Zinedine Zidane kuifundisha timu ya Qatar

Zinedine Zidane ambae alikuwa Kocha wa Klabu ya Real Madrid ameingia mkataba wa miaka minne ya kuifundisha timu ya taifa ya Qatar.

Mapema hii leo habari zimeenea kuwa meneja huyo wa Real, Zinedine Zidane atakuwa akilipwa Euro milioni 15 kwa mwaka hii ikiwa na lengo la kuisaidia nchi hiyo inayotarajia kuanda michuano ya kombe la dunia mwaka 2022.

Zidane ameiyongoza Real Madrid kwa misimu miwili na nusu, akifanikiwa kutwaa mataji tisa huku Jumamosi iliyopita akiipatia timu yake kombe la klabu bingwa barani ulaya.

Comments

Popular posts from this blog