PICHA: SAFARI YA MWISHO YA FIDEL CASTRO WA CUBA
Mwili wake wa aliyekuwa Rais wa Cuba umechomwa moto hadi kuwa majivu kama alivyotaka, katika sherehe ya kibinafsi, na majivu yake yamezungushwa katika msafara maalumu kote nchini kabla ya kuzikwa katika Makaburi ya Mji wa Santiago leo Desemba 4, 2016. Cuba inaadhimisha siku tisa za maombolezo kufuatia kufariki kwa Fidel Castro akiwa na umri wa miaka 90. Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwekwa garini tayari kwa kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini kabla ya kuzikwa katika Makaburi ya Mji wa Santiago Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Gari maalumu likiwa na Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Wananchi wakijipanga kuaga Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Cuba.