Mbunge Mteule Viti Maalum CUF, Bi Hindu Mwenda Azikwa

Mwili wa marehemu Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda, aliyefariki nyumbani kwake Kibada Kigamboni ukiwasili makaburi ya Kisutu Dar leo.
Maziko yakiendelea.
Sheikh (kulia) akifanya  maombi baada mazishi.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (katikati) akiwa katika mazishi hayo.
…Akiongea  na wanahabari baada ya maziko.
HATIMAYE Mbunge Mteule Viti Maalum Cuf, Hindu Mwenda,  aliyefariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake Kibada Kigamboni amezikwa leo makaburi ya Kisutu Dar na mamia ya wafuasi wa chama chake na wananchi wengine wa Dar es Salaam.
Sheikh aliyeongoza mazishi hayo aliwahimiza wanachama wa Cuf kuendeleza upendo na kufanya kazi kwa ushirikiano ambapo miongoni mwao ni mwenyekiti wa chama hicho anayetembuliwa na Msajili wa Vyama, Profesa Ibrahim Lipumba.
Lipumba alimsifia marehemu akisema alikuwa anajituma katika kazi zake na alikuwa mwanachama shupavu na alikuwa mfano kwa wanachama wengine wanaokipenda chama hicho.

Comments

Popular posts from this blog