Posts

HAMISA MOBETO KUZAA NA BWANAKE… ZARI THE BOSS LADY ATINGA BONGO KUPATA UKWELI

Image
                      Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ . BAADA ya maneno mengi kusemwa Bongo kufuatia madai ya bwana’ke kuzaa na mwanamitindo mwenye jina kubwa, Hamisa Hassan Mobetto, mwanamama mjasiriamali mwenye jina kubwa Afrika Mashariki, Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuendelea kuliamsha dude baada ya kutinga Bongo na kuanza kudodosa ili kupata ukweli wa ishu hiyo. Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni makini, awali Zari alitinga Bongo mapema wiki iliyopita na kupigwa chabo na ‘wadakuz’ AKIWA KATakiwa nyumbani kwa jamaa huyo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva huko Madale jijini Dar. Akiwa katika pozi. Ilidaiwa kwamba, hata hivyo, hakukaa sana kwani aliondoka kwenda kwenye kumbukumbu ya siku 40 za kifo cha mama yake, Halima Hassan nchini Uganda kabla ya kurejea Bongo wikiendi iliyopita.             Kwa taarifa yenu Zari amejaa tele Bongo na lengo lake ni kuchimba na kupata ukweli juu ya madai ya Hamisa kuzaa na bwana’ke.Unajua akiwa

Polisi wamkamata Mtekaji Watoto

Image
POLISI mkoani Geita kwa kushirikiana na wenzao wa Mkoa wa Arusha wamemtia mbaroni mtuhumiwa wa utekaji watoto akiwa na mtoto mwenye umri wa miaka miwili katika nyumba ya kulala wageni ya Shitungulu, Katoro Wilaya na Mkoa Geita aliyekuwa akimshikilia akidai apewe Sh milioni nne. Samson Peter amekamatwa usiku wa kuamkia jana baada ya timu maalumu ya Polisi ya askari tisa, watano kutoka Arusha wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi Amani na wa Geita askari wanne wakiongozwa na Mkaguzi wa Polisi, James, kuizingira nyumba ya wageni aliyokuwa amejificha mtuhumiwa na mtoto aliyemteka tangu Septemba Mosi. Akithibitisha hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo alisema mtuhumiwa alikamatwa saa mbili usiku juzi katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Shitungulu katika Mtaa wa California, Kata ya Katoro wilayani Geita akiwa chumba namba 11 na mtoto huyo Justine Ombeni (2) aliyemteka, akiwa hai na afya njema. Kamanda Mwabulambo alisema mtoto huyo alitekwa Sept

Mbunge Mteule Viti Maalum CUF, Bi Hindu Mwenda Azikwa

Image
Mwili wa marehemu Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda, aliyefariki nyumbani kwake Kibada Kigamboni ukiwasili makaburi ya Kisutu Dar leo. Maziko yakiendelea. Sheikh (kulia) akifanya  maombi baada mazishi. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (katikati) akiwa katika mazishi hayo. …Akiongea  na wanahabari baada ya maziko. HATIMAYE Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda ,  aliyefariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake Kibada Kigamboni amezikwa leo makaburi ya Kisutu Dar na mamia ya wafuasi wa chama chake na wananchi wengine wa Dar es Salaam. Sheikh aliyeongoza mazishi hayo aliwahimiza wanachama wa Cuf kuendeleza upendo na kufanya kazi kwa ushirikiano ambapo miongoni mwao ni mwenyekiti wa chama hicho anayetembuliwa na Msajili wa Vyama, Profesa Ibrahim Lipumba. Lipumba alimsifia marehemu akisema alikuwa anajituma katika kazi zake na alikuwa mwanachama shupavu na alikuwa mfano kwa wanachama wengine wanaokipenda cha

Uhuru Kenyatta Ampa Onyo Raila Odinga

Image
Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta. Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta a mefunguka na kutoa onyo kwa mpinzani wake Raila Odinga kuwa asahu kuhusu tume mpya ya uchaguzi lakini pia amemtaka Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga kutoingilia kwani wao wameheshimu maamuzi ya mahakama. Uhuru Kenyatta mpinzani wake Raila Odinga (kushoto). Uhuru Kenyatta amesema chama chake cha Jubilee kipo tayari kwa uchaguzi huo wa marudio na sasa wanasubiri Tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC iweze kutangaza siku ya uchaguzi na wanaiomba itangaze siku hiyo haraka. Aidha Uhuru Kenyatta amesema kuwa wapinzani hao hawana haja ya uchaguzi bali ni watu ambao wanataka serikali ya mseto kitu ambacho yeye hawezi kukiruhusu hata kidogo Mahakama ya juu nchini Kenya Septemba 1, 2017 ilifuta matokeo ya Urais nchini Kenya na kuamuru kuwa uchaguzi mpya ufanyike katika nafasi ya Urais kutokana na mahakama hiyo kubaini baadhi ya mapungufu wakati wa utoaji wa matokeo hayo ya uchaguz

Waziri Mkuu Majaliwa atoa suluhisho la ajira

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watendaji katika mikoa yote nchini kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya viwanda katika maeneo yao kwani  vitasaidia katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana. Waziri Mkuu alipozungumza na watendaji na wananchi wa mkoa wa Morogoro amesema mpango wa Serikali wa kujenga uchumi wa viwanda ambao unalenga kuinua uchumi wa Taifa kutoka wa chini kwenda uchumi wa kati, hivyo ni muhimu kuvifuatilia. “Viwanda hivi vinatupa uhakika wa ajira nchini kwa vijana kwa sababu vinauwezo wa kuajiri watu wengi na wa kada mbalimbali, hivyo ni muhimu tukafuatilia utendaji wake. Lakini mbali na kutoa ajira nyingi, pia viwanda vitawezesha wakulima kupata soko la uhakika la mazao yao na kukifanya kilimo kuwa na tija," Mhe. Majaliwa. Pamoja na hayo Majaliwa ameongeza na kusema kwamba muda mrefu sekta ya viwanda nchini ilikuwa haifanyi vizuri jambo ambalo lilisababisha kuongezeka kwa tatizo la ajira na mazao yalikosa soko. Ha

Wema Sepetu atupa jiwe gizani

Image
 Malkia wa filamu Bongo , Wema Abraham Sepetu ametupa jiwe gizani ambalo bado halijajulikana ni kwenda kwa mtu gani na kumwambia bado wa kumshusha hajazaliwa kwani yeye alivyo ni majaaliwa kutoka kwa maulana na siyo kujitakia. Wema ametupa jiwe hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram na kusema kuna mtu kamuharibia siku hivyo na kumwambia kwamba yeye hakujitakia kuwa alivyo hivyo mtu huyo ajue kutofautisha. "Wa kunizima hajazaliwa bado jamani... Alafu mjue kutofautisha kati ya Kujaaliwa na kujitakia... Alhamdulillah nyingi kwa Maulana wangu... Sikujitakia... Ni majaaliwa tu... To whom it may Concern... Kuna mtu kajua kuniharibia siku wallah... " Wema Sepetu.  Dongo la Wema mtandaoni Aidha Wema ameongeza kwa kusema katu hawezi kujitutumua kwani anaogopa kujiumiza. Vilevile  tukio hilo linaunganishwa moja kwa moja na mtu ambaye Wema Sepetu amemuhisi anataka kujaribu kudukua mtandao wake wa Instagram hali iliyompelekea kumuandikia ujumbe kuwa katu hatam

UCHAGUZI KENYA: Mahakama Kuu imefuta matokeo ya uchaguzi wa urais wa nchi hiyo yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta. Imeamuru uchaguzi urudiwe ndani ya siku 60.

Image
  Mahaka Kuu ya Kenya. IDARA ya Mahakama imesema majaji wa Mahakama Kuu nchini Kenya wameanza kutoa uamuzi  kuhusu kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyowasilishwa na Umoja wa Vyama vya Upinzani (NASA) saa 5:00, leo ambapo ndiyo siku ya mwisho kikatiba kwa mahakama hiyo kutoa uamuzi. Matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi Kulikuwa na wagombea wanane katika uchaguzi wa urais uliofanyika tarehe 8 Agosti mwaka huu. Matokeo ya uchaguzi huo yalitangazwa Ijumaa tarehe 12 Septemba na mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati. Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo: Ekuru Aukot 27,311 (0.18%) Abduba Dida 38,093 (0.25%) Cyrus Jirongo 11,705 (0.08%) Japheth Kaluyu 16,482 (0.11%) Uhuru Kenyatta 8,203,290 (54.27%) Michael Wainaina 13,257 (0.09%) Joseph Nyagah 42,259 (0.28%) Raila Odinga 6,762,224 (44.74%) Waliokuwa wamejiandikisha kushiriki katika uchaguzi huo ni 19,611,423 lakini waliopiga kura walikuwa 15,073,662 ambao ni sawa na asilimia 78.91. Ma

Rais Magufuli atoa samalu ya Eid kwa Waislam

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa salamu kwa waumini wa dini ya Kiislam na kuwatakia sikuu njema ya Eid. Katika ukurasa wake wa twitter Rais Magufuli ametoa ujumbe huo kuwatakia Eid njema, huku akihimiza kudumisha amani, upendo na mshikamano. "Nawatakia Waislamu na watanzania wote sikukuu njema ya Eid el-Hajj, tunaposherehekea sikukuu hii tuendelee kudumisha upendo,amani,umoja na mshikamano wetu. Eid Mubarak", aliandika Rais Magufuli. Waumini wa dini ya Kiislam nchini leo wanaungana na Waislam wenzao wote duniani, kusherehekea sikuku ya Eid ambayo huadhimishwa kila mwaka, mara baada ya ibada ya Hija kukamilika, na mara nyingi husherehekiwa kwa kuchinja wanyama waliohalalishwa kwa binadamu.

Mahakama imeelezwa Sethi wa IPTL Amewekwa Puto Tumboni

Image
Upande wa utetezi umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi amewekewa ‘Puto’ tumboni kutokana na ugonjwa unaomkabili hivyo asipohudumiwa inavyotakiwa anaweza kupoteza maisha. Mbali ya Seth, mwingine ni Mfanyabiashara James Rugemarila ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12, yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya TSh 309,461,300,158. Wakili wa utetezi, Joseph Mwakandege amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mteja wake Seth anatakiwa apelekwe Hospital ya Taifa Muhimbili lakini hadi sasa hajapelekwa na ni dhahiri upande wa mashtaka umedharau amri mbili za Mahakama. ”Ugonjwa uliosababisha Seth atakiwe kwenda Muhimbili ni baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa ambapo tumboni kwake kumewekwa Balloon ‘Puto’ hivyo asipohudumiwa ipasavyo inaweza kusababisha kifo, naomba mshtakiwa apelekwe Muhimbili kwa sababu ni Hospitali ya juu na yenye vifaa na watalaamu wa kuto

Hakimu Akataa Msokoto wa Bangi Kesi ya Wema

Image
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imekataa kupokea ushahidi wa msokoto wa bangi na vipisi viwili vya madawa hayo ya kulevya katika kesi inayomkabili mwigizaji Wema Sepetu . Uamuzi huo umetolewa na Hakimu, Thomas Simba , aliyesema mahakama haiwezi kupokea vielelezo hivyo kwa sababu msokoto wa bangi na vipisi vina kasoro kwa kuwa shahidi hakuvifafanua mahakamani. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 12 mwaka huu.

Serikali yataifisha magari yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria

Image
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetaifisha jumla ya magari sita yakiwepo magari matatu aina ya Ranger Rover Sports yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria baada ya watuhumiwa hao kukiri kuwa wamefanya kosa hilo. Rais Magufuli mwezi Machi mwaka huu alipokwenda bandarini alikuta kuna makontena yenye magari ndani yake huku wamiliki wa makontena hayo wakidai  makontena hayo yalikuwa na nguo na mabegi  lakini baada ya kufunguliwa zilionekana gari za kifahari zikiwa kwenye makontena hayo, jambo ambalo lilionekana wamiliki wa mahari hayo walikuwa wakiingiza magari hayo kinyume na utaratibu na sheria za nchi. Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, DPP Biswalo Mganga amesema kuwa baada ya mahakama kuwakuta na hatia raia hao wakigeni ambao walidai kuwa kontena hizo zilikuwa na nguo na mabegi wakati ni magari hivyo serikali imetaifisha magari yao na sasa kuwa magari ya serikali. "Rais hao wamekiri makosa yao yote mawili na kutokana na kukiri kwao mahakama ime

‘Masogange’ Ana Kesi ya Kujibu Dawa za Kulevya

Image
Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogang aliyevaa gauni la kijani aikitoka mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema kuwa Video Queen , Agnes Gerald ‘Masogange’, anayo kesi ya kujibu kwa kudaiwa kutumia dawa za kulevya, hivyo anapaswa kujitetea. Kesi hiyo ambayo imeunguruma leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, amesema kuwa amekubaliana na hoja za ushahidi wa upande wa mashtaka ambapo mshtakiwa amekutwa na kesi ya kujibu na hivyo ana haki ya kujitetea. Baada ya kauli ya hakimu huyo, Masogange amesema atajitetea kwa njia ya kiapo na atakuwa na mashahidi watatu. Hakimu Mashauri ameiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 12, mwaka huu ambapo mtuhumiwa ataanza kujitetea. NA DENIS MTIMA/GPL

Ridhiwani Kikwete Amvaa Kigwangala

Image
 Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amemvaa Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Khamis Kigwangala na kumwambia anaweza kuwa sehemu ya wachochezi kwa anachokifanya. Ridhiwani Kikwete amebainisha hayo kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya  Mhe. Kigwangalla kuonyesha kusikitishwa na kitendo kilichofanywa na Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma katika kuwafanyia usaili baadhi ya wataalamu waliojitokeza kwenye usaili  wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao umefanyika mapema leo Agosti 30, 2017. "Unaweza dhani unauliza swali kumbe nawe unakuwa sehemu ya wachochezi! Mhe. Waziri unaweza kuwa hujui kusoma lakini picha inatoa jibu sahihi", aliandika Ridhiwani. Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma leo Agosti 30, 2017 ilifanya usaili kwa ajili ya nafasi za kazi katika Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ambapo takribani watu 30,000 walijitokeza huku ikiwa watu 400 pekee ndiyo wanaotakiwa.

Zijue faida za uaminifu katika mahusiano ya Ndoa

Image
Suala la uaminifu katika mapenzi kwa karne hii limekuwa kikwazo kikubwa kwa watu wengi sana, wengi wemekuwa si waaminifu wakati mwingine kupelekea mahusiano hayo kufa. Hivyo uaminifu ni muhimu sana katika mapenzi kwa kuwa katika mahusiano ya kimapenzi kuna faida nyingi kwa mwili na akili. Watu walio katika mahusiano bora ya mapenzi huishi maisha marefu na kufurahia afya njema kuliko wale wasiokuwa katika mahusiano ya aina hiyo. Faida hii haina pingamizi kwa sababu ya ukweli kwamba watu wanaokuwa katika mahusiano ya karibu wanajijengea hisia na nguvu fulani ambayo huwasaidia kusaidiana na kujaliana wakati wa shida. Siyo tu kwamba watu walioko katika mahusiano ya aina hii wanaishi muda mrefu lakini pia ni kweli kwamba wanakuwa na furaha na wanaridhika na maisha kuliko wale wanaoshindwa kukaa katika mahusiano. Pili, kuwa katika mahusiano mazuri ya mapenzi kunasaidia katika mambo mbalimbali ya kimahitaji. Kusaidiana katika mahitaji mbalimbali baina ya wapenzi ni nji

Mobeto Ampukutisha Zari

Image
Hamisa Mobeto. DAR ES SALAAM: Mwanamitindo Hamisa Mobeto amedaiwa kuwa sehemu ya kupungua mwili kwa mwanadada mjasiriamali maarufu, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Kwa mujibu wa chanzo makini, tangu Mobeto aanze kuibua mjadala mtandaoni kuhusiana na mtoto wake kudaiwa kuwa ni wa bwana wa Zari, mjasiriamali huyo amejikuta akipungua mwili kutokana na mawazo aliyonayo. “Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi. Zari. “Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,” kilisema chanzo. Hata hivyo mwanahabari wetu aliingia kwenye ukurasa wa Instagram wa Zari na kujionea jinsi alivyopungua baada ya kuona picha zake mpya na kulinganisha na picha zake za zamani. Lic

Muigizaji wa Siri za Familia apata ajali

Image
Luwi Cappelo Muigizaji wa filamu Luwi Cappelo wa nchini Kenya ambaye ameigiza tamthilia ya Siri za Familia inayorushwa na East Africa Television, amepata ajali ya gari na kulazwa hospitali ya Pandya mjini Mombasa Kenya, katika chumba cha wa wagonjwa Mahututi. Mkurugenzi wa Jasson Production ambao ndio watengenezaji wa tamthilia ya Siri za Familia, Bw. Sanctus Mtsimbe, amesema kwamba mara ya mwisho aliwasiliana na Lui akiwa njiani kuelekea Mombasa kwenye harusi huku akiwa na wenzake, lakini baadaye alipata taarifa za ajali hiyo. Hata hivyo Siri za Familia zimetoa taarifa rasmi ya ajali hiyo kwenye ukurasa wake wa instagram, ukiandika...”Tumepata taarifa kupitia wenzetu wa Nairobi kuwa siku ya Jumapili saa 8 alfajiri, muigizaji wetu wa Siri za Familia msimu wa 4 kutoka Kenya Luwi na rafiki zake watatu, walipata ajali katika barabara ya Mombasa - Malindi wakiwa wanatoka kwenye sherehe ya harusi. Luwi alikuwa amekaa nyuma na aliumia, kwa sasa Luwi amelazwa Hospita

HESLB Yaongeza Muda wa Uombaji Mikopo Vyuo Vikuu

Image
Mkurugenzi Mkuu wa HESLB, Abdul-Razaq Badru. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa wanafunzi kuwasilisha maombi ya mikopo. Hatua hiyo imeelezwa inalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi walioshindwa kufuata masharti kuyakamilisha. Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema muda huo umeongezwa hadi Septemba 11 badala ya Septemba 4. “Tumesogeza mbele kwa siku saba zaidi ili walioshindwa kufuata vigezo wakati wa kujaza fomu wafanye hivyo,” amesema. Amesema hadi kufikia jana Agosti 29 , wanafunzi waliojitokeza walikuwa 49,282 lakini ni 15,473 waliokamilisha maombi kwa njia ya mtandao.

VANESSA MDEE NA JUX ACHENI KUTUZUGA!

Image
Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunizawadia pumzi yake ambayo imeniwezesha kuandika barua hii ya leo inayokufikia wewe msomaji ambaye pia umekuwa ukinisaidia kwa maoni na ushauri kuhusu safu yetu hii. Leo nina kazi ya kuzungumza na wanamuziki wawili ambao kwa muda mrefu, wametengeneza moja kati ya kapo bomba kabisa za wasanii wanaojihusisha kimapenzi. Unapozungumza kuhusu wasanii wanaofanya vizuri kwa sasa katika Bongo Fleva, huwezi kuwaacha kando Jux na Vanessa ambaye ni maarufu kama Vee Money, kwani hivi sasa ni miongoni mwa vijana wanaotupa uwakilishi mzuri kimataifa, kwa sababu kazi zake ni moto barani Afrika. Binafsi ninawakubali, maana mimi pia ni muumini mkubwa wa aina ya muziki wanaofanya. Maisha ya kimapenzi ya wasanii hawa siku za nyuma, leo yamenisukuma niseme nao kidogo, hasa kwa kuangalia matukio yanayoendelea hivi sasa kati yao. Uhusiano wao uliingia dosari kwa namna ambayo hakuna hata shabiki mmoja alitegemea, maana ni kama kitu cha g

Majambazi wateka basi, wapora madiwani

Image
MAJAMBAZI sita wameteka basi la Kampuni ya Safi na likitokea Kijiji cha Mamba wilayani Chunya kwenda jijini Mbeya na kisha kuwapora abiria jana. Miongoni mwa waliotekwa ni pamoja na baadhi ya madiwani waliokuwa wakielekea mjini Chunya kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha Baraza la Madiwani Maalumu kwa ajili ya kupitia na kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika jana. Akizungumzia tukio hilo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Ramadhani Shumbi aliyekuwa mmoja wa waathirika wa uvamizi huo, alisema tukio hilo lilitokea saa moja kasorobo asubuhi katika eneo la Loge. Shumbi ambaye ni Diwani wa Kata ya Mamba, alisema walipofika eneo hilo lililo na msitu mkubwa, walikuta kuna gogo kubwa lililolazwa na kufunga barabara na kisha walijitokeza watu sita mmoja akiwa amebeba bunduki na wengine mapanga na fimbo. Alisema watu hao walipiga risasi tatu hewani na kuanza kupiga vioo vya basi wakiwaamuru abiria washuk

Mawakili wamgomea Tundu Lissu

Image
MAWAKILI WA KUJITEGEMEA WAKITOKA MAHAKAMNI BAADA YA KUMALIZA SHUGHULI ZAO KATIKA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JIJINI DAR ES SALAAM JANA. MAWAKILI wa kujitegemea wamekaidi kutii wito wa Baraza la Uongozi wa Chama cha Mawakili (TLS) wa kutohudhuria mahakamani kwa siku mbili baada ya jana kujitokeza katika mahakama mbalimbali kutetea wateja wao. MAWAKILI wa kujitegemea wamekaidi kutii wito wa Baraza la Uongozi wa Chama cha Mawakili (TLS) wa kutohudhuria mahakamani kwa siku mbili baada ya jana kujitokeza katika mahakama mbalimbali kutetea wateja wao. Jumapili, baraza hilo kupitia Rais wa TLS, Tundu Lissu, lilitangaza maazimio matano likiwamo la kuwataka mawakili wote nchini kutohudhuria mahakamani na kwenye mabaraza kwa siku mbili, jana na leo, ikiwa ishara ya kupinga kuvamiwa na kulipuliwa kwa bomu kwa ofisi ya kampuni ya uwakili ya IMMMA jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita. Mawakili jana walionekana kukaidi wito huo baada ya kuhudhuria ma