Posts

Video Mpya : DIAMOND PLATNUMZ Ft RAYVANNY - IYENA....VIDEO QUEEN NI ZARI THE BOSSLADY

Image
Msanii Diamond Platnumz ametoa video ya nyimbo yake iliyoko kweny album ya 'A Boy from Tandale' akimshirikisha msanii mwenzake kutoka WCB Rayvanny. Pia Video Queen wa Iyena ni Zari The bosslady Itazame hapo chini

MCHUNGAJI ATAFUNWA NA MAMBA AKIBATIZA ZIWANI

Image
MCHUNGAJI ambaye aliyekuwa akiendesha ibaada ya kubatiza waumini ufukweni mwa ziwa amefariki baada ya kushambuliwa na mamba wakati akibatiza Kusini mwa Ethiopia. Mchungaji huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Docho Eshete alikuwa akiendesha ibaada hiyo ya waumini 80 siku ya Jumapili iliyopita katika ufukwe wa Ziwa Abaya katika mji wa Arba Minch wilaya ya Merkeb Tabya. Wakazi wa mji huo waliliambia shirika la utangazaji la BBC kwamba Mamba huyo aliruka kutoka ndani ya maji wakati mchungaji huyo akiwabatiza waumini na kumng’ata miguu,mgongo na mikono majeraha yaliyosababisha kifo chake.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya watu 10 Kigoma

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya watu 10 baada ya basi walilokuwa wanasafiria kugonga Treni ya mizigo Mkoani Kigoma huku akitoa maagizo kwa wadau wa usalama kuwachukulia hatua madhubuti kuzuia ajali hizo.         Soma taarifa kamili:

Serikali Yalitaka Baraza la Maaskofu KKKT Kuufuta Waraka wa Pasaka

Image
SERIKALI ya Tanzania imelitaka Baraza la Maaskofu la Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Tanzania kufuta waraka lililoutoa wakati wa mfungo wa kwaresma kwa madai kuwa Baraza hilo halina mamlaka kisheria ya kutoa waraka huo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Msajili wa Vyama, imesema kuwa imethibitisha kuwa uongozi wa Kanisa hilo umeshindwa kutimiza masharti ya usajili, kutoa taarifa za fedha na kutoa taarifa za mabadiliko mbalimbali kinyume na sheria. Serikali imemtaka Askofu Mkuu wa KKKT kufika ofisi ya msajili ili apewe madeni na malimbikizo yake yanayopaswa kulipwa ndani ya siku 7 (kuanzia Mei 30, 2018). Taarifa ya Serikali inaeleza kuwa Katiba inayotumiwa na Kanisa hilo ni ya mwaka 1960 ambayo ilipitishwa na msajili mwaka 1963. Hivyo Serikali inalitaka Kanisa hilo kuomba kibali cha kufanya marekebisho ya katiba hiyo.

Tanzia: Mbunge Majimarefu amefiwa na Mkewe

Image
Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu 'Profesa Majimarefu’ leo Jumatano Juni 6, 2018 amefiwa na mkewe aliyekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Akizungumza na MCL Digital leo Mkurugenzi wa mawasiliano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha amethibitisha kifo cha mke wa mbunge huyo, kubainisha kuwa aliaga dunia saa 3 asubuhi. Spika wa Bunge, Job Ndugai akizungumza na MCL Digital, amempa pole Ngonyani pamoja na familia yake. “Ni kweli amefariki, tumepata taarifa hizo si muda mrefu leo na alikuwa amelazwa kwa muda mrefu katika pale Muhimbili ICU (chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum). Maofisa wa Bunge wakiwa na Ngonyani wako pale wanaendelea kutoa msaada wa karibu kabla ya kuendelea na taratibu nyingine,” amesema Ndugai. “Na kwa sababu huyu mama pia alikuwa ni diwani kule Korogwe, Bunge na halmashauri ya Korogwe vijijini tutashirikiana kwa pamoja lakini kwa sasa tunaendelea kuwasiliana na fam

Wachezaji wa Real Madrid waandika haya baada ya Zidane kutangaza kustaafu

Image
Wachezaji wa Real Madrid kwa sasa watakuwa wapo katika wakati mkgumu baada ya kocha wao aliyewapa mafanikio makubwa katika kipindi kifupi Zinedine Zidane, Alhamisi hii kutangaza kustaafu kuifundisha timu hiyo. Wachezaji hao wakiongozwa na Cristiano Ronaldo, Sergio Ramos, Karim Benzema wameonyesha kusikitishwa kwa maamuzi ya kocha huyo na mpaka kushindwa kuzuia hsia zao na kuamua kumuandikia ujumbe wa kuumbuka mchango wake katika kipindi walipokuwa pamoja. Cristiano Ronaldo I’m just proud of being your player. Mister, thanks for so much. Sergio Ramos Mister, as a player and now as a coach, you decided to fire you at the top. Thank you for two and a half years of soccer, work, love and friendship. You leave but your legacy is already indelible. One of the most successful chapters in the history of our beloved @realmadrid As a player and coach you decided to say goodbye at the top. Thank you for two and a half incredible years. Your legacy will never be erased,

Zinedine Zidane kuifundisha timu ya Qatar

Image
Zinedine Zidane ambae alikuwa Kocha wa Klabu ya Real Madrid ameingia mkataba wa miaka minne ya kuifundisha timu ya taifa ya Qatar. Mapema hii leo habari zimeenea kuwa meneja huyo wa Real, Zinedine Zidane atakuwa akilipwa Euro milioni 15 kwa mwaka hii ikiwa na lengo la kuisaidia nchi hiyo inayotarajia kuanda michuano ya kombe la dunia mwaka 2022. Zidane ameiyongoza Real Madrid kwa misimu miwili na nusu, akifanikiwa kutwaa mataji tisa huku Jumamosi iliyopita akiipatia timu yake kombe la klabu bingwa barani ulaya.

Mkataba TanzaniteOne kufumuliwa

Image
WAZIRI wa Madini, Angellah Kairuki, amesema serikali imeagiza leseni ya uchimbaji wa ubia baina ya Shirika la Madini la Taifa (Stamico) na Kampuni ya TanzaniteOne Mining Limited (TML) ili utaratibu mpya uandaliwe kwa manufaa ya pande zote mbili. Aliyasema hayo bungeni jana alipowasilisha hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha. Alisema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kasoro iliyoibuliwa na Kamati Maalum ya Spika Kuchunguza Uchimbaji na Biashara ya Tanzanite katikati ya mwaka jana. “Serikali imeagiza leseni ya uchimbaji wa ubia baina ya Stamico na TML irudishwe serikalini ili utaratibu mpya uandaliwe utakaoiwezesha serikali, TML na mwekezaji wa kimkakati kushirikiana katika uchimbaji, uendeshaji katika mgodi huo kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Madini, Sura ya 123 kama ilivyorekebishwa na Bunge mwaka 2017,” alisema. Alibainisha kuwa mgodi wa ubia kati ya Stamico na TML ni miongoni mwa migodi ya tanzanite iliyopo Mirerani mkoan

WALIOISHIA VETA SASA WANAWEZA KUSOMA ELIMU YA JUU CHUO CHA UFUNDI ARUSHA

Image
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) imethibitisha matumizi ya mtaala unganishi wa masomo ya ufundi nchini utakaowawezesha wahitimu wa vyuo vya Mafunzo ya Ufundi Stadi(Veta) kuendelea na elimu ya juu.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mtaala huo,Mkurugenzi wa Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi nchini,Dk Noel Mbonde amesema utasaidia kuwapa fursa vijana wengi waliotamani kuendelea na masomo ya ufundi ya juu kunufaika. Amesema serikali inathamini maboresho hayo yanayotoa nafasi ya kuwanoa wataalamu wa kutosha inayoenda sambamba na sera ya serikali ya awamu ya tano ya kufikia uchumi wa viwanda. Mkurugenzi wa Ufundi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Standi nchini,Dk Noel Mbonde akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mtaala Unganishi katika Chuo cha Ufundi Arusha(ATC)jijini Arusha ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ufundi(ATC),Dk Erick Mgaya. “Kulikua na tatizo la wanafunzi wetu wanaohitimu Veta kuendelea na kozi za juu za ufundi na sababu kubwa ilikua ni kukoseka

Tanzia: Mama wa Mbunge Hussein Bashe Afriki Dunia

Image
Mama mzazi wa Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini mkoani Tabora (CCM), Hussein Bashe amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Ijumaa, katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Muhumbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa. Kupitia akaunti yake ya Twitter, Bashe amesema; “Ndugu zangu nimeondokewa na mama yangu mpendwa. Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un.” Taarifa zaidi zitafuata baadaye.

ORODHA YA WAHITIMU KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA JKT

Image
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) , limefanya uteuzi wa wanafunzi waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita kutoka shule zote za Tanzania Bar a kwa mwaka 2018, kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa Sheria. Sanjari na uteuzi huo, JKT limewapangia Makambi ya JKT watakayokwenda kupatiwa mafunzo kwa muda wa miezi mitatu na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 01-10 June 2018. Wahitimu hao, wamepangiwa katika Kambi za JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu – Pwani, JKT Makutupora – Dodoma, JKT Mafinga – Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba – Tanga, JKT Makuyuni – Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa, Nachingwea- Lindi na JKT Mtabila – Kigoma. Aidha, wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (physical disabilities) wanatakiwa kuripoti kambi ya Ruvu JKT iliyopo mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia wa jamii hiyo. Vijana watakaochaguliwa watatakiwa kujigharamia nauli za kwenda na kurudi kwenye makambi ya JKT w

Mwanafunzi aunda gari linalobadili jua kuwa Umeme

Image
Mwanafunzi mmoja nchini Kenya ameunda gari linalotumia kawi ya jua, gari ambalo limekuwa likiwavutia watu kutokana na kubadili jua kuwa umeme. Samuel Karumbo, 30, ni mwanafunzi katika chuo cha mafunzo anuwai cha serikali mjini Kitale, Magharibi mwa Kenya, amesema gari lake, ambalo lina mitambo mitatu ya sola iliyobandikwa, linaweza kusafiri umbali wa kilomita 50 kwa siku. Karumbo anasema mchana, sola huchukua nishati ya jua na kuibadilisha kuwa umeme ambao unahifadhiwa kwenye betri ambazo ndizo zinazotumiwa moja kwa moja kuliendesha gari hilo na pia wakati jua halijawaka sana. Gari hilo lina uzani wa kilo 120 na kwenye mteremko hutumia mvuto wa nguvu za ardhi badala ya umeme. Nguvu hutumia tu kwenye kupanda milima au maeneo yenye miinuko.

Mbwana Samatta Afanya Ziara Makka

Image
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, na mchezaji wa timu ya Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta (kulia) akiwa msikitini Makka. …Akiwa na mchezaji mwenzake wa timu ya Genk,  Omar Colley. Nahodha wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta,  anayekipiga katika timu ya Genk ya nchini Ubelgiji baada ya kumaliza msimu wa ligi kuu nchini humo,  ameelekea nchini Saudia Arabia kwa ajili ya kufanya ziara ya kidini huko Makka. Samatta anatarajiwa kurudi Tanzania mwishoni mwa wiki hii kujiandaa na mchezo wa hisani kati yake na mwanamuziki Alikiba katika mchezo wa soka utakaofanyika Juni 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa taifa kati ya Timu Alikiba dhidi ya Timu Samatta.

Kauli Ya Kitila Mkumbo Kuhusu Katibu Mpya wa CCM

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo. Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Bashiru Ally ni mtu sahihi kwa zama za sasa kuwa katibu mkuu wa chama hicho tawala. Jana Halmashauri Kuu, ambayo ni chombo cha pili kwa ukubwa cha CCM ilikutana kwa siku mbili Ikulu jijini Dar es Salaam, na kumpitisha msomi huyo ambaye aliongoza kamati iliyohakiki mali za chama hicho kwa miezi mitano, kuwa katibu mkuu. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter Profesa Mkumbo amesema , “katika kipindi ambacho silaha ya siasa ni nguvu ya hoja, weledi, na uimara CCM imepata katibu mkuu sahihi kwa zama sahihi nakutakia mafanikio makubwa komredi Dk Bashiru Ally.” Uteuzi huo umekuja baada ya aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana kuandika barua ya kujiuzulu kwa mwenyekiti wa chama hicho, Rais John Magufuli.

Kimenuka! Fumanizi la Mwezi Mtukufu Laibua Ndoa Mpya!

Image
Mke wa Sele Gogo, Shani ldd (mwenye dela lenye rangi nyekundu na nyeupe) akiwa na kundi lake nje ya chumba cha Mwajabu, KUNA mambo ya ajabu ya kila aina ambayo hutokea kwa nyakati tofauti, lakini hili lililojiri katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, ni kali zaidi. Mke wa mfanyabiashara maarufu wa unga wa sembe mjini hapa, Seleman Husein almaarufu Sele Gogo aliyefahamika kwa jina la Shani Idd, anadaiwa kuzua timbwili zito katika tukio la fumanizi. Timbwili hilo la fumanizi linatajwa kutibua ndoa ya wawili hao kisha kuibua ndoa mpya kati ya Sele Gogo na mwanamke aliyedaiwa kufumwa naye, Mwajabu Juma ambaye baada ya kizaazaa hicho aliamua kufunga naye pingu za maisha. Kwa mujibu wa mashuhuda, fumanizi hilo lililojaza umati lilijiri kwenye chumba cha Mwajabu kilichopo Mtaa wa Makaburi B Kata ya Mji Mpya mjini hapa wakati wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.     Sele Gogo na Mwajabu wakiwa kwenye pozi baada ya kufunga ndoa, Mashuhu

Nape atoa ujumbe mzito wa kumuaga Kinana

Image
Mbunge wa Mtama, na Mjumbe wa Kamati Kuu CCM, Nape Nnauye amemaga na kumuahidi aliyekuwa Katibu wa chama chao, Ndg Abdulrahman Kinana aliyestaafu leo kuwa wataendelea kumuenzi na mbegu aliyopanda itaota. Nape ametoa ahadi hiyo kwa Kinana ikiwa ni muda mfupi baada ya kiongozi huyo kutangaza kustaafu nafasi hiyo na kukubaliwa na Mwenyekiti wa Chama hicho na Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli. Pamoja na hayo Nape ameweka wazi kumtambua kinana kama mwalimu uliyebadili mtazamo wetu juu ya siasa na utumishi kwa umma. "Pumzika rafiki wa kweli, pumzika Mlezi na Mzazi usiyemfano, pumzika Kiongozi, pumzika Komredi.  Mwalimu uliyebadili mtazamo wetu juu ya siasa na utumishi kwa umma! Umepanda mbegu na itaota,"

MKE AMUUA MUMEWE KISA WIVU WA MAPENZI KAGERA

Image
Victoria Salvatory (58), mkazi wa kata ya Katoma, Kagera anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mumewe, Salvatory Iteganira (62) kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi. Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Augustino Ollomi amesema mauaji hayo yalitokea jana saa 6:00 mchana. Akizungumza leo Mei 28, Kamanda Ollomi amesema mtuhumiwa anadaiwa kumpiga mumewe kwa kitu kizito kichwani na kumsababishia jeraha lililovuja damu nyingi na hatimaye kifo. “Wanandoa hao wanadaiwa kuwa na ugomvi ambao chanzo chake tunaendelea kuchunguza; baada ya ugomvi huo mtuhumiwa alimpiga mume wake kichwani kwa kitu kizito kilichosababisha jeraha lililovuja damu nyingi na kusababisha kifo chake,” amesema Ollomi. Kamanda huyo amewaasa wanandoa na wapenzi kutumia njia ya majadiliano, usuluhishi na sheria kutatua tofauti miongoni mwao badala ya kujichukulia sheria mikononi. Matukio ya hivi karibuni ya mauaji ya wanandoa ni pamoja na la Muuguzi mfawidhi msaidizi wa hos

Maafisa wakuu wakamatwa kwa tuhuma za ufisadi.Kenya

Image
Mkuu wa Shirika la Vijana wa Huduma kwa Taifa nchini Kenya (NYS) Richard Ndubai, pamoja na maafisa wengine wakuu, wamekamatwa na polisi kwa tuhuma za ufisadi. Hii inafuatia agizo la Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Umma aliyeagiza kushtakiwa kwa washukiwa wote waliotajwa katika kashfa ya Shilingi bilioni 9. Maagizo ya Mkurugenzi wa mashtaka ya Umma Noordin Haji yametolewa baada ya kupokea taarifa kuhusu kampuni 10 na pia zaidi ya watu 40 binafsi waliotajwa katika sakata hiyo NYS scandal kutoka kwa Mkurugenzi wa uchunguzi wa Uhalifu George Kinoti. "Mkurugenzi mkuu wa Mashtaka ya Umma amechunguza nyaraka zinazohusiana na sakata inayoendelea katika NYS na ameagiza mashtaka yafunguliwe mara moja dhidi ya wite waliotajwa kushukiwa ," iliandika ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma kwenye ukurasa wake wa Twitter Jumatatu asubuhi. Washukiwa wengine kadhaa pia wamekamatwa na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani katika kipindi cha saa 24, kulingana na afisa mmoja katik

Kesiha Ateuliwa Mjumbe Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM

Image
 MSANII wa Bongo Fleva, Khadija Shabani Taya maarufu kwa jina la ‘Keisha’ ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM (NEC) leo, Jumatatu, Mei 28, 2018.  Taarifa ya uteuzi huo imetolewa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole kufuatia Mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho uliofanyika leo, Ikulu jijini Dar es Salaam. Keisha ambaye aliwahi kutamba kwa ngoma yake ya uvuymilivu na nyingine, aliwapi pia kuwania Ubunge wa Viti Maalum (CCM) mkoa wa Dodoma na kushinda katika kura za maoni. Kabla ya uteuzi huo wa leo, alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM.

BREAKING NEWS: KINANA ANG’ATUKA UKATIBU MKUU CCM

Image
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Abdulrahman Kinana ameng’atuka katika nafasi yake hiyo ndani ya CCM huku Halmashauri Kuu ya chama hicho ikiridhia ombi hilo rasmi. Hayo yamewekwa wazi na taarifa ilizotolewa na Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole leo Mei 29, 2018 na kusema kwa pamoja wamemtakia mafanikio mema katika shughuli zake. “Napenda kumshukuru ndugu Kinana kwa utumishi wake katika Chama cha Mapinduzi (CCM) na CCM itaendeleaq kutumia uzoefu wake katika majukumu mbalimbali ya chama kwa kadiri itakavyohitajika” , imesema taarifa hiyo. Kwa upande mwingine, Kinana wakati anatoa neno lake la kuwaaga wajumbe wa NEC amewasisitizia wajumbe hao na wana CCM kiujumla kudumisha umoja wa wanachama na chama cha mapinduzi (CCM).