Posts

Tiko Apania Kuifunika Chura

Image
Stori: Gladness Mallya S TAA wa filamu na Bongo Fleva, Tiko Hassan amepania kutengeneza video kali itakayoifunika ile ya Chura ya msanii Snura Mushi iliyopigwa marufuku kuoneshwa. Akichonga na Risasi Vibes, Tiko alisema anaandaa video kali ya wimbo wake wa Watu ambayo ndani yake kutakuwa na kukata mauno ya kufa mtu kuliko ile ya Snura. “Itakuwa ni video ambayo haijawahi kutengenezwa hapa Bongo, ni hatari yaani, ninachowaomba mashabiki ni kuisubiri kwani ‘soon’ itashuka,” alisema msanii huyo na kuongeza kuwa hata hivyo, haitakuwa iliyokosa maadili.

Jinsi Vyakula Vinavyosababisha Magonjwa

Image
Jarida la Emerging Infectious Diseases linasema kwamba zaidi ya magonjwa 200 yanaweza kusababishwa na chakula. Hata hivyo, vijidudu vinavyosababisha magonjwa hayo yote si vingi sana. Huenda takwimu zifuatazo zinaweza kufanya mtu afikiri hivyo. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), kila mwaka watu milioni 130 hivi katika Eneo la WHO huko Ulaya wanaambukizwa magonjwa yanayosababishwa na chakula. Katika mwaka wa 1998, zaidi ya watu 100,000 nchini Uingereza walikuwa wagonjwa kwa sababu ya kula chakula kibaya, na 200 kati yao walikufa. Inakadiriwa kwamba kila mwaka watu milioni 76 hivi wanapata magonjwa yanayosababishwa na chakula huko Marekani, na   325,000 kati yao hulazwa hospitalini, na 5,000 hufa. Si rahisi kujua hesabu kamili ya ulimwenguni pote. Hata hivyo, shirika la WHO linaripoti kwamba watu milioni 2.2 hivi walikufa kutokana na magonjwa ya kuharisha katika mwaka wa 1998, na milioni 1.8 kati yao walikuwa watoto. Ripoti hiyo inasema: “Wengi kati ya wagon

Mrembo abakwa, auawa!

Image
Mrembo Sijaona Issa Na Gladness Mallya, RISASI MCHANGANYIKO CHALINZE: Inauma sana! Mrembo Sijaona Issa (25) mkazi wa Pela, Chalinze mkoani Pwani, amebakwa na kuuawa kikatili na watu wasiojulikana, ingawa yapo madai ya wivu wa kimapenzi. Akizungumza kwa uchungu, mama mzazi wa marehemu alisema kuwa tukio hilo lilitokea wiki iliyopita baada ya wasamaria wema kukuta mwili wa mwanaye umelazwa uwanjani ukiwa umefunikwa na kanga moja. Mama wa Marehemu “Jumanne jioni marehemu alirudi kutoka kazini saa tatu usiku, akala chakula kama kawaida na kuingia chumbani kwake na sikujua kama alitoka mpaka asubuhi ya saa moja Alhamisi, ambapo kuna kijana alikuja na kuniuliza kama marehemu yupo ndani, nikaenda chumbani kwake sikumkuta, nilikuta tu nguo zake alizotoka nazo kazini na viatu. “Baada ya kurudi na kumwambia hayupo ndipo huyo kijana alisema amekutwa ameuawa uwanjani karibu na Tanesco, ndipo kaka yake akaenda kumuangalia na kukuta kweli ni yeye,” alisema mama huyo.

MKUTANO WA USHIRIKIANO WA VYOMBO VYA HABARI KATI YA NCHI ZA AFRIKA NA CHINA UNAOFANYIKA MJINI BEIJING CHINA

Image
  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akieleza jinsi Tanzania ilivyofanikiwa kuhama kutoka mfumo wa urushaji wa matangazo ya Televisheni kutoka Analogia kwenda Digitali katika mkutano wa tatu wa ushirikiano wa vyombo vya Habari kati ya nchi za  Afrika na China unaofanyika Beijing nchini China.   Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (Kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel wakiwa katika ukumbi wa mikutano leo kabla ya kufunguliwa kwa mkutano wa tatu wa ushirikiano wa vyombo vya Habari kati ya nchi za  Afrika na China unaofanyika Beijing nchini China.   Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (Katikati), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Star Media Tanzania Liao Lanfang wakibadilishana mawazo leo  kabla ya kufunguliwa kwa mkutano wa tatu wa ushirikiano wa vyombo vya Hab

Kitwanga afunguka kwa mara ya kwanza, kutua bungeni wiki ijayo

Image
ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema yupo imara na amerejea nchini akiwa na matumaini mapya. Pamoja na hali hiyo, amesema kuwa hivi sasa anajipanga kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha anaisaidia nchi pamoja na wapigakura wake na kuwa na maendeleo ya kweli na Jumatano ya Julai 29, ataripoti bungeni. Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana baada ya kurejea akitokea nchini Israel ambako alikwenda kwa shughuli zake binafsi. Alisema licha ya mtihani uliomkuta, kwa sasa yupo imara kwa ajili ya kuwatumikia wapigakura wake kwa kuwawakilisha vema ndani ya Bunge. “Niko imara kabisa na nina nguvu na matumaini mapya, nimeingia nchini jana (juzi) nikitokea nchini Israel ambako nilikuwa na shughuli zangu binafsi. Unajua mimi ni mtaalamu (wa mawasiliano) na wewe unajua kabla sijaingia kwenye siasa nilikuwa nafanya nini. “Kifupi ninasema nilikwenda Israel kwa shughuli zangu binafsi kabisa ambazo kwa kipindi cha wiki tatu nilizokuwa huko ni

Ugomvi wa wabunge wa CCM na UKAWA wafikia pabaya

Image
Sakata la wabunge wa Ukawa kususa vikao vya Bunge vinavyoongozwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson limefika pabaya baada ya baadhi ya wawakilishi hao kuanza kutowasalimia baadhi ya wabunge wa CCM. Hatua hiyo ilikuwa dhahiri jana baada ya Ukawa kutangaza kuwa hawatashirikiana na wabunge wenzao wa chama tawala katika shughuli za kawaida za kijamii, kama vile michezo na kutumia kantini ya Bunge, wakisema wenzao wameanza kuwabagua. Mbali na kitendo hicho, wabunge hao pia walitoka kimyakimya bungeni baada ya Dk Tulia kuingia, lakini safari hii hawakufanya mbwembwe za kujiziba midomo kama walivyofanya juzi. Jana asubuhi, mbunge wa CCM  Kangi  Lugola alisema  kuwa alisikitishwa  baada ya kudai kuwa Mbunge wa Chadema (Viti Maalumu), Lucy Magereli hakumjibu salamu yake wakati akiingia bungeni licha ya kumsalimia mara tatu na kuwa katika umbali mfupi wa kusikika. “Kusalimia ni jambo la utamaduni wetu. Nilikuwa namsalimia mbunge wa kike wa Ukawa, lakini hakujibu. Lakini,

Mwalimu aporwa bodaboda, auawa!

Image
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji. Na Stephano Mango, RISASI MCHANGANYIKO RUVUMA: Mwalimu wa shule ya msingi Lupapila iliyopo kata ya Subira, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, Christopher Ndimbo (29) wiki iliyopita aliporwa pikipiki yake na baadaye kuuawa kwa kukatwakatwa na mapanga na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji, mwili wa marehemu ulikutwa katika Mtaa wa Making’inda, Kata ya Msamala mkoani hapa saa 12 jioni, Juni 14, mwaka huu ukiwa umekatwakatwa na kitu chenye ncha kali, baada ya kuwa ametoweka nyumbani kwake, Mtaa wa Mji Mwema, tangu Juni 11, mwaka huu. Kamanda Mwombeji alisema marehemu ambaye pia alikuwa akijishughulisha na biashara ya bodaboda, alikuwa na pikipiki yake aina ya Sanlg, yenye namba za usajili MC 762 ACK  ambayo imetoweka. “Mara ya mwisho marehemu alionekana akiwa katika maeneo ya Uhuru Pub iliyopo kandokando ya uwanja wa michezo wa Majimaji majira ya saa 2

Siwema amuumbua Nay

Image
Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ mama mtoto wake, Siwema Edison NA MUSA MATEJA, RISASI MCHANGANYIKO SIKU chache baada ya mzazi mwenzake na msanii Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego,’ Siwema Edison kutoka gerezani na kutakiwa atumikie kifungo cha nje, amefunguka ya moyoni huku akimuumbua ‘zilipendwa’ wake huyo aliyekuwa akidai alipambana kumsaidia. Siwema Edison Chanzo makini cha habari hii kilitutonya hivi karibuni kuwa, mbwembwe zote alizokuwa akizitoa Nay kuwa yeye ndiye kila kitu mpaka Siwema akarejea uraiani, si za kweli na zimemuumiza msichana huyo, kwani hakufanya chochote kumsaidia kwenye janga hilo. “Siwema analalamika sana, anaumizwa na majigambo ya Nay kuwa jitihada zake ndiyo zimemrejesha uraiani kitu ambacho si cha kweli. Ndugu wa Siwema walikuwa ndiyo kila kitu kufanikisha mtoto wao anaondoka kwenye majanga hayo, sasa hata haieleweki kwa nini Nay ameamua kuongea uongo kiasi hicho kwenye ‘midia’,” kilifu-nguka chanzo hicho. Baada ya gazeti

Breaking Newzzz…..Mwingine adakwa kwa kumkashifu Rais Magufuli kwenye mtandao wa “Whats App”

Image
Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais kwenye mtandao wa WhatsApp. Hapa cha muhimu ni kujuwa sheria hii inafanya kazi, inakamata, inahukumu na kufunga wananchi. Tutumie lugha ya staha, vijana hamko salama kwenye fb, twitter na WhatsApp…sheria ya mitandao ipo na inazunguka kama Simba aungurumae akitafuta mawindo. ========= Leonard Mulokozi Kyaruzi amefunguliwa mashtaka kwa kumkashifu Rais John Pombe Magufuli kupitia mtandao wa WhatsApp tarehe 2 Juni 2016. Kyaruzi anatuhumiwa kutenda kosa hilo akiwa jengo la Tanzanite jijini Dar es Salaam ambapo aliandika “Hivi huyu Pombe ni kwamba hana washauri? Hashauriki? Au ni zuzu? Bwege sana huyu jamaa, he doesn’t consider the law in place before opening his mouth!. Au na yeye anaumwa ugonjwa wa Mnyika?” Ilisema sehemu ya hati ya mashtaka.

Mhariri wa Gazeti la Dira na Mwandishi wake Wapandishwa Kortini

Image
MAHAKAMA  ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewapandisha kizimbani, mhariri na mwandishi wa gazeti la Dira ya Mtanzania, Musa Mkama na Prince Newton kwa kosa moja la kuandika habari za uongo zilizoleta mtafaruku kwa jamii. Akisoma hati ya mashtaka jana mbele ya Hakimu Respicius Mwijage, Wakili wa serikali, Timon Vitalis na Hellen Mushi, alidai mahakamani hapo kuwa, mnamo Juni 20 katika eneo la Biafra Kinondoni, Jijini Dar es Salaam washtakiwa hao waliandika na kuchapisha habari za uongo katika gazeti la ‘Dira ya Mtanzania’ toleo la 424 la tarehe 20 hadi 26 ambazo zilisababisha hofu na mshtuko kwa jamii kwa kutoa taarifa za uongo kuwa ’Kifaru cha kivita cha Jeshi la Wananchi(JWTZ), chaibwa.’ Alidai kuwa kitendo hicho ni kosa kisheria na ni kinyume na sheria ya magazeti. Wakili Vitalis alidai kuwa, upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Hata hivyo, washtakiwa hao walikana shtaka hilo na Hakimu Mwijage al

DK. JIM JAMES YONAZI ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MTENDAJI WA MAGAZETI YA SERIKALI (TSN)

Image

Nafasi ya Kazi Stamigold

Image
STAMIGOLD COMPANY LIMITED EMPLOYMENT OPPORTUNITY ‘STAMIGOLD Company Limited -Biharamulo Mine is a subsidiary company of the State Mining Corporation (STAMICO) operating a gold mine. The Mine is located in the Biharamulo Forest Reserve South West of Mwanza in Kagera Region. In order to run the mine effectively and efficiently, the Company invites applications from qualified candidates to fill the existing vacancy as detailed below THE ROLE: Work Station: Biharamulo Mine Site Work Roster: 6/3 (42 days on, 21 days off) Contract Duration: Not exceeding two years, subject to renewal SENIOR SUPPLIES OFFICER (01) The Senior Supplies Officer-will be reporting to the Procurement Superintendent and should ensure effective supplying of goods and services in response to internal needs by providing support, ,guidance and professional advice within the requirements of the Procurement and Supplies Professionals and Technician Board (PSPTB) and Public Procurement Regulatory A

Mahakama Yagomea Pingamizi la Mbowe kwa Jeshi la Polisi

Image
KESI ya madai iliofunguliwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ya kuiomba mahakama kupiga marufuku zuio la Polisi, leo limetupiliwa mbali. Mbowe alifungua kesi hiyo namba 79 ya mwaka 2016, baada ya hivi karibuni Jeshi la Polisi  kupiga marufuku mikutano ya hadhara kwa madai kwamba, hali ya usalama nchini si salama. Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai, Kilimanjaro katika shauri hilo, aliwashtaki Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa madai wanahusika kuzuia kufanyika kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa. Mbowe ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, walitangaza kufanya oparesheni iliopewa jina ‘Okoa Demokrasia nchini’ iliyokuwa na lengo la kuishtaki serikali kwa wananchi kwa kile alichodai, kuendesha nchi bila kufuata katiba ya nchi. Hata hivyo, baada ya kupigwa marufuku kwa maandamano, Mbowe alifungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya M

Mdosi mbaroni kwa ujambazi Moshi

Image
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, ACP Wilbroard Mtafungwa. Issa Mnally na Richard Bukos, UWAZI DAR ES SALAAM: Watu watatu akiwemo mmoja mwenye asili ya Kiasia ‘Mdosi,’ wametiwa mbaroni na polisi Moshi mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za ujambazi, Uwazi limeezwa. Akizungumza na waandishi wetu kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, ACP Wilbroard Mtafungwa alisema kuwa watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi hilo baada ya kukamatwa kutokana na ushirikiano wa polisi na raia wema. Akielezea jinsi polisi walivyowanasa watuhumiwa hao, Kamanda Mtafungwa alisema kuwa walimkamata kwanza mmoja Fredil Guston maarufu kwa jina la Chedieli ambaye ni mkazi wa Majengo, Moshi. Aidha, alisema Chedieli aliwataja wenzake ambao ni Frank Nkya maarufu kwa jina la Chabufa na Frank Mbesanyo Domani ‘Ausho’ mkazi wa Pasua na walipopekuliwa walikutwa na vitu kadhaa vya wizi. “Sasa hawa wakamtaja bosi wao ambaye ni kiongozi wao mkuu wa

Majibu ya Hoja za Wabunge Yaliyotolewa Jana na Waziri wa Fedha

Image
JUNI 20, 2016 DODOMA UTANGULIZI Mheshimiwa Spika, napenda kutumia fursa hii kukushukuru wewe binafsi, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa kuendesha vizuri majadiliano kuhusu Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa 2015 na Mpango wa Maendeleo wa 2016/17 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2016/17, niliyowasilisha tarehe 8 Juni, 2016. Mheshimiwa Spika, Kipekee, ninampongeza sana Mhe. Naibu Spika kwa umahiri na weledi wa hali ya juu alioonesha katika kusimamia Kanuni za Bunge wakati wote wa kikao hiki cha Bunge la bajeti. Hakika viwango vyake ni vya kimataifa. Japokuwa Mhe. Joseph Kakunda, mwanafunzi wangu Idara ya Uchumi Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam alichomekea sehemu fulani akidai kwamba mimi ni bahiri, (nadhani alimaanisha bahiri wa kutoa maksi za upendeleo!), nataka niliambie Bunge lako tukufu kwamba kwa viwango ambavyo Mhe. Naibu Spika alivyoonesha humu ndani, hakika ningempa maksi za haki asilimia 100 kama walivyofanya maprofesa