile alilonipa mama nikiwa na vunja ungo,” alisema Chuchu. “Mama aliniambia heshimu watu bila kuwa dhihaki kwa makundi,ama kuwa bagua kwa rika,” “Niwashukuru wote mlio nipigia kura amahakika mme tenda vema,likini mimi sio bora kuliko wenzangu ila nadhani kwa wino wakura zenu ulistahili niwe BEST ACTRESS, niwashukuru zaidi na zaidi, nikiandika maneno haya machozi yananitoka lakini hii yote ni heshima mlio nivika NENO LA KALE NI ASANTE,” aliongez

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) RAIS DKT. MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) ambaye ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein kabla ya kuanza kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Alichokisema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kwenye Sherehe za Maulid, Singida

Image
Katika kusherekea siku ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammed (S.A.W), Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuwatumikia Watanzania wote bila kujali imani zao za kidini. Majaliwa ameyasema hayo katika sherehe za kitaifa za Maulid ambazo zimefanyika mkoani Singida na kusema kuwa kuna matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza katika jamii na katika kuyachukulia hatua za kisheria vitendo hivyo Serikali haitakuwa ikibagua mtu kutokana na imani yake ya kidini kama jinsi inavyofanya kwa shughuli za maendeleo. “Serikali inawashukuru sana kwa kuendelea kuunga mkono jitihada ya Serikali ya Rais Magufuli, tunaamini juhudi tunazofanya za kuweka nidhamu kwa watumishi wa umma na taasisi binafsi mtaendelea kutuunga mkono, tutaendelea kuruhusu uhuru wa kuabudu na kushirikiana na viongozi wa dini lakini tu mafundisho yanayotolewa yasikiuke sheria na kanuni za nchi, “Serikali ipo macho kupambana na tukio lolote lenye nia ya kupoteza amani ya

Mzee wa Upako: Wote Walionichafua Watakufa Mwakani, Wasipokufa Nitaanza Kuuza Gongo

Image
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako jana amesema waandishi wote wa habari wanaoandika habari za kumchafua, watakufa kabla ya kufika Machi 2017. Kauli hiyo ameitoa ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yale yaliyoandikwa katika vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake na kulewa. “Kila mwandishi aliyeniandika vibaya, ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mko humu mmekuja na mnasikiliza tu,” alisema. “Akisema Mungu uishi wewe basi, nakuwa sina namna, lakini sijawahi kumtumikia Mungu ambaye ananyamaza. Nilishakubaliana mimi na Mungu, mpango wa Mungu ndiyo mpango wangu, sasa wajiandae, mimi siyo Sheikh Yahaya, mmeingia choo cha kike, nasema ‘Mama yangu mzazi’ nitaacha kuhubiri, nitaacha kuhubiri ….mimi

Meli Yenye Malori 600 ya Kiwanda cha Dangote Yawasili Mtwara

Image
MTWARA: Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Dangote Cement Industries ya jijini Mtwara, ambaye pia ni bilionea namba moja Barani Afrika, Alhaji Aliko Dangote jana Desemba 10, 2016 alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Dk Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam alimthibitishia kuwa hana lengo la kufunga kiwanda chake kama inavyodaiwa badala yake anatafuta fursa nyingine za kuwekeza hapa nchini. Katika kuthibitisha hilo, Mfanyabiashara huyo alisema jana kuwa meli yenye malori mapya 600 kwa ajili ya kusambazia saruji yake mikoani, itawasili nchini. Aliongeza kuwa lengo la kufanya biashara hapa nchini mbali na kutengeneza faida pia ana lengo la kuisaidia serikali ya Tanzania kutengeneza ajira hivyo hana sababu ya kuagiza mali ghafi toka nje ya nchi ambazo zinapatikana nchini. Baada ya kufanya mazungumzo hayo, meli yenye magari hayo 600 ilitia nanga katika bandari ya Mtwara ambapo ndipo kiwanda cha Saruji cha Dangote kilipo. Aidha, imeelezwa kuwa w

Baada ya Waziri Mkuu Majaliwa Kukabidhiwa Pembe, Mapya Tena Yaibuka Kifo cha Faru John

Image
Dar es Salaam. Kifo cha Faru John aliyehamishiwa Hifadhi ya Creta ya Ngorongoro kimeendelea kupunguza idadi ya wanyama hao ambao wanatafutwa kwa udi na uvumba na majangili kutokana na pembe zake kuuzwa ghali kwenye magendo, mara tatu zaidi ya dhahabu au dawa za kulevya aina ya cocaine. Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliliibua sakata la kutoweka kwa Faru John katika Hifadhi ya Sasakwa Black Rhino Sanctuary akidaiwa kufa. Kutokana na utata wa sehemu alipokuwa Faru huyo, makachero saba walifika Ngorongoro kufanya uchunguzi na kuwakamata maofisa watano waliotajwa kuhusika katika kumhamisha faru huyo. Hata hivyo, juzi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikabidhiwa pembe ikiwa ni kithibitisho kuwa Faru John amekufa. Pia, alipewa taarifa kuhusu utaratibu uliotumika kumhamisha kutoka Ngorongoro kwenda Sasakwa. Kilichosababisha Waziri Mkuu awe mbogo baada ya kuwapo kwa utata wa alipo faru huyo, ni upekee wake, thamani yake kiutalii na kuwa n

Mchungaji Awanywesha Waumini Dawa ya Kuua Bakteria “Dettol”

Image
MCHUNGAJI maarufu kwa jina la Rufus Phala kutoka kanisa la AK Spiritual Christian lililopo Makgodu, Limpopo, Afrika Kusini amewashangaza watu kwa kitendo cha kuwanywesha  Dettol waumini wake ilihali ina madhara kwa binadamu. Kwa mujibu wa Daily Sun SA, mchungaji huyo alifanya kitendo hicho kwenye ibada za kawaida kanisani kwake akiwataka waumini wenye matatizo na wanaohitaji maombi wanywe Dettol aliyokuwa ameishika mkononi mwake huku akiwambia watapona shida zao ikiwemo magonjwa. “Nafahamu kuwa Dettol ni sumu, lakini Mungu ameniagiza niwape na muitumie. Mimi nilikuwa wa kwanza kuinywa,”   – Mchungaji. Pia alisema kuwa amepokea meseji za WhatsApp kutoka kwa watu waliokunywa na wamethibitisha kupona. Baada ya kuwepo kwa taarifa hizo, amehojiwa Daktari kutoka Afrika Kusini, Dr Mabowa Makhomisane, ambaye amekiri kuwa Dettol ina madhara inapotumika tofauti na maelekezo ikiwemo kuinywa “Mtu akinywa Dettol na ikafika tumboni, kimsingi hupunguza m

Kamati Kuu ya CCM: Leo ni Kikao cha Kwanza kwa Mwenyekiti JPM, Yatakayojadiliwa Yapo Hapa

Image
Dar es Salaam. Kamati Kuu ya CCM inakutana leo huku kaulimbiu ya “Hapa Kazi Tu” ikitarajiwa kutawala kikao hicho cha kwanza kwa mwenyekiti John Magufuli, ambaye ameonyesha dalili za kufumua sekretarieti wakati huu wa kuelekea uchaguzi wake mkuu. Kikao hicho cha siku mbili kitachofuatiwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa, pia kinatarajiwa kujadili mambo mengine nyeti, kama maandalizi ya uchaguzi utakaofanyika mwakani kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa kwa kuchagua kamati Kuu mpya na suala la uchaguzi wa meya wa Kigamboni ambayo sasa ni wilaya. Pia kikao hicho kinatarajiwa kujadili chaguzi ndogo za mbunge wa Dimani na madiwani pamoja na ripoti ya wasaliti ambayo Magufuli alikabidhiwa na mtangulizi wake, Jakaya Kikwete Julai 23 baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti. Suala jingine linalotarajiwa kuchukua nafasi ni hali ya kisiasa nchini, ikijumuisha suala la Zanzibar, upigaji marufuku mikutano ya hadhara, hali ya kiuchumi ambayo inalalam

ALI KIBA, LADY JAYDEE NA DJ BONNY LOVE WANG'ARA TUZO ZA EATV 2016

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akikabidhi Tuzo ya Heshima kwa DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love baada ya kutangazwa mshindi wa heshima katika tuzo za EATV AWARDS 2016 zilizofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam. Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimsikiliza DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love alipokuwa akitoa shukurani zake mara baada ya kupokea tuzo yake ya heshima iliyotolewa na EATV. Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Lady Jay Dee akipongezwa na Mpenzi mara baada ya kupokea tuzo yake katika hafla ya utoaji wa tuzo za EATV AWARDS zilizofanyika kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam. Mwanamuziki Ali Kiba akipokea tuzo yake ya ushindiwa Wimbo Bora wa Mwaka kutoka kwa Nandi Mwiyombela kutoka kampuni ya Vodaco Tanzania katika Tuzo za Muziki za EATV AWARDS zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam. Msanii wa Muzi

Mongela Atinga Mitaani Kuhimiza Usafi wa Jiji la Mwanza

Image
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela akikatiza katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza kuhimiza usafi. Mhe. John Mongela akitoa maelezo kuondoa vitu vilivyowekwa nje ya duka la mkazi wa Mwanza. Wakazi wa Mwanza eneo la soko kuu wakiondoa uchafu katika mtaro uliopo eneo hilo. Mwananchi huyu akiondoa takataka zilizopo kwenye mtaro uliopakana na duka lake.    Zoezi la kusafisha Jiji la Mwanza likiendelea. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela ametembea mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza kuhimiza watu kufanya usafi katika maeneo wanayofanyia kazi pamoja na kutoa muongozo wa namna wafanyabiashara watakavyoendesha biashara zao. Ziara hiyo imefanyika baada ya kumaliza zoezi la kuondoa wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika maeneo yasiyoruhusiwa na kuwapeleka maeneo mbalimbali ambayo yalitengwa kwa ajili ya wafanyabiashara hao. Katika ziara hiyo iliyokuwa imeambatana na viongozi mbalimbali wa serikali walipita maeneo ya Makoroboi, Liber

Trump Kusitisha Uagizwaji wa Ndege Mpya za Air Force One

Image
Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump amesema anataka kufuta ombi la ununuzi wa ndege mpya za Air Force One ambazo hutumiwa na marais wa Marekani. Wiki sita kabla ya kuchaguliwa, aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter kuwa: “Boeing wanaunda ndege mpya aina ya 747 Air Force One za kutumiwa na marais siku zijazo, lakini gharama yake imezidi, zaidi ya $4 billion. Futa oda hiyo!” Serikali ya Marekani iliingia kwenye mkataba na kampuni ya Boeing ili kutengenezwa kwa ndege hizo mbili au zaidi za kuwabeba marais. Ndege hizo zilitarajiwa kukamilika na kuanza kutumiwa mwaka 2024. Hisa za kampuni ya ndege ya Boeing zilishuka kwa zaidi ya 1% baada ya ujumbe huo wa Trumpp kwenye Twitter, ingawa zilijikwamua baadaye. Trump hatarajiwi kutumia ndege hizo mpya, iwapo hatashinda uchaguzi wa muhula wa pili wa mwaka 2020.

Serikali Kuanzisha Tuzo za Mitandao ya Kijamii kwa Wanahabari

Image
Mwandishi wa habari wa mtandao huu, Denis Mtima (kushoto) akikabidhiwa kadi ya kujiunga na mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPF na Waziri Nape Nnauye. Nape akimkabidhi mwanadada mwandishi wa habari, kadi ya ATM ya NMB. …Akisisitiza jambo fulani kwa wanahabari. …Akizungumza jambo. Mwakilishi wa wadhamini wa semina hiyo ambaye ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Vicky Bishubo, akizungumza jambo kwenye hafla hiyo. Mkurugenzi wa mfuko wa hiari wa mwanachama wa PSPf, Adam Mayingu ambao nao walikuwa wadhamini wa semina hiyo, akizungumza jambo. Vicky Bishubo akimkabidhi Nape zawadi iliyokuwa imeandaliwa kutoka NMB. Taswira ilivyoonekana katika semina hiyo. WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema serikali inatarajia kuanzisha Tuzo za Umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs na website) kuanzia mwakani 2017. Hayo ameyasema jana wakati akifunga semina kwa mtandao wa wamiliki wa mitandao ya kijamii

Waziri Mkuu Majaliwa Ataka Nyaraka za Faru John Ifikapo Kesho

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameugiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya  Ngorongoro (NCAA), kumpelekea nyaraka zote zilizotumika katika kumhamisha faru maarufu kwa jina la John katika hifadhi hiyo ifikapo Desemba 8, 2016. Majaliwa amesema ana taarifa kuwa walimhamisha Faru John Kreta kwa siri na kumpeleka  V I P Grumet  Serengeti Disemba 17, 2015 na waliahidiwa kupewa sh. milioni 200 ambapo  na wamepewa sh.  milioni 100 kwa ahadi ya kumaliziwa sh. milioni 100 nyingine baadaye. Amesema hayo Desemba 6, 2016 alipotembelea Ofisi za makao makuu ya NCAA, zilizoko wilayani Ngorongoro mkoa Arusha  wakati akizungumza na watumishi wa mamlaka hiyo pamoja na Wajumbe wa  Baraza la Wafugaji ikiwa ni  sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani hapa. “Naomba niletewe nyaraka zote zilizotumika kumuomba na kumuondoa faru huyo na barua zilizotumika kujadili suala la faru John. Nasikia amekufa naomba pembe ziletwe ofisini na iwapo itath

Diamond na Zari Wamepata Mtoto wa Kiume Leo Des. 6, Bofya Hapa Kuona Pichaz

Image
Pretoria, Afrika Kusini: TAARIFA njema kwa mashabiki wa msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, Nasbu Abdul “Diamond Platnumz” ambaye leo leo Desemba 6, 2016, mpenzi wake Zarina Hassan “Zari The Boss Lady” amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Netcare iliyopo mjini Pretoria nchini Afrika Kusini. Mtoto aliyekuwa akisubiliwa kwa hamu kubwa. k Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Diamond kupitia ujumbe aliouandika kwenye akaunti yake ya Instagram ameeleza kuwa mtoto wao huyo amezaliwa majira ya saa 8:35 usiku kwa saa za Afrika kusini ambazo ni sawa na saa 10:35 alfajiri kwa saa za Afrika Mashariki. Mbali na Diamond kuposti picha zikionesha miguu ya mtoto huku akieleza kuwa mpaka sasa bado hawajapata jina la kumuita mtoto wao, mpenzi wake, Zari ameposti picha ikionesha mikono ya kichanga chao na kuwashukuru wale wote waliokuwa wakimuombea kwa Mungu ili ajifungue salama. Mtoto huyo anakuwa ni wa pili kwa Diamond kuzaa na mpenzi wake Zari baada ya m

Ajali ya Lori na Hiace Yaua Watu 9 na Kujeruhi 18, Iringa

Image
   IRINGA: Watu tisa wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa kufuatia ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Ifunda mkoani Iringa jana Desemba 5, 2016 baada ya lori kugongana na gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace.   Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amesema dereva wa lori lililopata ajali lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam, alishindwa kufunga breki na kuigonga Hiace iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara.   “Lori limeharibika kabisa na Hiace pia imeharibika vibaya,” alisema RC Masenza.   “Lori hilo liliposhindwa kufunga breki liliigonga Hiace ambayo ilikuwa na abiria na kwenda mbele na kisha kugonga watembea kwa miguu.”  RC Masenza alisema katika ajali hiyo iliyotokea jana jioni, madereva wa magari hayo wote wamejeruhiwa na wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa pamoja na majeruhi wengine. “Dereva mmoja yupo chumba cha upasuaji kwa kuwa mguu wake umevunjika na mwingine yupo wodini,” alisema RC Masenza.